Nimrod Mkono na Mkono Advocates watch

Game Theory

Platinum Member
Sep 5, 2006
8,545
835
Hii ni spi-off thread toka kwenye ile ya ditto na naamini kuwa itakuwa ni changamoto ya kutazama jinsi LAW inavyokluwa practised pale Bongo na je katika mazingira haya kutakuwa na wanafunzi ambao wamemaliza shule lakini kila siku wao ni ma runner katika law firms

anyways back to MKONO kuna poster mmjona humu ndani kwa jina la DUA ameposti hii na nadhani it will get interesting as time goes


Mkono anastahili kuchunguzwa ili afukuzwe Bungeni
Sheria ambazo inawezekana amezivunja makusudi ni:

1. Watu wenye madaraka serikalini kukoma utumishi wanapochaguliwa. Sheria ya 1992 Na. 4 ib. 23 sheria ya 1995 Na. 12 ib. 14 (ambayo ni lazima iwahusu chief executives wa private firms).

2. Masharti ya sheria ya maadili ya uongozi wa umma

3. Masharti ya kazi ya wabunge sheria ya mwaka 1984 Na. 15 ib 13


Kamati ya uongozi & kamati ya katiba, sheria na utawala ndizo lazima zishughulikie suala hili kama ilivyoelezwa katika
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania as specified kipengele 4 majukumu ya msingi na ya jumla ya kamati.

Kifungu 4.1 Bunge na kamati zake ndiyo darubini (oversight or watch-dog organ) ya kuhakikisha kwamba mambo yote ya uendeshaji wa kazi za dola unafanywa kwa kuzingatia katiba, sheria na kanunu zilizowekwa.

Wajumbe wa kamati hii ni :

1. Mwenyekiti –Spika
2. Kiongozi wa shughuli za serikali bungeni
3. Kiongozi wa upinzani bungeni
4. Wenyeviti wa kamati za kudumu
5. Mwanasheria mkuu wa serikali

Hata kama itabainika kwamba hajavunja sheria kamati ya kanuni za bunge inaweza kufikiria na kutoa mapendekezo juu ya kufanya mabadiliko katika kanuni za Bunge – uchunguzaji huu utatokea iwapo taarifa ya kutoa pendekezo lolote na hususan hili hasa kutoka kwa wabunge wa opposition. (Mkono anafanya tenda nyingi kutoka serikalini na wakati huohuo yeye ni Mbunge)

Haya sasa wabunge wa upinzani hii ni changamoto kwenu. Tusikubali Mbunge kumtetea criminal.
 
Naam jambo la kwanza tukumbuke kulikuwa na mbunge Mabere Nyaucho Marando ambae nae ni wakili na alikuwa akimtetea wakili mwenzie anaetuhumiwa kumuua mkewe... then Spika wa Bunge Samuel Sitta bado ana law firm yake pale mjini mtaa wa Mirambo.

Ukiachia Spika wa Bunge ambae naamini kama msimamizi wa one of the organ of state nadhani sio kosa kwa hawa mawakili kuweza kutetea mtuhumiwa katika kesi mahakamani, tukumbuke mfumo wa tanzania unatambua kwamba everobody is presumed innocent until proven guilty by the court of law...

Sasa kwa hiyo Ditopile ingawa binafsi nina maoni tofauti na sheria inavyosema lakini nadhani katika mstari wa sheria bado ni mtu huru mpaka hapo atakapopatikana na hatia, the law can be an ass sometimes.. they say that in America.

Naam na kuhusu pendekezo la kwamba mbunge kwa vile yeye ni mtunga sheria basi inakuwa sio busara kuendelea kuwa mahakamani, nadhani hii ni debatable, je mbunge ambae nae pia ni wakili anaweza kuendelea kuwa wakili bila kuathiri ile concept ya kutofungamana na upande wowote na pia kutokuwa na maslahi binafsi, nadhani hapa tunarudi pale pale kwamba sheria za tanzania zina walakini mkubwa ukichunguza unaona kabisa kwamba kuna hatari ya bunge letu kutekwa na vikundi maslahi.
 
tafiti
Naunga mkono mawazo yako, kabla sijaongea zaidi naomba tu nieleweshe ni kivipi Mkono ni mtumishi wa serikali au ana madaraka gani serikalini.

Ninavyojua mimi wabunge siyo watumishi wa serikali. naomba nieleweshe kwa hayo machache kabla na mimi kutoa mawazo yangu.
 
Sam,
Hata kama angekuwa mtumishi wa serikali, ule upumbavu wa awamu ya pili wa azimio la Zanzibar unamwezesha kufanya hivyo. Kumbuka baada ya Zanzibar hakuna tena conflict of interest au maadili ya uongozi.
 
Pamoja na kwamba sijui mambo ya sheria zetu sawasawa, sidhani kuwa Mheshimiwa Mkono amevunja sheria yoyote. Sheria zetu za sasa zinawaruhusu viongozi kufanya biashara yoyote ile ikiwa ni pamoja na kuchukua zabuni za serikali bila kujali madarakla yao serikalini. Ni uozo kabisa ndiyo maana ni lazima katiba yetu ifanyiwe marekebisho ili baadhi ya vifungu vya azimio la arusha virudishwe. Uozo kama huu ndio uliokuwa unamfanya Mheshimiwa Sumaye kujichoteea maeneo ya ardhi kiholela.

Hata huko Marekani, viongozi wa serikali na wabunge wanatawaliwa na sheria zinazowazuia biashara zozote zianzoingiliana na wajibu wao kwa umma. Biashara ya uwakili inayofanywa na mbunge Mheshimiwa Mkono inaingiliana kabisa na kazi yake ya ubunge. Ni lazima aachie uwakili au aacahie ubunge. Lakini kwa sasa hivi hakuna sheria inayombana; kwa hiyo ana haki ya kutunga sheria yoyote yenye lengo la kutengua kesi ya mteja wake.

Kama kuna anajua ufafanuzi waMasharti ya kazi ya wabunge sheria ya mwaka 1984 Na. 15 ib 13 tafadhali atutoelee ufafanuzi wake. Ila najua kuwa mwaka 1996 wakati mabwana Masumbuko Lamwai na Mabere Marando wakiwa wabunge walimtetea mwenyekiti wao wa NCCR-Mageuzi Bwana Mrema kuhusiana na mojawapo ya mabomu yake. hakukuwa na pingamizi lolte kuhusiana na kesi hizo.
 
Ingawa sijasoma kabisa sheria, lakini najaribu kutafakari swala hili ki kawaida. Je, wabunge ambao wanapata riziki yao kwa kufanya biashara au wenye makampuni ya uzalishaji, wakiingia bungeni wanaacha shughuli hizo? mfano Diallo ambaye ni waziri na ana viwanda kadhaa, na alishakuwaga naibu waziri wa viwanda!

Je Mkono si ilikuwa ndio shughuli yake hiyo kabla ya kuingia bungeni. Mi nafikiri kama kazi yake hiyo haiingiliani kwa aina yeyote na mazingira ya kazi yake, na pia sheria hazipingi ufanyaji wake wa shughuli hizo, basi ni haki yake kuendelea kutafuta riziki yake. Pia mshtakiwa/mtuhumiwa huwa innocent mpaka hapo mahakama itakapobaini na kumhukumu kuwa ana makosa.

Hivyo Dito bado ni suspect au wanasema wenyewe "the accussed", kwani ni serikali ndio inayomshitaki.

Tatizo ni pale serikali ilipokuwa inatetewa na kampuni ya mkono kwenye kesi yake na Dawasa/au ile kampuni ya usimamizi maji ya Canada. Je serikali ilifuata utaratibu unaotakiwa katika kutoa tenda na kuweza hatimaye kuipa tenda hiyo kampuni ya Mkono au walimpa moja kwa moja nk.
 
Naam kwanza kabisa bwana Sam ni kweli kabisa Mbunge sio mtumishi wa umma, kwenye ile nadharia ya separation of powers/mgawanyo wa madaraka kuna mihimili mitatu ya dola SERIKALI/BUNGE/MAHAKAMA ambapo kila chombo kimoja kinatarajiwa kufanya kazi independent of the other ndio maana utaona viongozi wa kiserikali wakisema tuiachie sheria ichukue mkondo wake... nk lakini hili ni nadharia zaidi kuliko ukweli ulivyo manake ni rais ndio anaeteua jaji na mawaziri wanaowajibika kwa wabunge.

Hivyo coming back to your question, mbunge sio mtumishi wa umma ni muwakilishi wa umma, anapeleka bungeni mawazo yako na yangu kwa watendaji wa serikali to hold them to account, if we dont like his job we send there someone else.

Hivyo basi Mkono kama mwanasheria anahusiana zaidi na mhimili mwingine pia wa dola ie MAHAKAMA kwani wakili yeyote ni officer of the court mwenye haki kamili ndio maana wanatakiwa wawe na wasifu mzuri zaidi kijamii na any immoral conduct inaweza kuwaondolea nafasi yao ya kiuwakili.

Naam sasa tunaona kwamba Mkono ni:

A.MBUNGE -mhimili wa dola - bunge
B.WAKILI -mhimili wa dola-mahakama

Kwa hiyo kwa vile viungo hivyo vinatakiwa kufanya kazi huru basi kuna walakini katika kazi zake hizo mbili manake bila shaka ni kuingilia uhuru wa mahakama manake yeye ni mtunga sheria na msimamizi wa sheria kwa upande mwingine inakuwa ni vigumu, tukumbuke kuwa kwa nafasi yake ya uwakili anakuwa na sifa ya kuwa JAJI vile vile akiteuliwa na rais!

Lakini wapo wanaotoa hoja kwamba combination hiyo hapo juu ni sawa kwa vile Mawaziri nao ni

a. wabunge-mhimili wa dola -bunge
b. mawaziri-mhimili wa dola-serikali /executive

Lakini tukiangalia katika nchi nyingine mbunge hana matatizo kuendelea na kazi zake nyingine alizokuwa akifanya hapo awali, nitatoa mfano wa nchi niliyosomea sheria mimi binafsi UK, hapa mbunge hana matatizo kuwa mjumbe wa bodi, au kufanya biashara au kuwa wakili bali ni mwiko kwa waziri kuwa na biashara au kuwa mjumbe wa bodi fulani.

Lakini having said that, Mbunge anapokuwa mjumbe wa bodi yeyote ile anatakiwa kudeclare interest kwamba nina hisa au nina maslahi fulani katika taasisi fulani ili ijulikane bayana kabisa.

Namuunga mkono mjumbe alotoa hoja kwamba Mkono hajafanya kosa lolote ila tu in reality nadhani isingefaa kwake yeye kujiweka katika controversial cases kama hizi manake mimi na wasomaji wenye uwezo wa kuingia humu bila shaka wanaelewa kuwa dito hajawa mhalifu bado lakini kwa walio wengi wanaona kabisa kwamba ni muuaji, sasa kwa mwakilishi wa wananchi kumtetea ''muuaji'' haikuwa yenye kupendeza, nchi zilizoendelea mwanasiasa akiwa matatizoni kama DITO wengine humkwepa kuepuka bad publicity na mtu akifanikiwa kisiasa watu humkumbatia ili nao wanukie ujiko....tanzania sivyo!!

In conclusion nadhani kwangu nadhani sheria zetu zina mikanganyiko mingi, azimio la arusha was a good shot at trying to implement corporate governance procedures lakini kwa sasa hili azimio la zanzibar limeondoa vingi, unakumbuka spika msekwa aliwahi kuwa Mwenyekiti wa bodi ya VODACOM? Jaalia muswada uende bungeni ukiwa na maslahi na vodacom, yeye kura yake itaenda wapi?
 
tafiti
Nakubaliana na wewe kabisa sheria nyingi ni mauza uza. Hata lile swala dogo la mawaziri kuwa wabunge nadhani ni mauza uza tu.

Ni kivipi maziri anaweza kufanya kazi yake vizuri na kuwawakilisha wananchi wake? Tafiti, JK anakuja huko kwenye January nadhani this time around utatuwakilisha vizuri.
 
huyu tafiti akiingia tu basi wote inabidi mnyamaza

sawa sawa ndio maana ta kutafiti huko
 
Wakati kesi hii inaendelea kusikilizwa bunge linatarajia kujadili sheria ya makosa ya jinai na sheria ya adhabu hiyo (ni mfano tu).

Kati ya mojawapo ya hoja zitakazojadiliwa ni nadharia nzima ya kosa la kuua kwa kukusudia, madaraja ya mauaji, n.k n.k. Kwa vyovyote wanavyozungumza matokeo ya sheria hiyo yataathiri kwa namna moja au nyingine kesi inayomkabili Ditopile, swali: Je Nimrodi Mkono achangie kwenye mjadala huo bungeni?

Kwa vile nafasi yake kama Wakili mwenye kesi mahakamani haiingiliani na wajibu wake kama Mbunge (tukiwaamini baadhi ya watu humu!) ataruhusiwa kupiga kura kwenye mswada ambao matokeo yake yanahusiana na kesi anayotetea mahakamani?
 
Kichwa cha habari kinasema Mkono, achunguzwe ili afukuzwe bungeni, sasa swali ni kwa kosa gani hasa? Na ni sheria gani aliyoivunja? Ya bunge au ya mhakama?

Kama ni kuingia kwake kwenye hii kesi ya Blaza Dito, mimi ninasema kwamba ameingia kutokana na shinikizo la kikundi fulani cha siasa cha kutoka chama tawala yaani CCM, na akahakikishiwa kuwa haitaingiliana kabisaa na masilahi yake, kisiasa au kiu-wakili, na atalindwa, ndio maana ameingia kesi hiyo na pia ni pamoja na ARROGANCE!

Na the big message hapa kwa Prosecutors wa serikali kina yahe, ni kwamba mimi ni Mkono, don't you know who I am? na nipo hapa kumtetea Blaza Dito katika kesi ambayo nyinyi mnafikiri haiwezekani lakini remmember who I am, inawezekana ndio maana nimeingia, that is all! I mean hii ndiyo maana nzima ya Mkono kuingia kesi hiii, nayo ni ARROGANCE, ya kwake na waliomtuma,

Kuiweka hii issue ya Mkono, katika intellectuall realms, in academic debate ni kuwapa hawa viongozi waliomtuma Mkono na yeye mwenyewe ujiko wa bure ambao hawastahili na sio worthy a precedent au history, maana wanachotaka kufanya hapa ni uhuni ambao wameuzoea kama wa IPTL na Madini,

Ndugu zangu ninawaomba tuliongelee hili suala kama lilivyo nalo ni baadhi ya cviongozi wetu kutaka kumtumia Mkono kama njia ya mkato ya kumuokoa kiongozi muhuni mwenzao Blaza Dito, ndio ninasema ni viongozi wahuni tu ndio wanaoweza kujihusisha na hii kesi mpaka kuweka career zao online kwa ajili ya kesi ambayo, ukweli ni kwamba si kesi at all,

Kwa kawadia zetu za bongo, Blaza Dito anahitaji kukaa Keko, yaani Rumande for at least 5 to 10, years kabla kesi yake haijaimbwa mhakamani, anything less au different ni mpango tu wakutaka kuwayeyusha wananchi mchana kweupe, na sisi hapa kuanza kujadilii hii issue in a higher politics au kisheria, ni ku-fall kwenye mtego wa hawa viongozi wetu corrupt,

Mkono ni wakili na mbunge wa serikali, kwenye kesi ya high political profile kama hii ya Blaza Dito alitalkiwa kukaa pembeni, maana hata Supreme Court ya US, iliapa baada ya kesi ya kumpa urais Bush mwaka 2000, kwamba haitarudia tena kuchukua kesi za kisiasa na ndio maan ile kesi ya Senator Toricelli ambaye baadye alijiuzulu, mahakama hiyo ilikataa kujihusisha nayo, pamoja na kwamba inao wajibu kisheria kuzisikiliza ua kuzikataa,

Mbunge Mkono anao wajibu kisheria kukataa hii kesi au kuichukua, isipokuwa kuichukua kwake ilikuwa ni part of ARROGANCE, kama ya Blaza Dito kumpiga risasi dereva wa basi la dala dala, kwako Mbunge Mkono do all of us wananchi a big favor, jitoe katika hii kesi,

Halafu, Mkono mbunge ni part of serikali jana wabunge wamerejea toka Hong Kong, walikwenda kumuwakilisha nani serikali au wananchi? Mbunge yoyote wa kuchaguliwa na wananchi au rais ni mfanyakazi wa serikali, anawawakilisha wananchi bungeni kama dhamana ya kuchaguliwa kwake, lakini akishakula kiapo cha serikali kule bungeni basi ni mfanyakazi wa serikali, kwa hiyo Mkono ni mfanyakazi wa serikali, anapokwenda nje ya nchi na rais au mwenyewe anakwenda kuiwakilisha serikali, kwa hiyo anapojiingiza kwenye kesi kama hii, sisi tunaelewa kuwa ni ujanja tu unaotaka kufanywa ili watakapo muachia Blaza Dito waseme alitolewa na wakili wa kimataifa, utadhani Mkono aliwahi kumtetea mtu huko the Haque, au Arusha, kama enzi zile tulivyokuwa tukiambiwa Professor Malima ndiye aliyeamua masuala ya uchumi, huku tunajipanga foleni ya unga, lakini tunaambiwa ni Professor huyo!
 
Kwa mtazamo wangu, Mkono ni legislator, yeye hayuko upande wa mahakama (judiciary) wala hayuko upande wa serikali (rais na mawaziri) hivyo basi hajavunja sheria yeyote kuwa wakili.

Ukitofautisha haya mambo matatu: Bunge, serikali, na mahakama, utakuta Mkono ana kila haki ya kuwa wakili. Hata kama angekuwa waziri bado angekuwa hajavunja sheria kwa kuwa wakili, kwasabbu kati ya bunge, serikali, na mahakama, ni mahakama tu ndio ipo independent of government na bunge.
 
Mzee Ukimwi,

Ni juzi tu kwa mara ya kwanza ndio tumesikia kuwa bongo kuna mahakama ambayo inatakiwa kuwa chombo cha checks and balance against serikali baada ya kuamua kesi ya Mtikila na Independent candidates, ama sivyo hatujawahi kusikia mahakama ikienda kinyume na serikali, labda kidogo kesi mbili ambazo mapaka leo hatujui kama kweli uamuazi wa mahakama ulifuatiliwa na serikali nazo ni ile kesi ya viongozi wa BOT against Mkapa, na familia ya Kombe against serikali, otherwise mimi binafsi sikuwa ninajua kuwa mhakama ya bongo inapaswa kuwa ni independent of government,

Sasa swali langu kwako, mahakama hii ya bongo inawezaje kuwa huru wakati ikitegemea viongozi wake yaani majaji, kuchaguliwa na rais bila political confirmation system? Maana kama ninakuelewa hapa, ni kwamba tuna system kama ya US au UK, ambako judicial branch ni huru kuirekebisha serikali kila inapokwenda nje ya mstari wa sheria ya msingi yaani CONSTITUTION ya nchi, na kama alivyosema Mzee Madison kule US enzi zile ilipokuwa ikianzisha Supreme Court,

kuwa ".....mahakama kinatakiwa kiwe chombo cha kuwatetea wnayonge, yaani minority kutokana na massive power ya federal government, ambayo basically ni combine between Executive branch na Congress...."

Sasa huko majuu tunajua kuwa legislators ni watu ambao wako huru na serikali, juzi Obama alipokuwa Kenya hakuiwakilisha serikali ya US, bali ni interest zake mwenyewe as a individual, lakini hiyo siyo case hapa bongo, mbunge ni kiongozi wa serikali na ndio maana wanapobisha bungeni Waziri Mkuu huwaita na kuwakalipia kama watoto wadogo,

Sasa kwa watu wowote wastaarabu duniani ni suala la moral right, as opposed to sheria na rest kwa Mbunge Mkono kujiingiza katika hii kesi, ambayo upande mmoja una wanyonge yaani minority na upande mwingine wa mshitakiwa kuna political power tena massive one, ndio maana hata Mbunge Mkono akaamua kujitosa, ni njia wazi ya kutaka kuwaonea wanyonge hapa kwa kisingizo cha sheria, ingawaje nia na madhumuni hapa ni kujaribu kuwanyima haki wanyonge, yaani familia ya marehemu kwa visingizio vya sheria na separation of power, ni mamneno mazito kwa familia ya marehemu kuyaelewa au wanyonge kwa ujumla kuyaelewa, Mbunge Mkono kuwakilisha mshitakiwa ni wazi kabisa kuwa kuna Conflict of interest, ila tu kwa vile ni bongo inawezekana tu, lakini hatutalala kwenye hiii kesi!
 
Naam aliefungua mjadala huu nadhani aliweka wazi kwamba anataka mjadala ulenge katika kuangalia nafasi ya Mkono kama wakili as well as kama mbunge mwakilishi wa wananchi.

Kuna mjadala baina wa kujadili mwenendo wa kesi nzima upo hivyo hapa ni sahihi kabisa kuweka intellectual and coherent arguments za kueleweka ili tujue sheria zetu, sometimes binafsi yangu huwa ninaelimika kwa elimu ya humu ndani at least kwa kutekenywa mawazo nikatafute zaidi.

Mzee Mwanakijiji umeraise valid points kuhusu mjadala unaoendelea bungeni kuhusu makosa ya jinai, hapa ndio unaona pana walakini mkubwa kwa kweli manake Maoni yoyote ambayo wakili mkono atayatoa akiwa ndani ya bunge yanaweza kutafsirika kama ni mpangilio wa kutaka kuvuruga kesi. Ingawa katika hali halisi hilo haliwezekani manake kesi ipo mahakamani na inaamuliwa kwa exisiting laws hii ''sheria'' inayojadiliwa bungeni bado ni muswada tu itatake time kubwa mpaka kufikia kutumika mahakamani.

Mzee ES naona umejikanganya sana katika mjadala huu, ukijaribu kuelezea masuala mengi intellectually huku ukimix na conspiracy theories... sikubaliani na hoja kwamba wabunge ni watumishi wa serikali, no! kama alivyosema mwanzo hapo juu MGONJWAUKIMWI kwamba mgawanyo wa madaraka unaonesha wazi kuwa inaweza kukawa na inter-relationship lakini kamwe wabunge hawahusiani na serikali.

Mawaziri ndio the best example ya inter relation ilivyo, kwamba wao ni wabunge at the same time ni key players katika serikali, lakini then Mkono sio waziri angekuwa waziri bila shaka kazi ya uwakili ingekuwa on hold. Mzee ES wabunge kwenda nje kwac safari za kazi sio kuwa wawakilishi wa serikali kama ambavyo majaji kusafiri kwenda nje kikazi sio kuwa ni watumishi wa serikali, ndio maana Jaji Mohamed Chande wa Mahakama Kuu Mbeya yupo Israel hivi sasa akiwa anachunguza allegations za improper war conducts za Israel wakati wa mapigano yake na Hizbollah, hayupo huko kama mwakilishi wa serikali bali ni kama independent and impartial individual worthy of doing this job...

Ama kwamba Lowassa amekuwa akikaripia wabunge, I can appreciate the argument but I am not accepting it, hii ni paradox ya kichama kwamba waziri mkuu ana uwezo wa kuwaita wabunge wa chama wakakaa na kuamua hatuhoji kuhusu umeme, ni tatizo in its own right lakini haimanishi kwamba wabunge ni watu wa serikali....hii ni concept ya kwamba bunge linakaa kama chama, kama ambavyo wapinzania huamua kukacha baraza la wawakilishi kule zanzibar kwa msimamo wa pamoja, wakiamua kuhudhuria hawawi watumishi wa serikali...

Uhuru wa Mahakama? Naam upo kama hujajua hilo Mzee ES tafiti vizuri, manake umekuwepo from time immemorial manake ukiangalia tangu enzi za jaji Wolfgang Dourado kumekuwa na maamuzi mengi tu yanayokinzana na serikali:

1. Mwalimu Nyerere katika peak ya kushindwa kwake alisema wale wote wenye kumiliki mali,ni wahujumu uchumi, watu wakapitiwa majumbani wakikutwa na dawa za miswaki basi ni wahujumu, wakasekwa rumande, kesi ikaenda mahakamani, jaji akaidismiss kwamba hawana kosa la kujibu kwa vile Tanzania hakuna sheria inayohusu kuhujumu uchumi!

Nyerere akaitisha bunge haraka haraka ikatungwa sheria ya kuhujumu uchumi kesi ikarudishwa mahakamani, jaji Dourado akaidismiss tena na kuwaachia watu huru kwamba wamekamatwa wakati sheria ikiwa haiexist, the new suspect ndio watahukumiwa nao sio wale waliokamatwa awali.

Nyerere akaagiza sheria iwe backdated!

Naam mfano huo hapo juu unakupa maelezo ya namna mahakama ilivyo huru kufanya kazi zake ingawa ni kweli kuwa bado mabavu makubwa yanayotumiwa nac serikali lakini the elements and idea is there, yes wanateuliwa na rais lakini wana protection kwamba Rais akishawateua majaji hawezi kuwafuta kazi... good idea lakini kama ulivyosema tunahitaji kuona wakithibitishwa openly in a due process of the law lakini tunaona hata nchi nyingine ni waziri mkuu anaeteua majaji lakini kwa kushirikiana na jopo huru.
 
Wandugu mimi kama sikosei huyu Mkono ni Mwenyekiti wa:HIGHER EDUCATION STUDENTS LOANS BOARD (HESLB) ? Kumradhi kama nimekosea ila nakumbuka ana ama aliwahi kuwa na wadhifa fulani katika chombo kinachoshughulikia mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

Kama hivyo ndivyo na bado anaishikilia nafasi hiyo then ni mwajiriwa wa Serikali chini ya Wizara ya Elimu ya Juu.
 
Hata kama Mkono si mfanyakazi wa serikali, kwa position yake kama mbunge inamlazimu aone kuwa kuna conflicts of interests na biashara yake ya uwakili. Anaweza kuendelea na biashara hiyo kwa kutumia mawakili washiriki wake, lakini siyo yeye mwenyewe physically.

Again, katiba na sheria zetu ziko bubu kuhusu swala hilo, kwa hiyo kinachohitajika ni uamuzi wake mwenyewe. Nitatoa mfano mmja uliotokea mwaka 2000 huko Florida wakati wa uchaguzi wa rais wa Marekani uliomleta huyu jamaa wa ajabu madarakani. Baada ya kuonekana kuwa kura zile zina utata, Jeb Bush ambaye kisheria alitakiwa kusimamia shughuli zote za uchaguzi jimboni mwake alijivua madaraka hayo kwa vile mmoja wa wagombea alikuwa ni kaka yake. Hakuna sheria iliyokuwa inamtaka kufanya hivyo lakini busara ya kazi ndiyo ilimtuma kufanya hivyo ingawa aliendelea kumshughulikia kaka yake kutoka kwenye mlango wa nyuma. Mifano ya namna hiyo ipo mingi sana.

Ni kwa utaratibu huo huo kuwa Mzee Mkono alitakiwa asiendelee kujishughulisha na utetezi kesia mahakami moja kwa moja, na badala yake angekuwa anatumia wanasheria wake huku yeye mwenyewe akifanya kazi hizo kutokea mlango wa nyuma.
 
KICHUGUU

Upo right kabisa kwamba any reasonable person fikira yake ingekuwa kwamba hii kesi itamuharibia public standing lakini kwa Mkono kaona sivyo na yeye aingie kula ujiko, kama alivyoita ES hii ni arrogance kwa kweli.


Naam kuhusu utumishi wake serikalini, argument niliyokuwa najibu ni ile ya administrative law kwamba mbunge ni mtumishi wa serikali, kama ni mwenyekiti wa bodi ya mikopo then pana academic argument hapo kwa kweli kwamba ana presence serikalini, nahitaji kujua kama kapewa kwa vile ni mbunge au kwa vile ni mtu of public standing in the society, will be back...
 
Ieleweke kuwa hatuzungumzii Mkono kuwa wakili kwani hiyo ni fani yake na kazi yake, tunachozungumzia ni kuwa yeye kama Mbunge haikumpasa kwenda mahakamani kufanya kazi ya uwakili.
 
TTJ,

Mar Jaji Mwakibete nakumbuka alifukuzwa kazi na Mwinyi!!................pale ilikuwaje??
 
Ogah,
Mwinyi, kama kawaida yake alishauriwa vibaya. Rais hana mamlaka ya kumfukuza jaji.
 
Back
Top Bottom