Nimeshangazwa na Matokeo ya Kidato cha Nne 2021

Ila tuache utani jamani
Shule za Serikali wanafunzi wanajitafutia maarifa mtaani
Si ajabu kukuta mtu kapata B Geo ila akikwambia alivyohaso utamuonea huruma.
 
Sababu kubwa ya wingi wa hizi division 1 ni kutokuwa na zile penalt za hesabu!

Ufaulu wa hesabu kwa mwaka huu ni wa kiwango cha chini sana kuliko miaka yote na kama penalt zingekuwepo basi division 1 huenda mwaka huu zingekuwa chache kupita miaka mingine!

Wapo wanafunzi wengi sana wana division 1 lakini wana F za hesabu.
He! Hakuna penalt ya hesabu?
 
Mkuu umeongea jambo zuri sana. Tatizo ni mitihani ya kubet inayowapeleka wanafunzi shule za sekondari wakiwa hawajui kusoma wala kuandika. Tazama video ifuatayo kwa ushahidi zaidi; sipendi kuongea maneno matupu. Tazama video
View attachment 2084395


Na huko sekondari mitihani ya NECTA imerahishishwa kwa makusudi ili kuwafaulisha wanafunzi kisiasa. Tazama mtihani wa Biology wa NECTA 1999 ulinganishe na mtihani wa NECTA 2017 utapata jibu mwenyewe. Zamani kupata divisheni wani halikuwa jambo la mchezo. Maswali rahisi kama haya (2017) hata mkulima ambaye hakwenda shule atapata divisheni wani misa ya kwanza tu!

NECTA 1997
View attachment 2084398
NECTA 2017
View attachment 2084401



Hii ni Kali Aiseee.
 
He! Hakuna penalt ya hesabu?

Duh, hiki kitu kumbe wengi hawajui ee…?
Penalt zilishakufa miaka mingi sana iliyopita…
Hawa nilioonyesha miaka ya nyuma wangekuwa na three..lakini wana F za hesabu na wana division 1 na 2.
IMG_1495.jpg
 
Hivi hamuelewi kuwa kwa sasa kidato cha nne ndiyo shule ya msingi?nina uhakika mtoto akifika kidato cha nne atakuwa anajua mambo ya msingi....siasa ipo
Unaongelea mtaala gani mkuu? Mi nimeshika kitabu Cha mtoto wangu wa Darasa la tano naona wanasoma vitu ambavyo Enzi zetu tulisoma O level. Nimeona wanasoma Hadi Reproduction
 
Duh, hiki kitu kumbe wengi hawajui ee…?
Penalt zilishakufa miaka mingi sana iliyopita…
Hawa nilioonyesha miaka ya nyuma wangekuwa na three..lakini wana F za hesabu na wana division 1 na 2.
View attachment 2084581

Hapa ndio Maana tuna Mashaka na Division 1 unakuwaje una Division 1 na Basic Mathematics una ‘F’ huyu akienda Kusoma PCB au CBG akakutana na Na Mathematics Hawezi kutoboa au ile ya Advance wameifanyaje? Kwenye baadhi ya Combinations?
 
Mkuu umeongea jambo zuri sana. Tatizo ni mitihani ya kubet inayowapeleka wanafunzi shule za sekondari wakiwa hawajui kusoma wala kuandika. Tazama video ifuatayo kwa ushahidi zaidi; sipendi kuongea maneno matupu. Tazama video 👇
View attachment 2084395


Na huko sekondari mitihani ya NECTA imerahishishwa kwa makusudi ili kuwafaulisha wanafunzi kisiasa. Tazama mtihani wa Biology wa NECTA 1999 ulinganishe na mtihani wa NECTA 2017 utapata jibu mwenyewe. Zamani kupata divisheni wani halikuwa jambo la mchezo. Maswali rahisi kama haya (2017) hata mkulima ambaye hakwenda shule atapata divisheni wani misa ya kwanza tu!

NECTA 1997
View attachment 2084398
NECTA 2017
View attachment 2084401
Real eyes realize real lies..

We have been conned big time
 
Duh, hiki kitu kumbe wengi hawajui ee…?
Penalt zilishakufa miaka mingi sana iliyopita…
Hawa nilioonyesha miaka ya nyuma wangekuwa na three..lakini wana F za hesabu na wana division 1 na 2.
View attachment 2084581
Kumbe serikali imeondoa penalty kwa makusudi ili kuongeza idadi ya divisheni ones kisiasa :oops: Mungu anawaona kwa kweli; ndio maana nchi hii imelaaniwa!!!! :oops: :oops: :oops:
 
Nani ana kumbukumbu ya matokeo ya mwaka 2012....ilikuwa ni kizazaa...wanafunzi walifeli kupita kiasi...nchi nzima...cha kushangaza yaliporudiwa aliyekuwa na div2 anajikuta ana div.4,,,, na mweny div4...anajikuta ana Div.2 au 3,,, sasa sielewi ni mchezo gani ulifanyika hapo katikati....Mi pia ni muhanga wa miaka hiyo 2012
Duuh unajua hii kitu huwa natafakari sana jibu nakosa .
Kuna watu walikuwa na points 26. Kuna watu walikuwa na points 33-35.
Cha kushangaza matokeo yaliporudiwa
Wale wenye 33,34,35 wakaenda mpaka points 21 nk. Huku wengine wenye 26 wakabakia vilevile
 
Kama wamekosida CA kweli hawako serious...yani CA ambazo walimu wamejaza bila hata kuwa na hizo test amabazo zilitakiwa kujazwa.

Kwa mfano mwaka huu wameondoa project kwenye CA wakaweka mock.cha ajabu kuna wanafunzi walijaziwa matokeo ya mock wakati hata hawakufanya.mfumo haruhusu uache wazi hata kama mwanafunzi hakufanya mtihani
 
Nani ana kumbukumbu ya matokeo ya mwaka 2012....ilikuwa ni kizazaa...wanafunzi walifeli kupita kiasi...nchi nzima...cha kushangaza yaliporudiwa aliyekuwa na div2 anajikuta ana div.4,,,, na mweny div4...anajikuta ana Div.2 au 3,,, sasa sielewi ni mchezo gani ulifanyika hapo katikati....Mi pia ni muhanga wa miaka hiyo 2012
Mi pia ni muhanga wa 2012, kuna shida saba NECTA.
 
Wasalamu Wakuu

Leo Baraza la Mitihani Tanzania Bara, Limetangaza matokeo ya Kidato cha Nne Na Kuonesha Ufaulu ukiongezela kwa Asilimia Chini ya 2%. Well And Good.

Lakini Baada ya Kufuatilia Matokeo Ya Shule Nyingi Nimeona Division 1 zikiwa Nyingi sana na Division 4 zikipungua Sanaa. Hii ikanipa Maswali na Kujiuliza Kuhusu Ubora wa Mitihani Wanayotungiwa Vijana wetu na Ubora wa Elimu. Nakubaliana na wanaosema kuwa Ubora wa Elimu haupimwi kwa Ufaulu lakini mwaka 2021 nimeona ndio Mwaka ambao Division 1 zimekuwa Nyingi sanaa kuliko miaka Yote na Wasichana Wamefaulu sanaa kuliko Miaka Yote.

Hii imenipa Maswali na Kuhisi Kuwa Huenda Siasa Imeingia Kwenye Elimu yetu, Yaani Katika Kuunga Juhudi za Rais Mwanamke na Ufaulu umeenda Sana kwa Wanawake kuonesha Juhudi ambazo Serikalo inafanya kuwainua wanawake. Hii nimewaza kwa sauti.

Naweza kuwa sina Points nzuri za Ku Address hili lakini Kiukweli kuja Harufu ambayo sio Nzuri kwenye Elimu yetu.

Najiuliza hizi Division 1 je ni sawa na zile za miaka ya 2012 kuja Chini? Zile za miaka ya 2000-2011? Ni sawa na hizi? Je, waalimu mtusaidie Mitihani ni sawa? Au mitaala kwa Ujumla Imebadilika?

Hii inanifanya kuwaza Mbali, Huenda hawa Vijana Wetu wakaja kukumbana na Kitu Kizito katika Matokeo yao ya kidato cha sita ambacho wengi Wanatarajia Kufaulu vizuri kwenda Chuo na Kupata Mkopo wa Serikali, kwasababu Hapo serikali Itahitajika kutenga Budget Kubwa Huenda Hawa Vijana wetu walio Pitishwa Kiholela Wakashindwa Kwa Wingi kwenda Chuo kwa Kigezo cha Serikali kuogopa Kutoa Mikopo ya Elimu Ya Elimu Ya Juu kwa Wanafunzi Hawa, na Kuongeza Late ya Unemployment mtaani na Kitakacho tokea ni Hawa Kuamua Kwenda Diploma kuendelea kupoteza muda wa Kuajiriwa na Kuongeza ugumu wa Maisha.

Tuwajibu kama wadau wa Elimu Nchini Kuangalia Hili kwa Undani sanaaa? Nakumbuka Kipindi Chetu Mama Ndalichako Alifahamika na Wanafunzi wote kwasababu Ya Mitihani Yake, Lakini Mrithi wake wa sahizi sijui hata kama anafahamika kama Mama Ndalichako, katika Kusimamia Ubora Wa Mitihani.

Mfano Mkubwa Ni Mdogo wangu Ambaye Amefaulu kwa Division 1 ya 7 huku nikijua Fika Kichwa chake ni Kigumu, na Hajawahi Kuwa Kwenye 20 bora Darasani Kwao. Inanipa Wasiwasi Kwa Form 6

Wadau Tuangalie sana hili
Kuna siasa nyingi sana mkuu.

Wakati mwingine wanafanya standardization kuaminisha umma elimu iko juu,sababu mwananchi wa kawaida anachojua kupata hizo one na two nyingi badi elimu ni bora. Siasa ni nyingi Sana kwenye matokeo ili kupunguza au kuondoa kelele.

Kidato cha pili ndiyo usiseme. Naongea haya kwa uzoefu wangu.
 
Back
Top Bottom