Jamani, hivi hawa mashabiki wa vyama (vyote tawala na upinzani) wanaoshinda kwenye ofisi za halmashauri au viwanja vya mpira ati kusingizia kulinda kura au kusubiria matokeo... Hivi hawa hawana kazi za kufanya? Si vyama vina wawakilishi na viongozi wao si ndio wafanye hiyo kazi.
Nafikiri wewe u mgeni Tanzania hii. Wenzio wanasikitika wanafanya kazi lakini kipato hawakioni. Wamechoshwa na kupeleka watu Bungeni wanaenda kusinzia. Wanasikitika kuwa na Rais anayewaambia hajui kwanini watanzania ni maskini wakati rasilimali chama chake kimegawa kwa wageni.
Hawaoni maana ya kuwa na viongozi wanaokumbatia ufisadi. Hawataki kuwaona viongozi wanaolea uzembe makazini na wanaojipenda wenyewe. Nahisi nawe ni mmoja wa viongozi hao au mtoto wao ndo maana hujui kama tanzania kuna shida.
Tuna shida ya mfumuko wa bei, madawa feki mahospitalini, shida ya umeme, maji, usafiri, walimu nk.
Sitakutofautisha na yule Malkia wa Ufaransa.
Ni vyema kulinda kura yako leo siku moja na ukaishi kwa uhakika miaka mitano kuliko kujifanya unajua kazi ukaendelea na usanii.