Nimuonavyo Anne Makinda na Baadhi ya Wabunge/Mawaziri wa CCM - Miswada ya Petroli na Gesi

MWANAKB

Member
Jun 21, 2015
51
18
Habari wanaJF,

Siku mbili zilizopita kumekuwa na purukushani ndani ya Bunge Tukufu la Tanzania.

Kilichofanyika wengi wetu tumekishuhudia na pia tumepata kutolea maoni sehemu mbalimbali.

kwa upande wangu namtazama spika wa Bunge, Mama Anne Makinda kwa sura ya huruma, Kilichotokea hakika naweza kukitafsiri kama hakuwa na jinsi!

Kifupi alionekana kuwa hakuwa na namna nyingine yoyote ile ya kuwezesha miswada hiyo kubarikiwa na "viti" vilivyomo ndani ya jengo la Bunge isipokuwa kwa kuwatoa nje walio kalia viti hivyo ili "viti" vibaki vikipitisha miswada hiyo.

Kwanini? jibu ni rahisi sana; WAKUBWA wameshaamua iwe hivyo! Siku zote hakuna wakumpinga BWANA MKUBWA! Ni nani ana ubavu huo!? yuko wapi ajitokeze!

Anne Makinda alijaribu kuwazuia walipotaka kulizima sakata la ESCROW; akapigana "ki uwoga uwoga" huku akitegemea zaidi sapoti ya wabunge wa pande zote mbili hatimaye kwa kupitia kwa Naibu spika kupitia kwa alichokiita kuomba ushauri wa wabunge, hatimaye sakata likafumuliwa na baadhi ya viongozi wakalipuka.

Hata hivyo kuna minong'onong'o isiyo rasimi kuwa naibu wa spika alipigwa adhabu kwa kuruhusu bomu hilo kulipuka wakati alikuwa na uwezo kulizuia! Angezuiaje wakati wabunge wa pande zote mbili walilishadadia?

Asingeweza kutofautia na wabunge wenzake wa upande wake! Sasa hili la miswada ya gesi na Petroli, Anne Makinda kakosa sapoti ya wabunge wa upande wake!

Waliolivalia njuga si wenzao, sasa angepitia wapi kutofautiana na WAKUBWA wakati WAKUBWA walisha viteka viti vyote vya BUNGENI! Viti vyote vimeshatekwa, sasa unadhani yeye angefanyaje? Jibu ni rahisi tu; Kuwatoa nje wale wote wanaong'ang'ania kukalia viti wakati viti vyote vimeshabukiwa na WAKUBWA na wanawakalisha hapo wanao wataka wao!?

Yamkini Wangejitokeza hata wabunge wa Upande wake watatu tu wa kuungana na hawa wengine wa upinzani, huenda Mama ANNE angejitutumua kusema neno kwani angepata la kujitetea kuwa "nilikuwa na wenzangu"! Sasa woooote, wanasema: Ndioooooooooooooooo!! Yeye ni nani aseme HAPANA!

Wananchi tumeliona hilo,wenye akili wamesha-note,walioruhusu mabwana wakubwa kugawana Gesi na Mafuta tena kama walivyogawana madini.

Zigo hiloo uliliweka mwenyewe madarakani kwa kulipigia kura au kwa kutoenda kupiga kura,sasa limejidhirisha muda mwafaka.

Sio mbali ni mwezi wa 10 tu unao uwezo kwenda kuliondoa...Umejiandikisha?

Usiendelee kulalamika,hayo yana mwisho mwezi wa 10 nenda kalitue zigo unalohisi limekulemea.
 
Jamani ,hebu edit umebabanisha mnoo. Hakuna aya, wala nukta.
 
Ukawa tujuzeni ubaya wa hii miswada,,acheni kupiga piga chenga

Hivi ndugu yangu asilimia 25 unaiona kubwa kweli kweli!Maskini nchi yangu.Haya na ile mikataba mibovu itaendelea kama ilivyo na masharti yake yatakuwa kama yalivyo,halafu eti ukweli na uwazi.Kaka ona kwa macho,sikjliza kwa makini yatafakari yote utapata jibu.Tumepigwa changa la macho na tuliowapa dhamana ya kutuongoza.
 
Hivi ndugu yangu asilimia 25 unaiona kubwa kweli kweli!Maskini nchi yangu.Haya na ile mikataba mibovu itaendelea kama ilivyo na masharti yake yatakuwa kama yalivyo,halafu eti ukweli na uwazi.Kaka ona kwa macho,sikjliza kwa makini yatafakari yote utapata jibu.Tumepigwa changa la macho na tuliowapa dhamana ya kutuongoza.

asilimia 25 ya nini hiyo? lete habari kamili.
 
asilimia 25 ya nini hiyo? lete habari kamili.

Ya mapato.Ni kama ile ya mrahaba wa asilimia 3 wawekezani asilimia 97Upo?Na hii ni hivyo hivyo.Asilimia 75 mapato ya mwekezaji na asilimia 25 ya serikali.Upo?
 
ccm CCM ni hatari kwetu... hima jiandikishe ...tuwang'oe kwa mustakbali wa taifa letu....
 
Habari wanaJF,

Siku mbili zilizopita kumekuwa na purukushani ndani ya Bunge Tukufu la Tanzania.

Kilichofanyika wengi wetu tumekishuhudia na pia tumepata kutolea maoni sehemu mbalimbali.

kwa upande wangu namtazama spika wa Bunge, Mama Anne Makinda kwa sura ya huruma, Kilichotokea hakika naweza kukitafsiri kama hakuwa na jinsi!

Kifupi alionekana kuwa hakuwa na namna nyingine yoyote ile ya kuwezesha miswada hiyo kubarikiwa na "viti" vilivyomo ndani ya jengo la Bunge isipokuwa kwa kuwatoa nje walio kalia viti hivyo ili "viti" vibaki vikipitisha miswada hiyo.

Kwanini? jibu ni rahisi sana; WAKUBWA wameshaamua iwe hivyo! Siku zote hakuna wakumpinga BWANA MKUBWA! Ni nani ana ubavu huo!? yuko wapi ajitokeze!

Anne Makinda alijaribu kuwazuia walipotaka kulizima sakata la ESCROW; akapigana "ki uwoga uwoga" huku akitegemea zaidi sapoti ya wabunge wa pande zote mbili hatimaye kwa kupitia kwa Naibu spika kupitia kwa alichokiita kuomba ushauri wa wabunge, hatimaye sakata likafumuliwa na baadhi ya viongozi wakalipuka.

Hata hivyo kuna minong'onong'o isiyo rasimi kuwa naibu wa spika alipigwa adhabu kwa kuruhusu bomu hilo kulipuka wakati alikuwa na uwezo kulizuia! Angezuiaje wakati wabunge wa pande zote mbili walilishadadia?

Asingeweza kutofautia na wabunge wenzake wa upande wake! Sasa hili la miswada ya gesi na Petroli, Anne Makinda kakosa sapoti ya wabunge wa upande wake!

Waliolivalia njuga si wenzao, sasa angepitia wapi kutofautiana na WAKUBWA wakati WAKUBWA walisha viteka viti vyote vya BUNGENI! Viti vyote vimeshatekwa, sasa unadhani yeye angefanyaje? Jibu ni rahisi tu; Kuwatoa nje wale wote wanaong'ang'ania kukalia viti wakati viti vyote vimeshabukiwa na WAKUBWA na wanawakalisha hapo wanao wataka wao!?

Yamkini Wangejitokeza hata wabunge wa Upande wake watatu tu wa kuungana na hawa wengine wa upinzani, huenda Mama ANNE angejitutumua kusema neno kwani angepata la kujitetea kuwa "nilikuwa na wenzangu"! Sasa woooote, wanasema: Ndioooooooooooooooo!! Yeye ni nani aseme HAPANA!

Wananchi tumeliona hilo,wenye akili wamesha-note,walioruhusu mabwana wakubwa kugawana Gesi na Mafuta tena kama walivyogawana madini.

Zigo hiloo uliliweka mwenyewe madarakani kwa kulipigia kura au kwa kutoenda kupiga kura,sasa limejidhirisha muda mwafaka.

Sio mbali ni mwezi wa 10 tu unao uwezo kwenda kuliondoa...Umejiandikisha?

Usiendelee kulalamika,hayo yana mwisho mwezi wa 10 nenda kalitue zigo unalohisi limekulemea.

Tukutane october..
 

Attachments

  • 1436202056937.jpg
    1436202056937.jpg
    25.6 KB · Views: 260
Ukawa tujuzeni ubaya wa hii miswada,,acheni kupiga piga chenga

Huna haja ya kuwa na elimu kubwa kujua viashiria vya hatari! Kwanini serikali ina nga'ang'ania kuijadili haraka haraka hivyo? Tena kwa dharura? kuna haraka gani kipindi hiki cha mwisho mwisho kama si kutengenezeana ulaji hapa! "...tabia ya ukweli ni kujitenga na ubay..." ipo siku mtajua tu kwanini walilazimisha iwe hivi ilivyokuwa.
 
Mleta mada nakushukuru sana kwa mada ilojaa umahiri ingawaje umechefua hapo uliposema.... Bunge Tukufu la Tanzania.Kiukweli hata kipofu atakubaliana na mimi kuwa hakuna utukufu ktk bunge la Tz hii haijawahi kutokea zaidi ya uozo tu wa walio wengi pale.Wameamua kumtumia Bi Kiroboto kutuzika tukiwa hai masikini waTZ!Mola azilaze roho zetu panapostahili kwa wema au ubaya wetu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom