Nimetazama dakika 45 ya Mhe. Mwigulu Nchemba -Waziri wa Fedha jana jumatatu nimemuelewa katika haya

Koryo2

JF-Expert Member
Nov 28, 2016
2,056
2,515
Dakika 45 za Mhe. Mwigulu Nchemba nilisikiliza kwa umakini mkubwa na baadaye nimekubaliana naye juu ya tozo ya miamala ya simu kwa sababu zifuatazo:- (1) Alitamka wazi kuwa makato yanayoelezwa na watu kuwa ni kubwa ni upotoshaji.

Yeye alisema kama mtu atatuma mathalani Tshs.1,000,000 makato yake yatakuwa siyo zaidi ya Tshs.10,000 ambayo kwangu naona ni sawa. (2) Makusanyo haya yanaenda kugharamia ujenzi wa madarasa, vituo vya afya, Mabweni ya wasichana kwa kila Mkoa.

Kwa maelezo yake sioni ubaya wowote. Nchi inajengwa na wenye nchi hivyo kama wananchi inatupasa tujenge nchi yetu.

ANGALIZO:- Sisi kama wananchi tunataka makusanyo haya mwisho wa siku yatolewe taarifa na kazi zilizofanyika na Serikali kuonyesha kila mradi uliotekelezwa kinyume cha hapo hatutakubaliana na maelezo ya Mhe. Waziri.
 
Kwa hiyo kabla ya tozo ya uzalendo madarasa yalikuwa hayajengwi? vituo vya afya havikujengwa, mabweni ya waschana yataanza kujengwa leo kwa tozo ya madelu? huna akili...pumbav.
 
Naomba unijibu! ni kwa nini kwenye line za simu tuu( makampuni ya simu ) ndo kodi ya uzalendo ilipo! na Cyo kwenye mabenki??. Na kama kweli ni uzalendo, kwa nini mawaziri, makatibu, wa RPC, na wengineo wasitembelee magari ya 120mil na kwenye ngazi za mikoa na wilaya wawe below 60mil ?? Kwani tatizo liko wapi?? , Hapo ndipo tutaona uzalendo kwa wote.
 
Kama yeye waziri angekua mzalendo kweli na ana nia ya dhati kweli ya maendeleo angeanza na paye kwa wabunge, angepunguza kiinua mgongo kwa wabunge wanazolipwa zaidi ya 200m kwa miaka 5 zaidi ya mwalimu wanaofanya kazi kwazaidi ya miaka 30 lkn kiinua mgongo ni kidogo, wangepunguza posho za wabunge au kuondoa kabisa, wangepunguza matumizi ya v8 na misafara, kupunguza wabunge wa kuteuliwa na viti maalumu.

Alafu watuambie kwanini matumizi ya kawaida kwenye bajeti ni makubwa kuliko matumizi ya maendeleo maana tunaweza kuongeza tozo na Kodi kandamizi kwa mwananchi masikini kwenda kugharamia maisha ya anasa ya viongozi. Watanzania tunaipenda nchi yetu na hatukatai kutoa Kodi na tozo kwaajili ya maendeleo
 
Dakika 45 za Mhe. Mwigulu Nchemba nilisikiliza kwa umakini mkubwa na baadaye nimekubaliana naye juu ya tozo ya miamala ya simu kwa sababu zifuatazo:- (1) Alitamka wazi kuwa makato yanayoelezwa na watu kuwa ni kubwa ni upotoshaji. Yeye alisema kama mtu atatuma mathalani Tshs.1,000,000 makato yake yatakuwa siyo zaidi ya Tshs...
Ujinga mtupu hiyo kodi ya Uzalendo mbona alivyokuwa hai JPM hatukusikia kodi ya ushuzi huu. CCM ni wezi maana waliwapiga Wajasiriamali kwa vitambulisho fake sasa wanakuja na eti kodi ya mshikamano kwanini hao Wabunge wasianze kukatwa kodi huu nu uzwazwa wa hali ya Juu. Ila nafurahi wehu wote wanaoiunga mkono CCM nao wanaungua na huu moto.
 
Kadanganya.

Kutuma 1000000-300000:makato ni 5000 tozo ni 9400 jumlani 14400

Ulientumia akitaka kutoa makato 6000 tozo 9400 jumla 15400

Viwango ni vilubwa sana
 
Tuliaminishwa na Serikali ya awamu ya 5 kuwa nchi hii ni tajiri sana. Wengi wetu tulielekeza fikra zetu katika utajiri wa rasilimali - madini, sekta ya utalii na ardhi. Sikutegemea kuona kuwa ujenzi wa madarasa, wodi etc utegemee kodi za miamala ya simu.

- kuna sababu zipi za msingi. kushusha kodi kwenye vileo(bia) na kupeleka vilio kwenye mafuta na tozo za miamala ya mawasiliano?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom