Nimuelewe vipi huy demu,,au nimueke kundi gani ?

GHIBUU

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
4,432
3,006
Niwape story wananguuuu,,,,,

Nakumbuka nikuwa naishi tanga kwa muda nikipiga mzigoo,natoka asubuhi na usafiri wangu wa maringi mawili narudi jioni au usiku saa moja mbili hadi 8,kila siku mie ndio mbio zangu,sasa kulikuwa na njia sehemu hiyo ndio kila siku napita,kwa bahati nzuri aliletwa mtu mpya kazini kwa work experiance kazini kwangu,si unajua sura za kipemba zinafanana,aliekuja ni mtoto wa bso wangu tumefana sana sikutarajia.

Basi yule kija sijui alifikia wapi nikawambia njoo kwangu tukae wote kama upo kwa muda,tukawa wote asubuhi tunatoka jioni tunarudi,siku moja narudi kazini usiku nakuta msg kuwa nipige hiyo number kuna wanamke ananitafuta,nikashtuka, daaaaaah nimeuwa au nimetenda nini mimi,nikapuuza,siku ya pili tena nakuta ujumbee..

mi sikufatilia tena naendela na yangu,siku ya tatu nimepokea barua kunapicha na barua maelezo mengi ya mapenzi,sijui ananipenda na mengi zaidi,lakini barua imeandikwa jina la rafiki yangu ambaye tunaishi wote. alijichanganya,rafiki yangu akawa anaisukumizia mie mzigo,basi nikasema ngo basi asitusumbue huyu.

Mie nilichofanya ni kumuulizia,nikakutana na mtoto mmoja wa matanii kwangu mnyamwezi,wa kujinata,, hehehe nikamuuliza huyu mtu unamjua kanipa direction anayokaa demu,kumbe nikienda kazini napita kwao hapo huniangaliaa.

sasa siku moja nikapita usiku nikaita fulaniii kaitikia naaam nikasema njooo,hapo kwao kulikuwa na miti miti ikisha taa ya njee imezimwa kizaa,basi akaja akaniambia ooh baba yupoo baadae,,ah na mimi nikapuuza

Siku zikienda nasumbuliwa kila siku,basi kuna siku nikaamzukia tena wanaguu,nikamuona njee kwao mchana nikamwita njoo tuongee,basi akaja anaanza kualla mika oh mie nakupenda sana sijui hivi,sasa nikawa najiuliza madhumuni ya barua ni nani alimletea au tunamchanganya sura zetu,lakini poa haya tunaongea.

Kilichojiri mimi nikamuambia dada ombi nitakukubalia pindi ukifata masharti yangu,sawa,nikamwambia mimi hunijui unaniona tu,akasema ndio,nikamuambia mimi nimetembea na madada wengi sana,ivyo unavyonipenda wewe na ho walikuwa kama hivyoo,sasa cha kufanya kukuonea huruma bora mie nikapime HIV kwanza lakini nahisi tuende wote,ili tujue afya zetu then tuendelee na uhusiano huu,au unasemaje.

Akaniambia yeye hawezi,dah kwanini anasema yeye anaogopa hawezi,nikamuambia kama ni hivyo basi ,kuotkana mimi nakuonea huruma wewe nisije kuwa mie muathirika nikakumaliza wewe,bora twende wote tukashudie kachomoaa.

Sasa ndugu zangu watanzania wenzangu huyu demu alikusudia nini ? Kwa nini aliogopa kuenda kupima HIV ? AU LITAKA KUNIMALIZA KWA MAKUSUDI ? nimueke kundi gani mwanamke wa aina hiii..
 
Maswali ya nini sasa na mtu hataki kupima?? Piga chini endelea na mipango yako. Unajiuliza uliza nini sasa kuna muda wa kurisk maisha yako siku hizi???
 
sio wote wanakuwa na ujasiri wa kwenda kupima ongea nae taratibu muelimishe faida na hasara za kupima/kutokupima
 
Pole sana ndio maisha bana huyo demu atakuwa ana wasiwasi na njia zake alizopitia
 
Pole sana ndio maisha bana huyo demu atakuwa ana wasiwasi na njia zake alizopitia

Inawezekana kwa sababu demu alikuwa mzuri god bless her daaaaaamn.... Lakini moyo ulipiga konde niliogopa nikaona bora nijitoe kimaso maso tukapime wote duh.
 
Dah, siku hizi ukiona Binti anakufata fata inabidi uwe makini... Aisee pole sana!!!
 
Kaka anza tena na mita mia moja.. kama anakupenda si mkapime? yeye anataka muchakachue bila kupima.? achana naye endelea na shughuli zako mzee.
 
umefanya haraka kumuambia mkapime. ulikuwa umkubalie na kujipatia point 3 za vikisses na touches then ndo unakuja kumuambia. lkn kuwa bize kunamuepusha mtu na mengi...
 
Kwanza mdada, anajua jinsi ya kumkwepa mdingi wake...sasa inamaanisha nimtaalamu wa kutoka usiku.
2. Katuma barua kupitia kwa mashikaji...inawezekana ndio zake
3. Amekuona wewe mpole na hujui nendo zake....maanake alikopita si kwema sana
4. Yuko radhi awe na wewe hatakama umelala la mia.....maanake yeye yupo kikazi zaidi...

Jibu,
1. Msukume kwenda kupima, akigomaa kabisaa ........KIMBIA MBALI NA BARABARA TUMIA MAIN ROAD, asije kukubaka...ehehhe!!!
 
Nimepata tabu kuelewa haya maandishi yako..Unajua kuna baadhi ya watu swala la kupima ni gumu sana kwao kulielewa kutokana na woga
Endelea kumshawishi labda anaweza kukubali ..Lakini kama ataendelea na msimamo wake basi huna njia nyingine zaidi ya kufanya maamuzi yako binafsi + -
 
Kwa hiyo na wewe umempenda??
Hivi mwanaume akitongozwa yeye hazungushi zungushi eeh!! Yani hapotezi muda??
Haya muelewe kama Demu na umweke kwenye kundi la mademu!!
 
umefanya haraka kumuambia mkapime. ulikuwa umkubalie na kujipatia point 3 za vikisses na touches then ndo unakuja kumuambia. lkn kuwa bize kunamuepusha mtu na mengi...
sikufanya haraka unajua ningemvamia ningeshindwa kuzuiya hisia zangu,nafikiri suluhisho tosha ikiwa yupo tayari na mapenzi angekulai tukaenda kupima ,,,,,,mimi mwenyewe nilikuwa sijijui lakini nilikuwa na hakika niko poa,ila demu amenipa heart attack lool demu mzuri sana mtaani wote wanamzimia ila watu wa eneo waliniambia ni bahati sasa kwa nini aliogopa kupima..
 
Dah, siku hizi ukiona Binti anakufata fata inabidi uwe makini... Aisee pole sana!!!
Tena sana ila tuwe makini sote hata ma binti wawe makini na mimi nilikuwa makini sana,,kupima ndio vizuri zaidi tena kabla ya mazungumzo mukashindwa kuzuiya hisia zetu,zetu pia....sikukusea mazee au vipi ?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom