Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,351
- 40,224
Mnavyojua tena, maisha ya harakati huwa hayana mwisho. Wiki tatu zilizopita nilikuwa nachat na mrembo mmoja matata, niliyekutana naye katika mtandao mmoja wa kuonyesha sura.
Nilitokea kumpenda sana huyo binti, na tukafahamiana vizuri tu. Yeye yuko kwenye mambo ya mitindo. Tatizo yeye anaishi mkoa tofauti na niliopo mimi; nikawa nimemjulisha wikiendi ijayo tuweze kuonana, na tukawa tumeafikiana. Sasa leo asubuhi, akawa amenijulisha anataka aje kuniona; mi nikaona sawa tu hakuna shida.
Akaomba nauli, nami nikamtumia mara mbili yake. Kilichonishtua zaidi, kuwa nauli imeliwa, alianza kuniambia nitume na hela ya mafuta fulani kwa ajili ya massage, yanagharimu 50,000; nikatafakari, nikamwambia tutayanunua huku huku ukishafika.
Baada ya hapo, nikipiga simu haipokelewi, meseji hazijibiwi, w/app hajibu. Imebidi ni hitimishe tu; nauli yangu imeliwa. Ingawa angekuja ningetumia zaidi pamoja na posho ya kwake, lakini kilichoniuma zaidi ni kutokuwa muaminifu.
Wakuu, nimfanyeje huyu mkulungwa?
Nilitokea kumpenda sana huyo binti, na tukafahamiana vizuri tu. Yeye yuko kwenye mambo ya mitindo. Tatizo yeye anaishi mkoa tofauti na niliopo mimi; nikawa nimemjulisha wikiendi ijayo tuweze kuonana, na tukawa tumeafikiana. Sasa leo asubuhi, akawa amenijulisha anataka aje kuniona; mi nikaona sawa tu hakuna shida.
Akaomba nauli, nami nikamtumia mara mbili yake. Kilichonishtua zaidi, kuwa nauli imeliwa, alianza kuniambia nitume na hela ya mafuta fulani kwa ajili ya massage, yanagharimu 50,000; nikatafakari, nikamwambia tutayanunua huku huku ukishafika.
Baada ya hapo, nikipiga simu haipokelewi, meseji hazijibiwi, w/app hajibu. Imebidi ni hitimishe tu; nauli yangu imeliwa. Ingawa angekuja ningetumia zaidi pamoja na posho ya kwake, lakini kilichoniuma zaidi ni kutokuwa muaminifu.
Wakuu, nimfanyeje huyu mkulungwa?