Nimetishwa na Kauli ya Magufuli, Kauli Iliyotanguliwa na Udictator wa Ajabu wa Kutumia Polisi.

TL. Marandu

JF-Expert Member
Jul 12, 2015
3,625
5,807
Nikiri kuwa huko nyuma nilishawahi kuomba sana Vyama Vinavyounda Ukawa wampe Magufuli Ushirikiano, Kisha Nikaenda Mbali na Kusema Kuwa Magufuli ni Mtu Mzuri, Ila sasa Pasipo na Shaka kwa Tamko lake la Kidictator na Kinafiki sana, la Kuzuia Shughuli za Kisiasa ati mpaka baada ya Miaka mitano imenifanya Niwone Magufuli Kuwa Ni Mvunja katiba asiyejua Tofauti ya Shughuli za Siasa na Kampeni. Na Mvunja Katiba hakuna neno lingine la Kumuita hata kama tunataka kumpenda sana Kuvunja Katiba ni Uhalifu.

Tumeona Pia Magufuli akitumia Polisi, Kiharamu na Kihalifu, akiingilia sherehe, mikutano na vikao vya vyama vya upinzani kwa Visingizio vya Uwongo kama ilivyokuwa Kuzuia matangazo ya Bunge ya Moja kwa Moja ya TBC. Alipotumia Polisi Kuvamia Sherehe za wanachuo wa Chadema walidai kuwa kwanini walikuwa na sare na Bendera, lakini walipoona kuwa Hata Maafali ya CCM yalihusisha sare za chama na Bendera wakabadilisha maneno na Kusema ilikuwa ni kwa sababu ya Ugonjwa uliozuka Dodoma ingawa, mikusanyiko na sherehe za wengine ziliendelea kama kawaida.

Napenda Niwaase sana Watanzania, Msidanganyike na sijui Kutumbua majipu, sijui huduma za afya na elimu bure, Kwa asilimia 90% Magufuli ni Mnafiki wa Kutupa, Katika hili hana nia yoyote njema. Aeleze wazi Ni kwa Jinsi Gani Vikao, Sherehe, Mikutano, na Masikini hata Misiba ya Vyama vya Upinzani Vitamzuia Kufanya Kazi zake na Kutekeleza ahadi zake.

Amesema Pia na Nikamsikia Kuwa atashirikiana na Vyama vya Upinzani, Kivipi, kama haruhusu wakutane, wafanye Mikutano, au Watoe hoja Bungeni, atapata wapi mawazo yao? Atamtuma Mkewe akapate mawazo yao majumbani kwao au?

Pia Mh. Magufuli Amesema Kuwa ati hatamvumilia Mtu yeyote atakayemchelewesha,
Labda Nimuulize Maswali Kama 4,
1) Ni jinsi Gani Mazishi ya Alfonzo Mawazo yangemchelewesha Kutekeleza Ilani ya CCM?
2) Ni Kwa Jinsi Gani sherehe za Wanachuo wa Chadema kama zilivyokuwa kwa wahitimu wa CCM Zingememchelewesha Kuwawajibisha wezi wa Lugumi?
3) Ni Kwa Jinsi Gani Mkutano wa Zitto Ubungo au Mkutano wa Mbowe Mwanza Ungemchelewesha Kutoa elimu ya bure aliyoiahidi?
4) Ni Kwa Jinsi Gani TBC kutangaza matangazo ya Bunge live kunamchelewesha Kufuta Mkataba wa IPTL ambao kwa Kumtumia "Mbia hewa" ambaye hakuwa na Mtaji wowote akishirikiana na CCM waliwaibia Wananchi kwa Kulipa bili kubwa za Umeme Kiasi cha Kuwezesha hisa zao hewa zikafikia $ 75,000,000 ambazo walivuna kwa wire na pesa Taslimu za Magunia na Marumbesa. (Anitajie Mtu Mtaji wa "Mwakilishi wa Mafisadi IPTL, Uliomwezesha Kuvuna Kiasi hiki kwa niaba yao, maana aliwagawia kila mtu)
5) Ni Jinsi gani Maswali ya Tundu Lisu yanamzuia anayeshughulikia Wafanyakazi hewa ashindwe kuvunja Mikataba ya Kiwizi ya Mafuta, na Kuivunja Bank iliyotakatisha fedha za Escrow ya Stanbic, Kama Vile ilivyotaifishwa bank ya Meridian "Beyao" Bank miaka ile ya 90. Anijibu tu haya Mimi nitaona kweli ni, "Msema kweli" ha

Kama alivyosema Zitto Kabwe Mapema sana, Na Huyu Kijana Tunu na Shujaa wa Tanzania ni kama Nabii, Magufuli ni Dictator, Waliiba Urais kwa Kiburi Kikubwa kwa Kunyang'anya Computer, Wakafuta Matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar ambapo Maalim Seif alishinda, Walipoonda Wapinzani Wapenda amani wamekaa Kimya wakanusa Udhaifu.
Nimalize kwa Msemo usemao Mtu mwovu Ukimpa inch, hatasema asante, atachukua mile. Sasa ifike mahali Wapinzani tutathmini kama kweli tunataka kuendelea Kuwapa picha hii kuwa Sisi ni Dhaifu.

Kama Nelson Mandela, Naona kama tumefikia wakati wa Kuendelea Kukubali Kupigwa Mabomu, kudhalilishwa, Kuvunjiwa katiba juu ya Vichwa vyetu, pale ambapo tunataka Kushiriki Kwa Mujibu wa Katiba, Maswala ya Kuitumikia Jamii yetu, Kisiasa na Kiuchumi. Kama Magufuli na CCM hawataamua Kuwa na Busara na Kuitii katiba na Kujua hii ni nchi yetu sote, Watakuwa wamejidanganya sana. Na ndoto zao za Kutawala Tanzania miaka 100 kwa Nguvu na Mizengwe itageuka Jiinamizi.

 
Naona kama unajiumiza Sana huu mtandaoni mkuu. Ujasir huu ungepita nao mtaani coz waliomchagua hawaijui JF. Ila kwa sababu huna ubavu na ushawishi mtaani nakuonea huruma ipo siku utakuja kujiua kwa kihoro. Wajanja tumeling'amua hilo mapema ndio maana tumeziba midomo. JK is not like JPM.
 
Naona kama unajiumiza Sana huu mtandaoni mkuu. Ujasir huu ungepita nao mtaani coz waliomchagua hawaijui JF. Ila kwa sababu huna ubavu na ushawishi mtaani nakuonea huruma ipo siku utakuja kujiua kwa kihoro. Wajanja tumeling'amua hilo mapema ndio maana tumeziba midomo. JK is not like JPM.
Kama JF sio Sauti Kwanini Magufuli na Kikwete wanaisoma na Kwanini Watu kama Ninyi mnajishughulisha Kunyamazisha watu hapa. Wanafuata watu Mpaka Whatzup iwe JF, Asante Kwa Ushauri, Lakini keep it with you.
 
Uhuru Wa kutoa maoni ndio uliowafikisha wazungu na nchi ya Amerika kupigahatua,mwaka ambao Clinton alituhumiwa na kukutwa na kashfa ya ngono aliomba msamaha kwa raia waliomchagua.

Aftika kiongozi anapotafuta cheo hutumia maneno laini na kuwa chini ya sheria,akipata madaraka,waliompa hugeuka kuwa maadui wake milele.

Kauli hizo hats Congo,Uganda na Rwanda na Burundi zipo cha ajabu wameacha think tank yao wakategemea WB,UN,WHO na UNICEF wawatafunie mipango ya uchumi. Tudiwaruhusu watanzania kusema,wakawa sehemu ya maendeleo hatutapiga hatua katu
 
Nikiri kuwa huko nyuma nilishawahi kuomba sana Vyama Vinavyounda Ukawa wampe Magufuli Ushirikiano, Kisha Nikaenda Mbali na Kusema Kuwa Magufuli ni Mtu Mzuri, Ila sasa Pasipo na Shaka kwa Tamko lake la Kidictator na Kinafiki sana, la Kuzuia Shughuli za Kisiasa ati mpaka baada ya Miaka mitano imenifanya Niwone Magufuli Kuwa Ni Mvunja katiba asiyejua Tofauti ya Shughuli za Siasa na Kampeni. Na Mvunja Katiba hakuna neno lingine la Kumuita hata kama tunataka kumpenda sana Kuvunja Katiba ni Uhalifu.

Tumeona Pia Magufuli akitumia Polisi, Kiharamu na Kihalifu, akiingilia sherehe, mikutano na vikao vya vyama vya upinzani kwa Visingizio vya Uwongo kama ilivyokuwa Kuzuia matangazo ya Bunge ya Moja kwa Moja ya TBC. Alipotumia Polisi Kuvamia Sherehe za wanachuo wa Chadema walidai kuwa kwanini walikuwa na sare na Bendera, lakini walipoona kuwa Hata Maafali ya CCM yalihusisha sare za chama na Bendera wakabadilisha maneno na Kusema ilikuwa ni kwa sababu ya Ugonjwa uliozuka Dodoma ingawa, mikusanyiko na sherehe za wengine ziliendelea kama kawaida.

Napenda Niwaase sana Watanzania, Msidanganyike na sijui Kutumbua majipu, sijui huduma za afya na elimu bure, Kwa asilimia 90% Magufuli ni Mnafiki wa Kutupa, Katika hili hana nia yoyote njema. Aeleze wazi Ni kwa Jinsi Gani Vikao, Sherehe, Mikutano, na Masikini hata Misiba ya Vyama vya Upinzani Vitamzuia Kufanya Kazi zake na Kutekeleza ahadi zake.

Amesema Pia na Nikamsikia Kuwa atashirikiana na Vyama vya Upinzani, Kivipi, kama haruhusu wakutane, wafanye Mikutano, au Watoe hoja Bungeni, atapata wapi mawazo yao? Atamtuma Mkewe akapate mawazo yao majumbani kwao au?

Kama alivyosema Zitto Kabwe Mapema sana, Na Huyu Kijana Tunu na Shujaa wa Tanzania ni kama Nabii, Magufuli ni Dictator, Waliiba Urais kwa Kiburi Kikubwa kwa Kunyang'anya Computer, Wakafuta Matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar ambapo Maalim Seif alishinda, Walipoonda Wapinzani Wapenda amani wamekaa Kimya wakanusa Udhaifu.
Nimalize kwa Msemo usemao Mtu mwovu Ukimpa inch, hatasema asante, atachukua mile. Sasa ifike mahali Wapinzani tutathmini kama kweli tunataka kuendelea Kuwapa picha hii kuwa Sisi ni Dhaifu.

Kama Nelson Mandela, Naona kama tumefikia wakati wa Kuendelea Kukubali Kupigwa Mabomu, kudhalilishwa, Kuvunjiwa katiba juu ya Vichwa vyetu, pale ambapo tunataka Kushiriki Kwa Mujibu wa Katiba, Maswala ya Kuitumikia Jamii yetu, Kisiasa na Kiuchumi. Kama Magufuli na CCM hawataamua Kuwa na Busara na Kuitii katiba na Kujua hii ni nchi yetu sote, Watakuwa wamejidanganya sana. Na ndoto zao za Kutawala Tanzania miaka 100 kwa Nguvu na Mizengwe itageuka Jiinamizi.



Mkuu hata kama uko ulaya kumbuka kuna Interpol!Mie naogopa kusema zaidi

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Mkuu hata kama uko ulaya kumbuka kuna Interpol!Mie naogopa kusema zaidi

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
INTERPOL WA KAZI GANI NA MIMI? UNAFIKIRI WANAPENDA UMUGABE NA UIDIAMINI? Watu wanamsema Pope, Obama, Putin, tena kwa Uwongo, Nikasumbuliwe na Interpol Mimi Kwa Kumsema Mtu kwa Uhalifu wake ulio dhahiri dhidi ya haki za Kimsingi za Raia. Mnajidanganya sana, Katika Dunia Nii, Magufuli Ni Mtu Mdooooooogo sana! he is no body mwogopeni ninyi. Mimi Nitampa heshima kama Ninavyowaheshimu wanadamu wengine na sii zaidi. Kuwa Kiongozi hakumpi mtu, thamani au Ubora juu ya wanadamu wengine ni fursa anayotakiwa aipokee kwa kutetemeka na sio kujiona Mungu. Narudia tena Mh Magufuli ni Kiumbe kama Viumbe wengine na Siwezi kumwogopa au Kumwabudu. Mimi sihofu Polisi wa Niliko au Interpol kwa Kuwa Sijavunja sheria, Ila Niko Makini na Wanafiki kama Waliomfuata Kadegeya wa Rwanda na Kumuulia Hotelini South Africa. Kwa Hilo Niko fiti, Majirani zangu ni Maredneck, Nje ya Nyumba yangu Kuna Eneo Sensitive Kuna Sheriff officer 24/7 Mimi mwenyewe pamoja na Majirani zangu hatuitagi 911 Akija Mhalifu, well niseme wanapiga 911 baada ya jamaa kuwa historia. Kuna Mkuu mmoja wa Mkoa kachokonoa facebook yangu, akitaka kujiingiza kama Rafiki, Nimefuta Ombi lake, ila akijaribu tena Nitamriport FBI.
 
INTERPOL WA KAZI GANI NA MIMI? UNAFIKIRI WANAPENDA UMUGABE NA UIDIAMI. watu wanamsema Pope, Obama, Putin, tena kwa Uwongo, Nikasumbuliwe na Interpol Mimi Kwa Kumsema Mtu kwa Uhalifu wake ulio dhahiri dhidi ya haki za Kimsingi za Raia. Mnajidanganya sana, Katika Dunia Nii, Magufuli Ni Mtu Mdooooooogo sana! he is no body mwogopeni ninyi. Mimi Nitampa heshima kama Ninavyowaheshimu wanadamu wengine na sii zaidi. Kuwa Kiongozi hakumpi mtu, thamani au Ubora juu ya wanadamu wengine ni fursa anayotakiwa aipokee kwa kutetemeka na sio kujiona Mungu. Narudia tena Mh Magufuli ni Kiumbe kama Viumbe wengine na Siwezi kumwogopa au Kumwabudu.


Jitahd kutokwa povu, ....... Haishi kutapatapa
 
Ulipokuwa unaandika thread hii ulikuwa mpakani? Maana uongozi tulionao wakati huu si wa kuwaambia ukweli, ukiwa mkweli unakuwa adui.

Anyway Mimi nikikumbuka kipindi cha kampeni nilikuwa mpinzani mkubwa wa baba J ila asilimia kubwa waliomuunga na kumchagua ni wale ambao hata mlo mmoja kwao ni tabu, walikomaa na wimbo "acha waisome nambaa eeeh sisiem mbele kwa mbeleee" sasa tuache kilanja aendelee kuvurunda tuone nani ataisoma namba.
 
mkuu mi sina hata masaa matatu.ndio nimeachiwa Leo nilikula ban,humu sikuhiz wanataka usifie tu usikosoe,ukikosoa ni sawa na kumtongoza Mama mkwe
Hata mimi Nilishakuwa banned lakini kwa Sehemu ilikuwa Ni Makosa yangu Mwenyewe, Niliingia kwenye Malumbano na WanaCCM wanakaa hapa kwa Lengo la Kuanzisha hoja za Kupotosha oh Mbowe hivi Chadema Vile. Mmoja akaleta Mitusi yake Nikamfyatua wakanifungia. Na Pia Nimeshawahi Kufutiwa Hoja zangu, Jana Tu Nimefutiwa Moja, Lakini In average bado nadhani wako fair sana. Nao Ujue wanaandamwa kwa hiyo they are watching their back!
 
Back
Top Bottom