Nimewasikiliza wabunge wa CHADEMA waliohojiwa na PCCB, yawezekana Lijualikali ni mwongo wa "Kutupwa"

Mmoja wa puppets ni johnthebaptist ambae anawavuruga akili wapambe wa Mbowe. Wanasahau kuwa pesa zilikatwa ili ziwekwe kwenye fixed account ili zitumike ajili ya uchaguzi.Sasa zimeyeyuka na aliyezichota anajulikana bingwa wa maigizo.
Mtagalagala mpaka mbaki kama mlivyo zaliwa na CDM itabaki kuwa juu juu juu zaidi. matumizi ya uwanja na trafic light chato hayajui mnajua ruzuku za CDM.
 
Huja msikia rais akibadilisha matumizi ya fedha za serikali tena bila kuidhinishwa na bunge?
Hivi nyie vichelema, mnamlinganisha Rais na mtu yeyote! Kwa taarifa yako Fedha yote ni mali yake kikatiba kama afisa masuhuli wa nchi hii. Hiyo bajeti inayosomwa ni yake
 
Uchunguzi bado unaendelea. Subiri majibu. Je kama zilichotwa baada ya kuhama?
Mbona mnasumbua watu kwa hisia? Jee kama, jee kama mpaka lini?
Tunataka ushahidi kama rule wa Gekule kumuomba katibu mkuu ccm mkopo 50M kwa barua (ambayo ipo JF) kisha Bashiru kuchenguka na ule upaja na kuamua kutoa 70M sio kama mkopo tena Bali kama ruzuku ya kumuwezesha mbunge kujikimu. Hizo ndio habari sio hekaya za Lijualikali kisha mnasumbua watu.
 
Mfano wa Nssf na pesa ya chama kwa akaunti maalumu ya uchaguzi haviendani
Pili deni lenyewe chama kilikopeshwa kwa mdomo kimabavu. Hii ni kwa mujibu wa Waitara. Ni deni hewa tu alilojitengenezea mwenyekiti. Hapa kuna mtu laziima aibike japokuwa alifanya maigizo.
Leta nyaraka sio eti kwa mujibu was Waitara.
Tunaposema mfano Gekule alipewa pesa za chama na Bashiru tunaonyesha nyaraka! Huo ndio mfano bora wa jinsi ya kutoa tuhuma
 
Mkuu umeeleza vzr. Somo limeeleweka. Katiba yao kama inasema hivyo pccb hawana lao labda wakamate KATIBA waiweke mahabusu kisha kisutu. Akili ya kushikiliwa
Hivi vila Laptop na 7G naona vinampongeza Mwenyekiti aendelee kupata Nguvu za kiume kwa Faru John
 
Huyu lijuamlizi hajaweza kuwa specific na matumizi mabaya kwa kuweka hata ushahidi.

Haona wananchi walihoji ununuzi wa bombadia umetumia bajeti gan na ulifuata taratibu zipi za manunuzi.?

Walau walionesha kitu halisi.

Sasa yeye watu wanahati inayordhisha ya ukaguzi wa hesabu afu unawatuhuhumu.
Ukiina hivyo ujue ni petty issues ambazo haziathiri chochote.

Tuendelee kunawa kwa maji tiririka.

Hakika huu ni ubazazi mtupu!
Kinachoendelea Kati ya TAKUKURU, CHADEMA na WABUNGE wake ni kudhihirisha UHUNI wa Serikali hii!
Michango mahali popote iwe ni ndani ya Serikali au Taasisi binafsi ya Kisiasa au Kidini inakubalika.
Hata Serikali huwa wanapitisha Michango including CCM wenyewe!
Sasa inapokuja TAKUKURU kuhoji Michango ya Wabunge wa CHADEMA kwa ajili ya KUIMARISHA CHAMA CHAO KULINGANA NA KATIBA YA CHAMA ni double standards na Ni Hila ya kuwachafua CHADEMA.

Tumeona Spika Ndugai akijimwambafy KUJENGA SHULE YA WASICHANA DODOMA KWA FEDHA YA MICHANGO YA WABUNGE WOTE!
Hii Ina tofauti gani na MICHANGO ya Wabunge wa CHADEMA?
 
Nyinyi watetezi wa chadema mnajitetea sana kwenye tope la tuhuma nzito.

Chama cha demokrasia na maendeleo kinachowatoza kodi viongozi wote kwa mgongo wa katiba ya chama, ambayo ni mbovu.

Suala la lijuakali sio michango.
Wala sio uhalali wa michango.
Huu ni upotoshaji.

Juakali anapinga matumizi ya fedha zinazokatwa kutoka kwa wabunge.

TAKUKURU haiwahoji wabunge kuhusu matumizi ya fedha. Bali inawahoji ili kujiridhisha kama kweli walichangishwa fedha hizo na hapo sasa.

MUZIKI halisi utaanzia kwenye ukaguzi wa matumizi ya halali fedha hizo,kama chama kinachopewa ruzuku ya serikali na ambayo ni fedha ya walipakodi wa nchi hii.
Hapo ndio jinai inapoweza kupatikana, jinai haiwezi kupatikana midomoni bali kwenye Documents za halali za orodha ya matumizi ya CHAGGA DEVELOPMENT MANIFESTO,
CHADEMA.na hili ndio haswa linalomfanya mwamba apige Faru john.
Mpaka kuanguka chakali.

Msijipe moyo mapema, mwenye album hii ni Mh mbowe mwenyewe sio nyinyi PUPPETS.

Acha uhanix wewe...!
Report ya CAG inaonesha hakuna matumizi mabaya ya Fedha za RUZUKU ndani ya CHADEMA! Michango ya CHADEMA NI KWA MUJIBU WA KATIBA YA CHAMA ILIYO RIDHIWA NA MSAJILI WA VYAMA!
 
"Nimalizie kwa kusema fedha yoyote ya taasisi huweza kubadilishiwa matumizi na hiyo siyo dhambi ndio maana hata fedha za bajeti zikifika serikalini zinaweza kubafilishiwa matumizi kwa nia njema tu ya kuleta maendeleo kwa haraka"

Mbona magufuli mnamlaumu kwa kutumia fedha bila idhini ya bunge?
 
"Nimalizie kwa kusema fedha yoyote ya taasisi huweza kubadilishiwa matumizi na hiyo siyo dhambi ndio maana hata fedha za bajeti zikifika serikalini zinaweza kubafilishiwa matumizi kwa nia njema tu ya kuleta maendeleo kwa haraka"

Mbona magufuli mnamlaumu kwa kutumia fedha bila idhini ya bunge?
Mabadiriko ya matumizi yanaruhusiwa, lakini yafuate taratibu zake.... lawama kwa Magufuli haikuwa kwanini kabadili, bali kwanini kazitumia bila kuidhinidhwa na bunge...
 
Definitely kama alivyosema Mwalimu Nyerere hao ni malaya hivyo watasema lolote wapate kula yao. Mtu unahama kwa ajili ya sera ama mission tofauti na ilivyopangwa na siyo kingne!
 
Na pesa ya chadema ni mali ya chadema.
Hivi nyie vichelema, mnamlinganisha Rais na mtu yeyote! Kwa taarifa yako Fedha yote ni mali yake kikatiba kama afisa masuhuli wa nchi hii. Hiyo bajeti inayosomwa ni yake
 
Back
Top Bottom