Nimeshuhudia wizi wa ajabu huku kwetu

Hao wametumwa kumkomoa huyo mwenye nyumba au walikua na personal issues na mlinzi
 
Kisa cha jana

Huku mtaani kwetu bwana kuna nyumba fulani inafanyiwa finishing. Hakuna aliyehamia bado.

So wamemaliza plasta so wanataka anza skimming na rangi. Wameleta ndoo kibao za rangi kwa ajili ya kuanza kazi. Nyumba ina geti so vifaa vinakaa ndani na fundi pia mmoja hulala humo.

So anaelala alitoka so wazee wa kazi wakaja kumuotea nadhan walimsomea raman ni mzee wa gambe.

Kinachonishangaza ni kitu walichoiba.

Eti wamekuta zile ndoo zina rangi, wao wana shida na ndoo.. so wamemwaga rangi kadhaa wakasepa na ndoo.

Rangi zile nyingine zina kost 130k za nje na zingine ni 32k zile za rangi. Lkn wameiba ndoo ya 2k.
Aina hii ya wezi huwa wanaitwa "amateur thieves". Hawa wanaweza kuingia ndani nyumbani kwako halafu wakaiba kiatu kimoja cha mguu wa kushoto, wakakuachia kingine kile cha mguu wa kulia. Wao kuiba ni aina ya mchezo fulani wa burudani kama vile mtu kucheza mpira au draft
 
Aina hii ya wezi huwa wanaitwa "amateur thieves". Hawa wanaweza kuingia ndani nyumbani kwako halafu wakaiba kiatu kimoja cha mguu wa kushoto, wakakuachia kingine kile cha mguu wa kulia. Wao kuiba ni aina ya mchezo fulani wa burudani kama vile mtu kucheza mpira au draft

Haah haah,hao watakuwa field wanaipambania coursework mkuu
 
Vibaka wa uswazi ni wapumbavu sana nakumbuka kuna likizo moja tuliondoka mkoani na familia bila ya kumwacha mtu home basi bana vibaka walivunja ila cha ajabu hawakuiba mifuko ya saruji, pikipiki, tv, wala kitu kikubwa cha thamani.

Ila walichofanya ni kupika msosi wakala na kunywa bia zote zilizopo kwenye friji, waliiba vyombo vya jikoni karibia vyote, mapazia na vyakula vyote vilivyo hifadhiwa kwenye friji na vilivyopo stoo.

Yaani hadi leo hii sifahamu akili zao zilikua zina waza nini hasa.
 
Back
Top Bottom