Cliffhanger
JF-Expert Member
- May 22, 2018
- 721
- 1,292
Nimeumia sana na jinsi hali ya kisiasa inavyoendelea hapa nchini.
Nimeumia zaidi kuona viongozi wa dini wanavyosifia serikali hii iliyojaa kila aina ya dhambi na kuacha kukemea mauaji, ukabila na uchama unaoshamili nchini.
Nimeumia sana kuona wasomi wenye elimu ya juu ambao wamesomeshwa kwa kodi za wauza uji na wauza karanga Tsh. 20,000 kwa mwaka na kodi mbalimbali wakisimama kutetea matumbo yao na kuacha haki ikiminywa.
Inaniuma sana kuona katiba ya jamhuri ikikanyangwa na wachache walioshika madaraka ya nchi hii kwa kuiba kura.
Naumia sana kuona jinsi gani nchi hii imekua ni nchi ya kufahamiana yaani kama hujulikani hauli matunda ya nchi yako.
Naumia sana kuona mapato ya serikali yanatumika vibaya kwa miradi isiyokuwa na tija kwa taifa iliyojaa dhuluma na upigaji wa hali ya juu.
WITO: Vijana tuna nguvu hii nchi ni yetu wote. Tupiganie nchi yetu tuliyopewa na Mungu.
Tuachane na hizi dini za kipuuzi zinazoshabikia uvunjifu wa haki. Tusiwape hela zetu kwa kisingizio cha sadaka. Ukitaka kutoa sadaka nenda kwa yatima na wajane ambao wametapakaa kila mahali.
The Gang of Three wamehodhi madaraka yote ya kuendesha nchi hii kiasi ambacho katiba haipewi umuhimu tena. Wanachotamka wao ndio katiba na sheria. Sijui Watanzania wote zaidi ya milioni sitini tumepatwa na nini mpaka watu watatu tu wanatupeleka puta!