'Nimeshikwa, nashindwa kujinasua, hebu nisaidieni'

as long dini yako inaruhusu wake zaidi ya mmoja-unaweza kumchukua huyo binti jumla
 
Swala la kuoa mke wa pili unajidanganya, unatakiwa uwe muadilifu kweli kweli vinginevyo mzee umekwisha. Muda si mrefu utatembelea ndala, kuna wenzako walijidanganya kwenye nafsi zao huku wakisingizia dini lakini chamoto wamekiona. Someni dini vizuri mtaelewa maana ya mke zaidi ya mmoja.
 
Unaweza usiniamini haya niyaelezayo hapa, lakini ni ukweli mtupu na sasa sijui namna ambavyo ninaweza kutoka katika uhusiano huu maana sitaki kumkosesha raha mke wangu, ni kwamba mwaka 2007 niliingia kwenye mahusiano na binti mmoja aliyekuwa katika chuo kimoja mjini Morogoro wakati huo akiwa field Moshi kwenye moja ya taasisi ya serikali, basi nikatupa ndoano tukawa pamoja na hata aliporudi chuo kumaliza kozi yake.

mwaka mmoja baadaye alimaliza akarudi moshi akaanafanya kazi kwenye taasisi moja binafsi tutaka pamoja tena nilimtafutia chumba nikamweka huko nikawa mimi kama baba mwenye nyumba, siku moja tukiwa kwake tulikorofishana nikaondoka kwake nyumbani bila kuaga wakati naondoka njiani alinipigia simu sikupokea kama mara tano, nikazima simu. Nilipofika nyumbani akapiga simu ya mke wangu masikini alipokea tu, yule binti akasema 'Mwambie mume wako kesho anipe sh. 40,000 nikatoe mimba yake, nampigia simu yake ajidai kazima'.

Mungu wangu basi mke wangu kwa hekima akaniuliza "mumwe wangu haya aliyosema huyu dada ni kweli au naota? nikamuuliza amesema nini na ni nani? akasema kuna dada namba yake hii inafanana na yangu na yako (maana nilichonga namba zinazofafa zote zinatofautiana namba ya kwanza tu) anasema umpe hela kesho akatoe mimba yako.

Nikamwambie hebu tulale tuzungumze kesho mke wangu usiku huu ni mwingi tutagombana bure kwa ajili ya simu si unajua mitandao? nikajitetea na hoja yangu ikakubalika. Asubuhi ilipofika tukaanza mjadala lakini nilipojitetea alikubali lakini kadiri tulivyokwenda alizidi kubadilika mke wangu kutokana na fikra mpya zinavyomjia kutokana na maneno yale ya binti yule hata hivyo tuliendeleea hivyo hadi alipokutana naye yule binti baada ya kumfuata kazini kwake na kupigana naye.

Baada ya ugomvi huo mimi nikamwambia yule mwanamke nimemuacha karibu mara tatu na kweli nilimuacha kama miezi mitatu lakini baadaye nilirudi tena nikamuacha nikarudi tena nikamuacha nikarudi tena hadi leo hii tumehama sehemu ambayo mke wangu alipajua alipokuwa anaishi na sasa nimempangia chumba sehemu nyingine lakini mke wangu tangu alipogundua nipo na binti huyo haniamini tena kwani tangu nimemuoa mwaka 1997 hadi leo hakuwahi kuhisi nimetoka nje ya ndoa hadi tatizo hilo la binti huyo wa kimasai, sielewi nitatokaje na nimemwahidi kwamba nitamuo mke wa pili kwa vile mimi ni mwislamu lakini mke wangu hataki anasema nikimuoa huyo yeye anarudi kwao Tabora sasa nifanyeje?

Naomba mnishauri wote nawapenda mke wangu ambaye tuna watoto watatu mmoja ana umri wa miaka 14, wa pili 12 na wa tatu miaka minne na nusu. je nifanyeje?

I feel very bad for what you have done to your wife!
Nenda ukamuombe msamaha haraka sana kakangu, Kilio anacholia mkeo na sala anayoiomba sijui kama utakuja kufanikiwa maishani mwako. Wengi wenu huwa mnatumia kigezo cha dini kufanya uzinzi wenu lakini si halali kamwe. Imagine kama mkeo angekufanyia hivyo ungejisikiaje?. Sio vizuri mkuu!
Wakumbuke pia watoto wako ukimchukua huyo hawara hawezi kuwahudumia vizuri kama mama yao angewahudumia, maisha yenyewe haya magumu ndo unataka kuwapanga hao wake utaweza?
 
as long dini yako inaruhusu wake zaidi ya mmoja-unaweza kumchukua huyo binti jumla

Dini sio kigezo cha kufanyia uzinzi na kumletea dharau mkeo wa ndoa, Naomba mkasome sheria "zenu" vizuri kama zinaruhusu hadi mke wa ndoa kupigwa na hawara na kuletewa dharau za kijingajinga. Kama zinaruhusu hayo sidhani kama inatenda haki itakuwa ni unyanyasaji tu!
 
Tabia haina dawa,huyo kaka ni mzinzi by nature! Binafsi fikiria kama mkeo nae angekufanyia unayomtendea! Dont' be selfish elewa kuwa unamuumiza mkeo wa maisha.
 
Sikiza wewe baba alichofanya huyo binti cha kumpigia mkeo is very nice

cz asingejua mambo yako unayoyafanya, naisitoshe unavomwambia unataka kuoa mke wa pili kisa dini inaruhusu

mbona hukumwabia mke wangu sasa hv natoka nje, kuoa mke wa pili kwa kisingizio cha dini ni kujikosha kwa mkeo kuonekana ww ni muwazi kumbe......lol?

kumbuka MSHAHARA WA DHAMBI MAUTI
 
Pole. Huna jinsi. Ongea vizuri na mke mkubwa ukimuomba radhi na kumweleza hali halisi ilivyo ukimuomba radhi akusamehe kwa dhambi ya uzinzi. Muombe akubali uoe mke wa pili kwa kuwa dini yako inaruhusu ila hukuwa mwaminifu tangu mwanzo. Akikataa kata kata, itabidi uachane na huyo binti.
 
Mzee mwenzangu mi naona hawa watoto huku wanakuzingua tu, ngoja nikupe mbinu...

Muache tena kwa mda huyo mdada, alafu wakati ukiwa hauko nae, akili itafikiria cha kufanya, japo kwa uzoefu wangu hutaweza kumuacha jumla.

Namna ya kumuacha; Wanawake (nyumba ndogo), wapo tu kwa ajili ya hela zako. Sasa wewe mdanganye kuwa kuna tatizo kubwa limetokea (mfano umeingiza hasara kazini), na hivyo karibia mshahara wako wote unakatwa. Kuanzia hapo punguza kutoa matumizi kwa asilimia 95, lakini ukijifanya bado unampenda sana. Kwa kweli siku si nyingi huyo mwanamke atatafuta kisingizio cha kukupiga chini, na wewe utapata mahala pa kuchomokea, maana atakuwa amekuuzi...
 
Sikiza wewe baba alichofanya huyo binti cha kumpigia mkeo is very nice

cz asingejua mambo yako unayoyafanya, naisitoshe unavomwambia unataka kuoa mke wa pili kisa dini inaruhusu

mbona hukumwabia mke wangu sasa hv natoka nje, kuoa mke wa pili kwa kisingizio cha dini ni kujikosha kwa mkeo kuonekana ww ni muwazi kumbe......lol?

kumbuka MSHAHARA WA DHAMBI MAUTI

Punguza mikwara...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom