Tanzania ni nchi kati ya nchi za Africa ambayo inauwezo wa kwenda mbali sana kiuongozi kwenye kila eneo. Tuna rasilimali karibu zote na kwasasa tunaanza kuona jidihata za uwekezaji na uzuiaji wa rushwa.
Kitu kimoja ambacho kinaturudisha nyuma na tumerudi nyuma sana ni demokrasia. Nchi yetu inajichanganya sana. Serikali imekuwa na double personality haijui kama inataka demokrasia au demokrasia ni kikwazo. Serikali wamekuwa wanajali vitu vidogo vidogo , vijimaneno na hii hali imeanza kutuletea shida sana. Lakini kibaya zaidi viongozi wengi wa serikali wamekuwa wanajali siasa zaidi ya kujali nchi kama njia ya kujionyesha.
Inawezekana kabisa hii wiki tukaikumbuka kitendo cha Mbowe na utaratibu wake na uvumilivu wake kususia uchaguzi sio kitendo kidogo kama wengine wanavyopiga madongo hapa. Hakuna mtu mtu anajua upinzani unawatu wangapi lakini Lowassa alipata karibu 40% ya wapiga kura na kuna wengine wengi hawana vyama lakini wanapenda demokrasia na haki. Tujiulize swala dogo tu Je Watanzania 35% tu wakisusia shughuli za kimaendeleo, wakagoma, wasitoe ushirikiano na viongozi, wakawaona kama maadui itasaidia vipi nchi.
Kitu kibaya zaidi ni kwamba nchi yetu itakuwa kama inapata shida na kutokuelewana kusiko na sababu. CCM tayari ina super majority kwenye bunge, Raisi anateua karibu kila kiongozi sasa kuna sababu gani ya kuingiza nchi kwenye hali hii wakati hatujui tunanufaika kwa lipi. Lissu akifa, Mbowe asigombee au Lema je itasaidia vipi nchi.
Kwa wale washabiki na mnaofikiri mambo hayatabadilika mnajidanganya maana hii siyo nzuri kwa nchi bila kuweka siasa. Na ndiyo maana nasema nchi hizi tungekuwa na mfumo ambao hakuna chama chochote cha siasa watu wanachaguliwa kama raia na kufuata katiba nchi ingekuwa mbali zaidi.
Kitu kimoja ambacho kinaturudisha nyuma na tumerudi nyuma sana ni demokrasia. Nchi yetu inajichanganya sana. Serikali imekuwa na double personality haijui kama inataka demokrasia au demokrasia ni kikwazo. Serikali wamekuwa wanajali vitu vidogo vidogo , vijimaneno na hii hali imeanza kutuletea shida sana. Lakini kibaya zaidi viongozi wengi wa serikali wamekuwa wanajali siasa zaidi ya kujali nchi kama njia ya kujionyesha.
Inawezekana kabisa hii wiki tukaikumbuka kitendo cha Mbowe na utaratibu wake na uvumilivu wake kususia uchaguzi sio kitendo kidogo kama wengine wanavyopiga madongo hapa. Hakuna mtu mtu anajua upinzani unawatu wangapi lakini Lowassa alipata karibu 40% ya wapiga kura na kuna wengine wengi hawana vyama lakini wanapenda demokrasia na haki. Tujiulize swala dogo tu Je Watanzania 35% tu wakisusia shughuli za kimaendeleo, wakagoma, wasitoe ushirikiano na viongozi, wakawaona kama maadui itasaidia vipi nchi.
Kitu kibaya zaidi ni kwamba nchi yetu itakuwa kama inapata shida na kutokuelewana kusiko na sababu. CCM tayari ina super majority kwenye bunge, Raisi anateua karibu kila kiongozi sasa kuna sababu gani ya kuingiza nchi kwenye hali hii wakati hatujui tunanufaika kwa lipi. Lissu akifa, Mbowe asigombee au Lema je itasaidia vipi nchi.
Kwa wale washabiki na mnaofikiri mambo hayatabadilika mnajidanganya maana hii siyo nzuri kwa nchi bila kuweka siasa. Na ndiyo maana nasema nchi hizi tungekuwa na mfumo ambao hakuna chama chochote cha siasa watu wanachaguliwa kama raia na kufuata katiba nchi ingekuwa mbali zaidi.