Nimeshakata tamaa ya maisha nimepanga kujiua ( mawazo yangu ni kujiua 100%)

sojer

Member
Sep 4, 2018
71
47
POLENI NA MAJUKUMU ( ee, MUNGU nisaidie)

Mimi ni kijana ambaye utoto wangu nimeishi maisha ya uyatima nasema hivi kwa kuwa tangu nizaliwe sijawahi kumwona mama wala sijui baba yangu anafananaje maana naambiwa mama alifariki nikiwa na umri wa miezi mitatu na baba hapo hapo akaniacha nikiwa na umri huo hivyo nimelelewa na bibi mzaa mama hadi kufikia umri wa kwenda shule ambapo hapo nimelelewa na baba mdogo kutoka darasa la kwanza

Baba mzazi sijawahi kumuona ila niliona maiti yake nikiwa darasa la tatu ambayo yalisafirishwa kutoka huko alikokuwa akiishi
Maisha yangu yamekuwa ya mateso muda WOTE hakuna siku nimewahi kupata raha au faraja katika maisha yangu nimeteseka sana ,nimefanya kazi kama mtumwa ,nimelala sana na njaa ( kulala siku mbili,au tatu bila kula sio jambo la kushangaza imekuwa kawaida yangu

Niseme wazi licha ya baba mdogo kuwa na hali ngumu ya maisha lakini kanisaidia kusoma hadi chuo cha UALIMU ngazi ya cheti (UALIMU shule za msingi) sina budi kumshukuru japo michango mingi na ada za shule nimelipiwa na tasisi mbalimbali hivyo yeye alikuwa mlezi wangu japo alikuwa akinipa na hela ndogo ndogo za matumizi licha ya kuwa anawatoto wake na hali ngumu ya maisha

Baada ya kumaliza chuo cha UALIMU mwaka 2015 nikaona kama ndo ukombozi wangu maana miezi na siku yoyote nitaajiriwa lakini mpaka Leo sijapata ajira ,nimefanya vibarua na kago mtaani làkini kila ninachokipata hakijawahi fanikisha malengo yangu kabisa kabisa nimeishia kukopwa na jamaa,marafiki na ndugu lakini ubaya wake hawajawai nirejeshea pesa zangu nimekuwa ni mtu wa kufanya bidii na kuhangaika huku na huku hakuna siku nimepata faraja katika maisha yangu

Kumbuka hapa nilipo siwezi kurudi kwa baba mlezi kwa maana umri wake umeenda na hajiwezi tena na Mimi nimekuwa nikijitahidi kumkumbuka kwa kadri ya kidogo nachopata lakini kadri siku zinavyoenda ndo hali yangu inazidi kuwa mbaya zaidi,

Nipo kwenye matatizo na majaribu mazito hapa nilipo sijala chochote toka juzi na macho yamevimba kutokana na kulia muda wote usingizi hamna kabisakabisa na nimeishiwa chakari kabisa hapa nimebakiwa na mia sita kwa ajiri ya kununulia sumu tu

Hali yangu ya maisha imekuwa ngumu mno na nilijaribu kuomba ushauri kwa baadhi ya watu wakaniambia nyota yako imechafuka hivyo unapaswa uende kwa wataalamu wasafishe nyota Leo Nina miezi kadhaa tangu niende huko sijapata hata tone la fanikio nimeishia kutoa pesa zangu nilizotafuta kwa jasho jingi


Nimehangaika sana nimehangaika mno sina namna ya kujikwamua sioni upenyo wowote yaani mbele sioni kabisakabisa ninaowadai wamenifungia simu zao na kuniblock mungu wape maisha mema unajua kujitoa kwangu kulikuwaje mpaka Leo nawaza hivi najua ni mapenzi yako ee mungu

Hii hali ilivyozidi kuwa mbaya siku hadi siku kule kijijini kulikuwa na mashamba ambayo walikuwa wakilima na kuyatumia wazazi wangu hivyo baada ya wao kutangulia mbele za haki baba mlezi kanipatia hayo mashamba NA kaniambia wazi kuwa niyauze ili nipate pa kuanzia lakini baada ya kuuza hayo mashamba ndo nimezidi kuumia kwa zaidi ya Mara mia zaidi

Pesa iliyopatikana niliamua kufanya ufugaji wa kuku lakini katika vifaranga 150 nilivyoanza navyo vilikufa na kubaki 11 tu na baadae vimefikia umri wa kutaga vikafa tena vikabaki 5 tu ambavyo niliamua kuuza kwa bei ya hasara

Nimefanya mengi bila mafanikio
Nimejiunga na shirika moja la ujasiriamali la utengenezaji bidhaa za viwandani lakini baadae likafungiwa maana lilikuwa halina usajiri kila nachogusa ndo kinaniumiza zaidi

Pesa niliyokuwa nimetunza sehemu iliyobaki baada ya kuuza mashamba kuna mtu kanishauri kuwekeza katika forex MUNGU WE MUNGU WE EEE MUNGU (MJINGA MM)

Jamani MUNGU nimekosa nini mm mbona kila jambo nalogusa sifanikiwi kibaya zaidi unaniacha nahangaika na kulala na njaa siku zote hizi mbona nikipata huwa nasaidia kila aliyeniomba msaada kwanini mm nipo hivi EE MUNGU NIMEKOSA NINI MM?

jamani nateseka sina cha kutegemea tena hali yangu imezorota sana nimekonda hakuna mfano, uso mzito maana Nina siku mbili ndani nimelala tu nashindia kulia tu sijala Leo naenda siku ya tatu

Jamani nimeingia huko forex nimeliwa kila kitu,TV na sabufa nimeuza kitanda nimeuza,simu nayo nataka niuze kwa ajiri ya nauli navyoenda kunywa sumu maana nimepanga kunywea mbali na meneo haya tena mtoni ili kupoteza ushahidi


Nimeshakata tamaa kabisakabisa naomba naomba kwa mwenye msaada wa mawazo yoyote ya kuninusuru maisha yangu anisaidie ,pia kama kuna mtu yeyote mwenye kuweza kunisaidia kupata ajira huko serikalini nisaidieni maana kama vyeti ninavyo na nimetuma maombi ya ajira Mara kadhaa serikalini bila mafanikio

Nisaidieni jamani nisaidieni jamani

Hapa chini utaona screenshot ya trade nilizounguza katika mfumo wa dola



Naombeni msaada wa hali NA Mali nisaidieni nisipoteze roho yangu kwa njaa ama kujiua

Naombeni msaada wenu nisaidieni mm msaada wenu tafadhali nipatiwe msaada
Wa mawazo
Au nipate ajira serikalini
Msaada hata pesa nitashukuru zaidi


Ahsante



Pia nimeambatanisha barua niliyoandikiwa na kijiji kipindi naenda chuo kama uthibitisho


Nimeandika ukweli mtupu japo tabu na mateso mengi niliyopitia sijaandika ila utayeguswa kwa namna yoyote ile nitashukuru kwa msaada wako
Screenshot_20190813-183517.jpeg
IMG-20190813-WA0003.jpeg
 

Attachments

  • IMG-20190729-WA0014.jpeg
    IMG-20190729-WA0014.jpeg
    50.3 KB · Views: 96
  • Screenshot_20190729-013547.jpeg
    Screenshot_20190729-013547.jpeg
    20.9 KB · Views: 101
  • Screenshot_20190729-013547.jpeg
    Screenshot_20190729-013547.jpeg
    20.9 KB · Views: 74
  • Screenshot_20190813-183611.jpeg
    Screenshot_20190813-183611.jpeg
    43.3 KB · Views: 76
  • Screenshot_20190729-013204.jpeg
    Screenshot_20190729-013204.jpeg
    35.1 KB · Views: 92
  • Screenshot_20190813-183611.jpeg
    Screenshot_20190813-183611.jpeg
    43.3 KB · Views: 87
  • IMG-20190813-WA0002.jpeg
    IMG-20190813-WA0002.jpeg
    13.6 KB · Views: 102
Aisee pole sana mkuu.

Kujiua sio suluhu ya matatizo. Usiwaze sana kwa kile usichonacho,bali mshukuru Mungu/Furahi kwa kile ulichonacho.

Nina amini mambo yatakuwa sawa,usichoke kuomba msaada kwa watu sahihi.

Maisha ni vita, don't yield.
 
Aisee pole sana mkuu.

Kujiua sio suluhu ya matatizo. Usiwaze sana kwa kile usichonacho,bali mshukuru Mungu/Furahi kwa kile ulichonacho.

Nina amini mambo yatakuwa sawa,usichoke kuomba msaada kwa watu sahihi.

Maisha ni vita, don't yield.
Mkuu yaani hivi kila mtu hapokei simu yangu na kuna watu nawaazima hata elfu mbili ya msosi wananiambia hawana na wakati wao huwa nawasaidia ila mungu atalipa
 
FOREX FOREX FOREX INATAKA KUTOA ROHO YA MTU..... ONTARIO utawaambia nini watu jamaa akijiua?


ila nini mkuu... KUJIUA SIO SULUHISHO, KUNA MAISHA MAZURI YANAKUSUBIRI MBELE, UNAPOKATA TAMAA UNAFELI SANA.

NAAMINI WATU WATAKUJA KUKUSAIDIA...MUNGU ANAONA KILIO CHAKO.
 
I once CRIED because I had no SHOES until I met Someone with no FEET..., Chochote kigumu unachopitia kuna watu wanashida maradufu ila wanapambana na hali zao...

Kukosa pesa au ajira unaweza kuona ni shida.., vipi yule ambaye hawezi hata kuamka kutafuta hizo pesa au ajira.., hata akivipata hana nguvu za ku-enjoy matokeo yake ?

Whenever you fall Pick Something Up and Move On.....
 
I once CRIED because I had no SHOES until I met Someone with no FEET..., Chochote kigumu unachopitia kuna watu wanashida maradufu ila wanapambana na hali zao...

Kukosa pesa au ajira unaweza kuona ni shida.., vipi yule ambaye hawezi hata kuamka kutafuta hizo pesa au ajira.., hata akivipata hana nguvu za ku-enjoy matokeo yake ?

Whenever you fall Pick Something Up and Move On.....
Mkuuu natamani nijipige picha unione kwa kweli hali ni mbaya sh mia sita tu NDO imebaki Amini nakwambia yasikukute
 
Ukiwa umezama kwenye maji ile pumzi unayoipata baada ya kuibuka ndio inayotakiwa kukufanya uishi, ishi maisha kama yanavyokuja, hutakiwi kujiua. Kwenye maisha fanya unavyoweza ili uishi tu. Watu hawatakupa msaada, watakusema lakini wewe ndo unajijua, ukishindwa kula leo utakula kesho. Bora wewe ulieuza kuku kwa hasara, mimi nimewahi kuwekeza hela yote nliokuanayo na sikurudisha hata mia. Nilikaa ndani zaidi ya mwaka, lakini mwisho wa siku nikatoka. Na leo hii huyu hapa, haya yote yanaisha.
 
POLENI NA MAJUKUMU ( ee, MUNGU nisaidie)

Mimi ni kijana ambaye utoto wangu nimeishi maisha ya uyatima nasema hivi kwa kuwa tangu nizaliwe sijawahi kumwona mama wala sijui baba yangu anafananaje maana naambiwa mama alifariki nikiwa na umri wa miezi mitatu na baba hapo hapo akaniacha nikiwa na umri huo hivyo nimelelewa na bibi mzaa mama hadi kufikia umri wa kwenda shule ambapo hapo nimelelewa na baba mdogo kutoka darasa la kwanza

Baba mzazi sijawahi kumuona ila niliona maiti yake nikiwa darasa la tatu ambayo yalisafirishwa kutoka huko alikokuwa akiishi
Maisha yangu yamekuwa ya mateso muda WOTE hakuna siku nimewahi kupata raha au faraja katika maisha yangu nimeteseka sana ,nimefanya kazi kama mtumwa ,nimelala sana na njaa ( kulala siku mbili,au tatu bila kula sio jambo la kushangaza imekuwa kawaida yangu

Niseme wazi licha ya baba mdogo kuwa na hali ngumu ya maisha lakini kanisaidia kusoma hadi chuo cha UALIMU ngazi ya cheti (UALIMU shule za msingi) sina budi kumshukuru japo michango mingi na ada za shule nimelipiwa na tasisi mbalimbali hivyo yeye alikuwa mlezi wangu japo alikuwa akinipa na hela ndogo ndogo za matumizi licha ya kuwa anawatoto wake na hali ngumu ya maisha

Baada ya kumaliza chuo cha UALIMU mwaka 2015 nikaona kama ndo ukombozi wangu maana miezi na siku yoyote nitaajiriwa lakini mpaka Leo sijapata ajira ,nimefanya vibarua na kago mtaani làkini kila ninachokipata hakijawahi fanikisha malengo yangu kabisa kabisa nimeishia kukopwa na jamaa,marafiki na ndugu lakini ubaya wake hawajawai nirejeshea pesa zangu nimekuwa ni mtu wa kufanya bidii na kuhangaika huku na huku hakuna siku nimepata faraja katika maisha yangu

Kumbuka hapa nilipo siwezi kurudi kwa baba mlezi kwa maana umri wake umeenda na hajiwezi tena na Mimi nimekuwa nikijitahidi kumkumbuka kwa kadri ya kidogo nachopata lakini kadri siku zinavyoenda ndo hali yangu inazidi kuwa mbaya zaidi,

Nipo kwenye matatizo na majaribu mazito hapa nilipo sijala chochote toka juzi na macho yamevimba kutokana na kulia muda wote usingizi hamna kabisakabisa na nimeishiwa chakari kabisa hapa nimebakiwa na mia sita kwa ajiri ya kununulia sumu tu

Hali yangu ya maisha imekuwa ngumu mno na nilijaribu kuomba ushauri kwa baadhi ya watu wakaniambia nyota yako imechafuka hivyo unapaswa uende kwa wataalamu wasafishe nyota Leo Nina miezi kadhaa tangu niende huko sijapata hata tone la fanikio nimeishia kutoa pesa zangu nilizotafuta kwa jasho jingi


Nimehangaika sana nimehangaika mno sina namna ya kujikwamua sioni upenyo wowote yaani mbele sioni kabisakabisa ninaowadai wamenifungia simu zao na kuniblock mungu wape maisha mema unajua kujitoa kwangu kulikuwaje mpaka Leo nawaza hivi najua ni mapenzi yako ee mungu

Hii hali ilivyozidi kuwa mbaya siku hadi siku kule kijijini kulikuwa na mashamba ambayo walikuwa wakilima na kuyatumia wazazi wangu hivyo baada ya wao kutangulia mbele za haki baba mlezi kanipatia hayo mashamba NA kaniambia wazi kuwa niyauze ili nipate pa kuanzia lakini baada ya kuuza hayo mashamba ndo nimezidi kuumia kwa zaidi ya Mara mia zaidi

Pesa iliyopatikana niliamua kufanya ufugaji wa kuku lakini katika vifaranga 150 nilivyoanza navyo vilikufa na kubaki 11 tu na baadae vimefikia umri wa kutaga vikafa tena vikabaki 5 tu ambavyo niliamua kuuza kwa bei ya hasara

Nimefanya mengi bila mafanikio
Nimejiunga na shirika moja la ujasiriamali la utengenezaji bidhaa za viwandani lakini baadae likafungiwa maana lilikuwa halina usajiri kila nachogusa ndo kinaniumiza zaidi

Pesa niliyokuwa nimetunza sehemu iliyobaki baada ya kuuza mashamba kuna mtu kanishauri kuwekeza katika forex MUNGU WE MUNGU WE EEE MUNGU (MJINGA MM)

Jamani MUNGU nimekosa nini mm mbona kila jambo nalogusa sifanikiwi kibaya zaidi unaniacha nahangaika na kulala na njaa siku zote hizi mbona nikipata huwa nasaidia kila aliyeniomba msaada kwanini mm nipo hivi EE MUNGU NIMEKOSA NINI MM?

jamani nateseka sina cha kutegemea tena hali yangu imezorota sana nimekonda hakuna mfano, uso mzito maana Nina siku mbili ndani nimelala tu nashindia kulia tu sijala Leo naenda siku ya tatu

Jamani nimeingia huko forex nimeliwa kila kitu,TV na sabufa nimeuza kitanda nimeuza,simu nayo nataka niuze kwa ajiri ya nauli navyoenda kunywa sumu maana nimepanga kunywea mbali na meneo haya tena mtoni ili kupoteza ushahidi


Nimeshakata tamaa kabisakabisa naomba naomba kwa mwenye msaada wa mawazo yoyote ya kuninusuru maisha yangu anisaidie ,pia kama kuna mtu yeyote mwenye kuweza kunisaidia kupata ajira huko serikalini nisaidieni maana kama vyeti ninavyo na nimetuma maombi ya ajira Mara kadhaa serikalini bila mafanikio

Nisaidieni jamani nisaidieni jamani

Hapa chini utaona screenshot ya trade nilizounguza katika mfumo wa dola



Naombeni msaada wa hali NA Mali nisaidieni nisipoteze roho yangu kwa njaa ama kujiua

Naombeni msaada wenu nisaidieni mm msaada wenu tafadhali nipatiwe msaada
Wa mawazo
Au nipate ajira serikalini
Msaada hata pesa nitashukuru zaidi


Ahsante



Pia nimeambatanisha barua niliyoandikiwa na kijiji kipindi naenda chuo kama uthibitisho


Nimeandika ukweli mtupu japo tabu na mateso mengi niliyopitia sijaandika ila utayeguswa kwa namna yoyote ile nitashukuru kwa msaada wakoView attachment 1180631View attachment 1180647
Kwanini hukwenda kuchota mafuta pale Msamvu ?
 
by the way kuna kipindi huyu mdau alikuwa anatafuta watu wenye visa vya kweli ili aweze kuvitengeneza katika movie.., huenda hii ikawa opportunity as well as kusaidia vijana wengine wasije-ingia kwenye risky business

Superman
 
Usimlilie Mungu kama haujajizogeza karibu, kilio chako hatakisikia kama hutatubu makosa yako kwanza, yaani UTUBU, hapo Mungu atakutizama kama Mwanae na atakuhudumia utabaki kutoa ushuhuda tu, Ushauri wangu ni kwamba tafuta kanisa lolote la kiroho, sio kwa nabii au mtume, Kanisa la kiroho, mueleze Mchungaji atakusaidia tu. Ukijiua ujue moto hukumu inakusubiri.
 
POLENI NA MAJUKUMU ( ee, MUNGU nisaidie)

Mimi ni kijana ambaye utoto wangu nimeishi maisha ya uyatima nasema hivi kwa kuwa tangu nizaliwe sijawahi kumwona mama wala sijui baba yangu anafananaje maana naambiwa mama alifariki nikiwa na umri wa miezi mitatu na baba hapo hapo akaniacha nikiwa na umri huo hivyo nimelelewa na bibi mzaa mama hadi kufikia umri wa kwenda shule ambapo hapo nimelelewa na baba mdogo kutoka darasa la kwanza

Baba mzazi sijawahi kumuona ila niliona maiti yake nikiwa darasa la tatu ambayo yalisafirishwa kutoka huko alikokuwa akiishi
Maisha yangu yamekuwa ya mateso muda WOTE hakuna siku nimewahi kupata raha au faraja katika maisha yangu nimeteseka sana ,nimefanya kazi kama mtumwa ,nimelala sana na njaa ( kulala siku mbili,au tatu bila kula sio jambo la kushangaza imekuwa kawaida yangu

Niseme wazi licha ya baba mdogo kuwa na hali ngumu ya maisha lakini kanisaidia kusoma hadi chuo cha UALIMU ngazi ya cheti (UALIMU shule za msingi) sina budi kumshukuru japo michango mingi na ada za shule nimelipiwa na tasisi mbalimbali hivyo yeye alikuwa mlezi wangu japo alikuwa akinipa na hela ndogo ndogo za matumizi licha ya kuwa anawatoto wake na hali ngumu ya maisha

Baada ya kumaliza chuo cha UALIMU mwaka 2015 nikaona kama ndo ukombozi wangu maana miezi na siku yoyote nitaajiriwa lakini mpaka Leo sijapata ajira ,nimefanya vibarua na kago mtaani làkini kila ninachokipata hakijawahi fanikisha malengo yangu kabisa kabisa nimeishia kukopwa na jamaa,marafiki na ndugu lakini ubaya wake hawajawai nirejeshea pesa zangu nimekuwa ni mtu wa kufanya bidii na kuhangaika huku na huku hakuna siku nimepata faraja katika maisha yangu

Kumbuka hapa nilipo siwezi kurudi kwa baba mlezi kwa maana umri wake umeenda na hajiwezi tena na Mimi nimekuwa nikijitahidi kumkumbuka kwa kadri ya kidogo nachopata lakini kadri siku zinavyoenda ndo hali yangu inazidi kuwa mbaya zaidi,

Nipo kwenye matatizo na majaribu mazito hapa nilipo sijala chochote toka juzi na macho yamevimba kutokana na kulia muda wote usingizi hamna kabisakabisa na nimeishiwa chakari kabisa hapa nimebakiwa na mia sita kwa ajiri ya kununulia sumu tu

Hali yangu ya maisha imekuwa ngumu mno na nilijaribu kuomba ushauri kwa baadhi ya watu wakaniambia nyota yako imechafuka hivyo unapaswa uende kwa wataalamu wasafishe nyota Leo Nina miezi kadhaa tangu niende huko sijapata hata tone la fanikio nimeishia kutoa pesa zangu nilizotafuta kwa jasho jingi


Nimehangaika sana nimehangaika mno sina namna ya kujikwamua sioni upenyo wowote yaani mbele sioni kabisakabisa ninaowadai wamenifungia simu zao na kuniblock mungu wape maisha mema unajua kujitoa kwangu kulikuwaje mpaka Leo nawaza hivi najua ni mapenzi yako ee mungu

Hii hali ilivyozidi kuwa mbaya siku hadi siku kule kijijini kulikuwa na mashamba ambayo walikuwa wakilima na kuyatumia wazazi wangu hivyo baada ya wao kutangulia mbele za haki baba mlezi kanipatia hayo mashamba NA kaniambia wazi kuwa niyauze ili nipate pa kuanzia lakini baada ya kuuza hayo mashamba ndo nimezidi kuumia kwa zaidi ya Mara mia zaidi

Pesa iliyopatikana niliamua kufanya ufugaji wa kuku lakini katika vifaranga 150 nilivyoanza navyo vilikufa na kubaki 11 tu na baadae vimefikia umri wa kutaga vikafa tena vikabaki 5 tu ambavyo niliamua kuuza kwa bei ya hasara

Nimefanya mengi bila mafanikio
Nimejiunga na shirika moja la ujasiriamali la utengenezaji bidhaa za viwandani lakini baadae likafungiwa maana lilikuwa halina usajiri kila nachogusa ndo kinaniumiza zaidi

Pesa niliyokuwa nimetunza sehemu iliyobaki baada ya kuuza mashamba kuna mtu kanishauri kuwekeza katika forex MUNGU WE MUNGU WE EEE MUNGU (MJINGA MM)

Jamani MUNGU nimekosa nini mm mbona kila jambo nalogusa sifanikiwi kibaya zaidi unaniacha nahangaika na kulala na njaa siku zote hizi mbona nikipata huwa nasaidia kila aliyeniomba msaada kwanini mm nipo hivi EE MUNGU NIMEKOSA NINI MM?

jamani nateseka sina cha kutegemea tena hali yangu imezorota sana nimekonda hakuna mfano, uso mzito maana Nina siku mbili ndani nimelala tu nashindia kulia tu sijala Leo naenda siku ya tatu

Jamani nimeingia huko forex nimeliwa kila kitu,TV na sabufa nimeuza kitanda nimeuza,simu nayo nataka niuze kwa ajiri ya nauli navyoenda kunywa sumu maana nimepanga kunywea mbali na meneo haya tena mtoni ili kupoteza ushahidi


Nimeshakata tamaa kabisakabisa naomba naomba kwa mwenye msaada wa mawazo yoyote ya kuninusuru maisha yangu anisaidie ,pia kama kuna mtu yeyote mwenye kuweza kunisaidia kupata ajira huko serikalini nisaidieni maana kama vyeti ninavyo na nimetuma maombi ya ajira Mara kadhaa serikalini bila mafanikio

Nisaidieni jamani nisaidieni jamani

Hapa chini utaona screenshot ya trade nilizounguza katika mfumo wa dola



Naombeni msaada wa hali NA Mali nisaidieni nisipoteze roho yangu kwa njaa ama kujiua

Naombeni msaada wenu nisaidieni mm msaada wenu tafadhali nipatiwe msaada
Wa mawazo
Au nipate ajira serikalini
Msaada hata pesa nitashukuru zaidi


Ahsante



Pia nimeambatanisha barua niliyoandikiwa na kijiji kipindi naenda chuo kama uthibitisho


Nimeandika ukweli mtupu japo tabu na mateso mengi niliyopitia sijaandika ila utayeguswa kwa namna yoyote ile nitashukuru kwa msaada wakoView attachment 1180631View attachment 1180647
Sijaona hata sababu inayokufanya kuona kifo ni suluhu yake, nimepitia nyuzi zako nimeona unachukulia maisha kama bahati nasibu ndiyo maana unatafuta waganga, nimetafakari sanaaaa, ila kilichonishangaza unalalamika hauna pesa ila haudaiwi na mtu bali wewe unadai.kutokana na tafakri yangu huu ndio ushauri wangu.

1. Kuwaza kujiua ni upumbavu hasa unaoandamana na matatizo ya kiakili

2. Kulaumu watu unaowadai kwa kushindwa kukulipa nao ni upumbavu. Kuna watu hawana pesa ya kula na wanamadeni na hawajui watapata wapi pesa na matumaini wanayo makubwa

3. Chakula hata ukitoka hapo ukaenda kwa jirani naamini utapata chakula. Niliwahi funga siku mbili usiku na mchana bila kula wala kunywa lakini sikufa, amuka nenda kwa jirani nenda hata kaanguke uwanjani kwake ukilia njaaa nawe utapata msaada

4. Maisha siyo lelemama, usifikri ukifa dunia itapoteza wewe ndiyo utapotea na maisha yataendelea. Jiulize mimi niliyesoma uzi wako ukifa nitapoteza nini?

5. Chanzo cha matatizo yako ni wewe mwenyewe wala si mwingine, nakutakia kifo chema.
 
Ukisoma haya maelezo sio siri kuna chumvi humu imeongezeka,machale yananicheza nahisi kuna utapeli
OK hayajakukuta ukweli ninao mm wala sio lazima ukanisaidia kipesa nimeomba tu ushauri pia nimeomba kwa wenye connection serikalini kupata ajira kama ikibidi kuhusu kumsaidia mtu sioni kama kila aombaye msaada ni tapeli tusameheane mkuu sisi sote. Tunapita
 
Kosa kubwa unalofanya ni kukata tamaa..

Hivi unafikiri hayo unayoyapitia uko peke yako, kuna lundo la watu wana matatizo zaidi ya hayo!!

Ebu amka na ishi maisha yako, usitake kuniambia kwamba umekosa kabisa kazi ya kufanya!

Pambana kijana, mwanaume hutakiwi kulia lia.. Shida zipo tu.. Kila mtu akieleza maswahibu yake humu utajiona una afadhali!
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom