Nimetishiwa Maisha au?...

Status
Not open for further replies.

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,929
Katika ukurusa wa comments kwenye KLH News.. kuna mtu kanitumia ujumbe huu akijibu hoja zangu kuhusu "Mashariki ya Kati: Tanzania tuko Upande Gani?"

Anajiita "Statesman"

"Yap in response to ur intro... unasikitisha maana unataka kucheza ngoma usiyojua mwisho wake.Raisi Busha baada ya milipuko ile na ile ya WTC akatamka wzi kama ' Either uko na USA au uko na Magaidi'sasa unataka kutueleza kama for the past about 10 years Mkapa (Mkristo) kama Raisi Tanzania ilikuw upande mzuri n a sasa baada ya Kikwete (Muislamu) ina chagu upande wa magaidi. Kijana be carefully we are reading between your line of argument. Unajua kauli zako hizi zitaleta implication mbaya kwenye jamii na kusababishwa nchi kutengwa?Mimi nadhani Serikali ya Tanzania ilishatoa msimamo wake ambao ni kulaani pande zote kwa kuendeleza mapambano na kuua raia wasiokuwa na hatia. Haikusema kama upande upi uko right. Angalia PRESS RELEASE YA WAZIRI ASHA. Ama kuhusu waandamanaji kuegemea upande mmoja wa wanamgambo wakiislamu wa Hizb huwezi ku sema kwa serikali kuruhusu maandamano yale ndo imechagua kuwa upande wa Magaidi. London nasikia yalifayika mandamano kama yale kupinga Israel na huwezi kusema kama British Government iko upande wa Magaidi.

Sasa to make the story short toa apology yako kwa Serikali kabla mkono mrefu wa serikali haujakufuata hapo ulipo."

Sijui kama amedhamiria kuninyamazisha, kunitisha au anajifurahisha.. anyway, nimempa jibu lake kama alivyotaka na zaidi. Hata hivyo show ya leo imekuwa rated PG 13
 
Kichaa huyo achana naye analeta enzi za JKN za kutumia hela nyiingi za wananchi kwa ajili ya usalama wake na serikali huku akiita usalama wa taifa!!! Kiini macho. Kwanza akija muwahi yeye kabla hajakuwahi.
 
Huyu jamaa anaonekana kuwa ana lake jambo .Wewe una haki ya kusema mawazo yako na mgogoro wa Mashariki ya Kati kwanza Tanzania kuongelea ni kupoteza muda .Tanzania tuna nafasi gani kwenye mgogoro ule ?Kauloi ama tamko la Serikali limenishangaza na najiuliza kama kweli tuna lolote hata kufanya ikiwa ni pamoja na maandano ya Waislam wa TZ ambao uelewa wao ni mdogo sana .Waliandamana na kuchanga pesa kuwapa magaidi wa Hamas kuendelea ugaidi wao na Hezbollah lakini tu crisis nyingi Africa we never heard of Arabs in the street in our support .Huu ni ujinga kuanza kuingilia mambo ya Middle East tunaacha shida zetu Tanzania .Endelea kutupa maneno .
 
Najua hivi vitisho hatimaye vingetokea.. lakini kwa sababu ya Mashariki ya Kati..ndo vimenishtua... nimezungumza mikataba.. viongozi duni..n.k hakuna aliyesema kitu ila kugusa Mashariki ya Kati.. "Mkono Mrefu wa serikali" unatishiwa kunyoshwa dhidi yangu!!! Hivi Mashariki ya Kati haizungumziki? Hivi mtu hawezi kuwakosoa Waislamu bila kuonekana kibaraka wa Marekani?
 
Mzee Mwanakijiji
Unaonekana kuogopa sana lakini nasema haya ni kawaida hakuna mkono wa srikali wala nii huyu kaamua kukunyamazisha kwa ujahidina wake .Sisi tuko hapa huyo ni Mullah ama kibaraka wa Hassan Hezbollah anakutisha endelea kusema mawazo yako na sirikali ni watu na sisi tutakulinda sema bwana .Kwani mashariki ya kati ni Tanzania ?Kama sirikili ina interest na mashariki ya kati bila ya sisi watanzania kujua basi ni muda tujue .Mzee wa Kijijini kumbuka kwamba waandishi wa habari wako kapuni hawasemi la maana juua ya Tanzania , maisha ya watanzania , bunge na siasa zetu ila masifu kwa uongozi .Hawawezi hata kuhoji Nazir Kirimagi na statements ambazo zinamu implicate rais na wawekezaji lakini wanatamani kukutisha kisa umesema mawazo yako .Tunasema the hell no bakuna mkono wa vitisho
 
Mzee Mwanakijiji
Nimesoma maandiko yako na haya huyu mtu anajiiita wa serikali nimegundua ni mmoja wa washabiki wa rais wa Iran na Hezbollah ameamua kukutokea uvivu.Huyu ni Mjahidina tu naweza kusema na hana hoja .Anataka kutumia vibaya madaraka yake kama kweli yuko serikalini lakini tunamkumbusha kwamba cheo ni dhamana na kesho tutamuuliza mambo yakiiva .You need as we do to practice freedom of speech and expression with no fear .Tutakuwa na wewe hadi mwisho hii ni vita dhidi ya ustaraabu naweza kusema .
 
Chifu.. ama sivyo watanitafutia sababu ya kufuta uraia wangu na kunifukuza nirudi kijijini kwetu....!!!
 
Huyu alikuwa one of the loosers anayedhani kuwa na madaraka na kuchanganya ujahidina wake vitasaidia sana kuwabana watu .No wewe sema tuone mwelekeo na kama natakakufuta Uraia basi afute tuone .Ishu ya Middle East tangu lini ilikuwa na nguvu Tanzania ama ndiyo anataka kusema Rais ni mwislam kwa hiyo nguvu zote kwa Waislam ? Kama anataka kuhabarisha hilo basi sawa tunangoja kuona mwelekeo maana hakuna mtoto mdogo hapa .
 
Mzee Mwanakijiji,

Bravo! Weka vitu hawa hawa ndio walionitisha kuhusu Mahita, na ile habari ya Mkapa kuchukua dola millioni moja kwa ajili ya uchaguzi wa awali Dodoma,

nimeisoma hii posting kwa haraka, isipokuwa badaye nitaikalia chini na kuifafanua, ili kujua kama kweli imetoka serikalini,

isipokuwa tu kwa haraka haraka, "mkono wa serikali" hautumii maneno cheap kama "Busha" kwa kumaanisha George Bush, hapo tu ninaamini kuwa kuna mzee mmoja ambaye ni mwanachama wahumu ndani na anajulikana kuwa ni MUJAHADINA, ndiye amebadili jina na kujiita statesman wa Busha, pumbavu mkubwa!

Nitaisoma kwanza yote tena na kumrudisha mawe huyu mzee Busha Stateman!
 
Mzee Mwanakijiji,

Tayari nimeisoma kwa makini hii posting, ukweli ni kwamba imeandikwa na mdini anayejali kuwa Mkapa, alikuwa mkristo, anayefuatilia kwa makini issues za kidini mpaka anajua kuwa kulifanyika maandamano London,

Halafu mwishoni anakutishia kwa kutumia jina la serikali, ya kwamba yeye ni usalama au shushu! Mikataba ya IPTL imemshinda huyu Statesman na usalama yake na mkono wa serikali yake!, City Water imemshinda! Manji amewashinda! Madini ndio hivyo yanachukuliwa kama hayana mwenyewe,

lakini yeye na usalama yake wanamuda wakufuatilia kwa makini hizi forum! What a mkono wa serikali, it is a big joke mzee Statesman! Hatukutengwa kwa kuwaua Waisilamu pale Mwembe chai bila sababu, lakini tutatengwa sasa kwa sababu ya maoni ya Mwanakijiji?, hatukutengwa kwa kuwaua wananchi kule Pemba bila sababu, tena Waisilamu, lakini tutatengwa kwa sababu mwanakijiji ametoa mawazo kwenye forum?

Hatukutengwa wakati gazeti la African Confidential liliposema kuwa rais wetu anapewa hela za uchaguzi na IRAN, lakini tutatengwa sasa kwa sababu ya Mwanakijiji,

Mzee Mwanakijiji, weka vitu huyu tena tumeshamjua ni nani huyu, hana lolote ni debe tupu hilo, yaliyojaa yaani usalama wenyewe kina Ubwete, huwa hawatishii watu humu! Weka vitu!
 
Yes sir!!! Labda alitarajia nitajiuzulu.. bado nina pumzi na kama nyinyi wenzangu tutaendelea kuzunguza wazi yale yagusuyo Taifa letu!!?
 
Yes sir!!! Labda alitarajia nitajiuzulu.. bado nina pumzi na kama nyinyi wenzangu tutaendelea kuzunguza wazi yale yagusuyo Taifa letu!!?
Vitisho vipo na vitashindwa na kulegea........na hii kuelekea 2010 kila mtu anataka kujitakasa mbele ya wapiga kura......na watu makini kama sisi ndio tunawindwa...
 
Mwanakijiji mzee mwenzangu,watu kama hawa huwa hawakosekani kwenye jamii yeyote msameheni bure maana katoa mawazo yake kama mchangiaji mwingine yeyote.
 
Katika ukurusa wa comments kwenye KLH News.. kuna mtu kanitumia ujumbe huu akijibu hoja zangu kuhusu "Mashariki ya Kati: Tanzania tuko Upande Gani?"

Anajiita "Statesman"

"Yap in response to ur intro... unasikitisha maana unataka kucheza ngoma usiyojua mwisho wake.Raisi Busha baada ya milipuko ile na ile ya WTC akatamka wzi kama ' Either uko na USA au uko na Magaidi'sasa unataka kutueleza kama for the past about 10 years Mkapa (Mkristo) kama Raisi Tanzania ilikuw upande mzuri n a sasa baada ya Kikwete (Muislamu) ina chagu upande wa magaidi. Kijana be carefully we are reading between your line of argument. Unajua kauli zako hizi zitaleta implication mbaya kwenye jamii na kusababishwa nchi kutengwa?Mimi nadhani Serikali ya Tanzania ilishatoa msimamo wake ambao ni kulaani pande zote kwa kuendeleza mapambano na kuua raia wasiokuwa na hatia. Haikusema kama upande upi uko right. Angalia PRESS RELEASE YA WAZIRI ASHA. Ama kuhusu waandamanaji kuegemea upande mmoja wa wanamgambo wakiislamu wa Hizb huwezi ku sema kwa serikali kuruhusu maandamano yale ndo imechagua kuwa upande wa Magaidi. London nasikia yalifayika mandamano kama yale kupinga Israel na huwezi kusema kama British Government iko upande wa Magaidi.

Sasa to make the story short toa apology yako kwa Serikali kabla mkono mrefu wa serikali haujakufuata hapo ulipo."

Sijui kama amedhamiria kuninyamazisha, kunitisha au anajifurahisha.. anyway, nimempa jibu lake kama alivyotaka na zaidi. Hata hivyo show ya leo imekuwa rated PG 13
Unatishiwa unaelezwa kwani wewe ni nani si mtu tu wa kawaida endelea tuone hao jamaa zako wanaokuunga mkono kama watakusaidia utakapokuwa segerea
 
Wewe unataka kubishana na internet thugs wasiojua kuandika sentensi straight?
 
kwanini msimtaje jamani?
mkuu FMES,mchane laivu tuanze kumshambulia
 
kMkuu Mwanakijiji kwani are you scared? If not then you have nothing to worry about. Lakini nakushauri tu mkuu kuwa makini because mtu huyo katuma ujumbe kupitia alias yake so you don't know what authority the person has to say what they said. I can't say if the person is making empty threats or not but once people are worried about what you say then the message is reaching them and touching them.
 
Last edited:
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom