Nimetapeliwa Pesa kupitia Account ya NMB

Azarel

JF-Expert Member
Aug 25, 2016
26,052
33,900
Habarini wadau,

Ninaomba msaada kwa anayeweza kunisaidia, nilipoteza kadi yangu ya NMB bank, nikaamua kujaza loss report tangu Oktoba mwaka jana kwa njia ya online. Niliambiwa kuwa malipo yamekamilika hivyo nikacomfirm polisi, sikwenda ku-comfirm sasa juzi kushinda jana ikanijia meseji kuwa shillingi 2000 imekatwa kwenye kadi namba yangu inayoishia na xxxx lakini baadae hela hiyo ikarudishwa.

Leo usiku huu nimepata tena message kuwa hela yangu 81000/= imekatwa kulipia huduma flani ya Inked in (sio LinkedIn) na Google Tempo. Wakati sijajiunga na huduma yoyote ile ya malipo ya mtandaoni.

Naomba sana mwenye kuweza kunisaidia anipe mwongozo nianzie wapi kwasababu nimetuma msg ya UTAPELI kwenda polisi hawajajibu.

NASHUKURU
 
Chukua ushauri wa chief hapo wahi asubuhi branch ili wazuie online transactions kwasababu aliyeiokota kadi kaanza kuitumia

Kumbuka ili kufanya transactions online hahitaji passwords ni kuingiza tu account no na zile namba tatu au nne zilizo nyuma ya kadi
 
Ukipoteza kadi piga simu kwanza bank yako waizuie haraka kabla hujafabya mambo mengine.

Kabla ya kwenda polisi piga simu bure kabisa wanazuia hiyo kadi hadi upewe mpya.

Kilichopo alieiokota ameitumia kufanya manunuzi online.

Umechewa sana usiku wote huu utakuja jamaa amekomba kila kitu.
 
Yaan toka October unasubiri mambo ya online na akati ungeyafanya hayo mguu kwa mguu sku iyo iyo wangeblock kila kitu na kadi mpya ungeshaipata ndani ya wiki 2
Sikuhizi unapiga simu tu wablock
 
Chukua ushauri wa chief hapo wahi asubuhi branch ili wazuie online transactions kwasababu aliyeiokota kadi kaanza kuitumia

Kumbuka ili kufanya transactions online hahitaji passwords ni kuingiza tu account no na zile namba tatu au nne zilizo nyuma ya kadi
My Godness!!Kwa nini wameruhusu urahisi namna hii?! Yaani hakuna hata kutumia password!Maana yake mtu akipoteza kadi yake ameisha!
 
Wewe mleta mada nadhani una shida flani kichwani. Yaani toka mwezi wa 10 hujaiblock hiyo card? Halafu unauliza kama zuzu eti hujafanya transaction yeyote kwa nini ukatwe hela? Seriously unauliza swali kama hili?
Halafu mnategemea nchi hii itakuja kuendelea. CCM watatawala miaka 1,000.

Kitatizo kidogo namna hii, kashindwa kutatua, kadi kapoteza tangu mwaka jana mwezi wa 10 hajafuatilia wakati bank yenyewe utopolo ipo kila kona.

Haya pesa ilikatwa kwanza 2,000 lileta mada lipo lipo tu kama bolizozo, wamekata tena 81,000

Badala ya kwenda Bank tena limekuja JF kulialia.

Malezi mengine hasara tu.

Subiri ikikatwa 10M kama imo tena urudi hapa.

Nchi hii kama huna roho wa Mungu kufa masikini ni UFALA.

No wonder kina Magufuli wanafanikiwa
 
Halafu mnategemea nchi hii itakuja kuendelea. CCM watatawala miaka 1,000.

Kitatizo kidogo namna hii, kashindwa kutatua, kadi kapoteza tangu mwaka jana mwezi wa 10 hajafuatilia wakati bank yenyewe utopolo ipo kila kona.

Haya pesa ilikatwa kwanza 2,000 lileta mada lipo lipo tu kama bolizozo, wamekata tena 81,000

Badala ya kwenda Bank tena limekuja JF kulialia.

Malezi mengine hasara tu.

Subiri ikikatwa 10M kama imo tena urudi hapa.

Nchi hii kama huna roho wa Mungu kufa masikini ni UFALA.

No wonder kina Magufuli wanafanikiwa
Mzembe sana huyo...
 
Back
Top Bottom