Wingu
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 4,318
- 401
Unaandika kwa kufikiria au ili mradi na wewe umepost.
Hivi Jamani hata hivyo, kuna tatizo gani mtu kutoa kauli ya kujitenga. Nahisi Kama Mbowe ndio alikurupuka kumuambia Nasari ametoa kauli ya kitoto.
Kama wazinzibar wanazungumzia kujitenga, kwa nini sehemu nyingine za Tanzania zisizungumzie kujitenga? Huyu Kijana anahoja ya msingi na watanzania tunapaswa kuitafakari inaweza ikawa ni the best option for us, especially kama Matakwa ya Wananchi kwenye mchakato wa Katiba na Uchaguzi wa 2015 hayataheshimiwa.
Utawala wa nchi hii chini ya Uongozi wa CCM umeshindwa kuwaletea watanzania tija katika umoja wao, Hata wazanzibar wanapopiga kelele za kutaka kujitenga ni kwa sababu wanaona kwamba Muundo wa Serikali ya Muungani hauwaletei tija,
Hivyo kama sehemu yoyote ile ya Tanzania inaona inaweza ikasimama yenyewe nje ya Ushenzi unaofanyika ndani ya Jamuhuri nawashauri waendelee kufikiria kujitenga.