Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hiyo laki 3 ni kitu kidogo sana kwenye ishu ya mapenzi,hata polisi hiyo kesi wataipuuzia maana walipeana kwa mapenzi yao.Pole Kwa kuachwa kwenye mataa ni kawaida sana kwenye mapenzi
Nalog off
Kama aliishi naye kuanzia miezi 6 atasikilizwaDawati la jinsia nadhani lina dili na wana ndoa sio wapenzi
na huenda aliangukia kwenye nyasi siyo kwenye mawe na kokoto zinazochomaHapa ulijiangusha mkuu subir uanguke automatic ndoutaelewa
Niko poa Dear...Hofu kwako..Am back Darling
Uko pouwaa
Niko poa kabisa my...Niko poa Dear...Hofu kwako..
Post zangu almost zote nimepost on behalf.Vijana wengi baada ya kufanya kazi zangu huhitaji kuendelea kufanya kazi,nami nina limit ya vijana/staff that's why nakuja kuwatangazia huku JF na kwingineko.
Hii ni chai tu Wala sio kweli ,mtaji wa ulembo na sendo mjenge nymba Tena mwaka mmoja tu hii haipo .Pia huwez kununua kiwanja na muanze ujenzi bila kiwa na barua ya mauziano .kuwa mkweli kama una shida omba msaada usaidiweHabari ya saizi waungwana?? Naamini mu wazima wa afya kabisa. Bila kupoteza muda niingie kwenye maada.
Kwanza kabisa. Mimi ni binti wa miaka 28, sijaolewa bado na mahusiano yangu yamevunjika wiki tatu zimepita na ndicho chanzo cha mkasa wangu.
Hapo nyuma wakati nipo home mama alinipa sh lak tatu nifanye biashara maana aliamini nina mkono wa biashara na kiukweli nilipoaanza kuuza sendo za kimasai zile niliuza kwa mafanikio makubwa. Tuachane na hilo.
Wakati nafanya biashara nilikutana na boyfriend ambaye tulijikuta tunapendana kweli kweli. Huyu bwana alikuwa muuza urembo. Tumedumu nae kwa muda wa miaka mitatu. Alikuwa na wivu mno hadi alivunja laini zangu na kunisajiria mbili kwa majina yake yeye.
Mwaka jana aliniambia tununue uwanja tujenge nikaona wazo zuri, akaniambia bei ya uwanja akapendekeza tuchangiane, kweli nilichangia kiasi fulani hivi tukapata uwanja. Mwaka huo huo akasema tujenge msingi, tukajenga. Na mwaka huu tulikuwa tunamalizia kuijenga.
Mimi kulingana na mtaji wangu na hela niliyotumia kujengea nyumba nikaishiwa kabisa na yeye akaniahidi kunipa mtaji mwingine tena maana alitaka tuchukue mkopo benki kwa dhamana ya nyumba mimi nikagoma kabisa.
Basi majukumu yangu yote akayavaa yeye kuanza kunilisha, kodi ya nyumba na vingine vingi maana mimi niliishiwa hela. Shida imekuja baada ya kodi kuniishia mimi nikamwomba awekee milango nyumba yetu ili mimi nihamie akasema kwa sasa hana hela, nikamwomba basi anilipie kodi sh elfu 75 tena akaanza kalenda.
Nilivyombana sanaa akawa mkali ndipo akafunguka sasa. Kumbe ile nyumba na uwanja si vyetu tena, alikuwa anamsaidia rafiki yake mwanajeshi, kwa hiyo yeye alikuwa msimamizi tu. Hela nilizokuwa natoa mimi sijui alichozifanyia na alivyoona nimekuwa mkali akakimbia na kwenda huko kusikojulikana.
Kwa hiyo nimetapeliwa na huyu bwana kwa namna hiyo. Sasa saizi mwenye nyumba kanibana ananipa vitisho vya kunitimua nami hapa sijabaki na hela. Nimesharipoti polisi kuhusu kutapeliwa na bado anatafutwa kubaini aliko.
Mwisho, naombeni msaada wa hali na mali jamani niweze kulipa kodi ya chumba sh 75,000. Na pili naomba ushauri wenu nifanyaje zaidi ili niweze kurudishiwa hela nilizotaperiwa na je siwezi kusimamisha ile nyumba kuguswa na mtu hadi kibari cha mahakama kitoke kwa maridhiano?
Naomba kuwasilisha.
Soma maelezo yake vizuri hii n stor katunga tu .lengo ANAHITAJI msaada Ivo kailjificha kwenye kivuli Cha utapeliPole sana, unaonaje ukirudi nyumbani kwa mama hadi biashara yako ikisimama tena.
Maana utasaidiwa kodi ya mwezi mmoja, na miezi inayofata itakuaje
Mpenzi anakushawishi kabisaa tujenge aisee uko serious na pesa wewe