Nimewasikiliza wabunge wa CHADEMA waliohojiwa na PCCB, yawezekana Lijualikali ni mwongo wa "Kutupwa"

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,840
141,765
Nimwwasikiliza wabunge wote wa Chadema waliohojiwa na vyombo vya habari baada ya kutoka kwenye mahojiano na maofisa wa Takukuru.

Kwanza nilimsikiliza Lijualikali aliyedai wabunge wa Chadema wamepanga njama za kuidanganya Takukuru.
Nikakaa mkao wa kuwasikiliza wabunge wengine ili nibaini hizo njama.

Nilichogundua baada ya kuwasikiliza ni kweli wabunge wamekiri kukatwa fedha zao kwa ajili ya ujenzi wa chama na hiyo ni kwa mujibu wa katiba ya Chadema

Pili, makato hayo hukatwa na ofisi ya bunge chini ya Baraka za mh Spika na kuwasilishwa kwa Katibu mkuu wa Chadema.

Tatu, matumizi ya chama husimamiwa na Katibu mkuu na fedha za chama hutunzwa na mhasibu mkuu wakati matumizi ya chama huamuliwa na kupitishwa na kamati kuu ya chama.
Suzan Lyimo kwa mfano alishangaa wao kuulizwa maswali yaliyopaswa kuelekezwa kwa mhasibu kwani wao kama wabunge katiba inawataka kuchangia ujenzi wa chama siyo kupanga matumizi.
Suzan Kiwanga amedai makato yao hubsrikiwa na mh Spika.

Naye mbunge Pareso anasema kanuni ya makato huelezwa kuanzia day one unapojaza fomu ya maombi ya ubunge hivyo ni uamuzi wako kama hutaki usigombee.

Katika mazingira haya ni wazi makato ya wabunge wa Chadema yako kikatiba na matumizi yake huidhinishwa na kamati kuu ya chama.
Labda ndio maana CAG aliwapa hati inayoridhisha

Nimalizie kwa kusema fedha yoyote ya taasisi huweza kubadilishiwa matumizi na hiyo siyo dhambi ndio maana hata fedha za bajeti zikifika serikalini zinaweza kubafilishiwa matumizi kwa nia njema tu ya kuleta maendeleo kwa haraka.

Nawatakia Dominica yenye baraka

Maendeleo hayana vyama!
 
Nimwwasikiliza wabunge wote wa Chadema waliohojiwa na vyombo vya habari baada ya kutoka kwenye mahojiano na maofisa wa Takukuru.

Kwanza nilimsikiliza Lijualikali aliyedai wabunge wa Chadema wamepanga njama za kuidanganya Takukuru.
Nikakaa mkao wa kuwasikiliza wabunge wengine ili nibaini hizo njama.

Nilichogundua baada ya kuwasikiliza ni kweli wabunge wamekiri kukatwa fedha zao kwa ajili ya ujenzi wa chama na hiyo ni kwa mujibu wa katiba ya Chadema

Pili, makato hayo hukatwa na ofisi ya bunge chini ya Baraka za mh Spika na kuwasilishwa kwa Katibu mkuu wa Chadema.

Tatu, matumizi ya chama husimamiwa na Katibu mkuu na fedha za chama hutunzwa na mhasibu mkuu wakati matumizi ya chama huamuliwa na kupitishwa na kamati kuu ya chama.
Suzan Lyimo kwa mfano alishangaa wao kuulizwa maswali yaliyopaswa kuelekezwa kwa mhasibu kwani wao kama wabunge katiba inawataka kuchangia ujenzi wa chama siyo kupanga matumizi.
Suzan Kiwanga amedai makato yao hubsrikiwa na mh Spika.

Naye mbunge Pareso anasema kanuni ya makato huelezwa kuanzia day one unapojaza fomu ya maombi ya ubunge hivyo ni uamuzi wako kama hutaki usigombee.

Katika mazingira haya ni wazi makato ya wabunge wa Chadema yako kikatiba na matumizi yake huidhinishwa na kamati kuu ya chama.
Labda ndio maana CAG aliwapa hati inayoridhisha

Nimalizie kwa kusema fedha yoyote ya taasisi huweza kubadilishiwa matumizi na hiyo siyo dhambi ndio maana hata fedha za bajeti zikifika serikalini zinaweza kubafilishiwa matumizi kwa nia njema tu ya kuleta maendeleo kwa haraka.

Nawatakia Dominica yenye baraka

Maendeleo hayana vyama!
Watu makini wanaweza kutenda makosa lakini wakalindwa na mfumo.Kwa vyama vya siasa huwezi kuwa Katibu Mkuu na ukakwepa hoja za matumizi ya fedha.Kwa hili kama ilivyo kwa matapeli,Mashinji hawezi kukwepa hata kama kenda kutapika yote,mfumo unamuingiza lakini kama kesi ilivyofuta Songea na hili litapita kwani litamgusa asiyestahili kuguswa.
 
Juakali hakulalamika juu ya makato ya fedha kwani hilo swala lipo ndani ya katiba bali alicholalamika ni kubadirishwa matumizi ya hayo makato ikiwemo mwenyekiti kujikopesha na mpaka sasa chama hakina fedha ni vyema tusiwe na haraka kwani zote ni tuhuma tusubiri takukuru wamalize uchunguzi mbivu na mbichi zitajulikana
 
Kum
Juakali hakulalamika juu ya makato ya fedha kwani hilo swala lipo ndani ya katiba bali alicholalamika ni kubadirishwa matumizi ya hayo makato ikiwemo mwenyekiti kujikopesha na mpaka sasa chama hakina fedha ni vyema tusiwe na haraka kwani zote ni tuhuma tusubiri takukuru wamalize uchunguzi mbivu na mbichi zitajulikana
KumbE nikubadilishiwa matumizi tu,Mimi nilidhani anasema zimeliwa!!.
 
Mkuu umeeleza vzr. Somo limeeleweka. Katiba yao kama inasema hivyo pccb hawana lao labda wakamate KATIBA waiweke mahabusu kisha kisutu. Akili ya kushikiliwa
Lijua likali ni kijana hatari sana kwa mabadikiko katika Taifa. Kama ameweza kuwasema vibaya hivyo Chadema, chama kilicho pigania ubunge wake mahakamani kwa gharama, chama kilicho msimamia wakati akiwa gerezani hadi kikamtoa, na mambo mengi mengi.

Mwisho fadhila anazo zitoa kwa Chadema ni kuwatukana na kusema mambo yasiyo na msingi juu ya chama. Je siku aki wachoka Ccm ataicha salama? Maana mdomo wa kupayuka hata uujaze mkate utasema tuu.

Lakini Mungu akitaka agano lake litimie hutumia njia nyingi sana angalia hata wakati wa ukombozi wa wana wa Israel alimtumia Musa kuwaokoa. Toka Misri. Hata sasa hawa waropokaji wana tumwa Ccm ili andiko litimie siku Chadema itakapo inuliwa upatikane ushahidi wa matendo maovu yafanywayo na Ccm.
Akumulikiae mchana usiku hukuchoma.. Ccm waangalieni hawa wachawi mnao wapigia makofi leo na kuwapa air time. Muda ni wakati mzuri sana.
 
Juakali hakulalamika juu ya makato ya fedha kwani hilo swala lipo ndani ya katiba bali alicholalamika ni kubadirishwa matumizi ya hayo makato ikiwemo mwenyekiti kujikopesha na mpaka sasa chama hakina fedha ni vyema tusiwe na haraka kwani zote ni tuhuma tusubiri takukuru wamalize uchunguzi mbivu na mbichi zitajulikana

Takukuru hawafanyi uchunguzi, bali wako kwenye utekelezaji wa siasa chafu fullstop.
 
Back
Top Bottom