Nimeshakata motor vehicle licence kabla ya siku ya bajeti. Je, nitarudishiwa pesa zangu na TRA?

Mdanganywa

JF-Expert Member
Jun 15, 2009
620
342
Jamani,

Mimi nime-renew Motor Vehicle license yangu wiki moja kabla ya bajeti kusomwa, tena ni shs. 230,000/=.

Sasa bajeti imesomwa nasikia kwamba kuanzia July 01, 2017 hazitafanya kazi. Maana yake nimeingia hasara.

Je, nitarudishiwa hela yagu nikienda TRA.

Nasema ni hasara kwa sababu wengi ambao renewals zao ni mwezi huu bada ya kusikia bajeti wako radhi kuweka magari nyumbani hadi July 01.

Mimi nilikata kwa sababu tu expiry ilikuwa wiki moja kabla ya bajeti.

Saidia kupata jibu na haki yangu.
 
Inaanza tarehe 1 July, hivyo imetoka hiyooo kwa sababu kwa mwezi huu ungekuwa na kosa la kutokuwa nayo.

Hii imekumba wengi na ndio hivyo tena.
 
Faraja kwako ni kwamba mwakani hutalipa tena, kwa sasa imetoka hiyoo!
 
effective date ni kuanzia tarehe 01 July, so wewe Umekata kabla ya tarehe tajwa - kubali maumivu.
 
mimi niko nje ya nchi kwa miaka 3 sasa nadaiwa mpaka basi na nilikua nikija nyumbani napanda daladala tu maana nafiria kuipia gari laki 6 kwa kuipanda wiki moja tu aaaa wapi bora nipande mwendo kasi na daladala.... ila sasa aaaa nikirudi naiwasha kabisa japo tayari inabidi niifanyie service ya kufa mtu, at the end ndio yale yale ila for the future nimeipenda sana kwa upande wangu ambae naitumia hiyo road wiki mbili kwa mwaka
 
Yangu inaisha Tarehe 19/6/2017 na Traffic watakavyokuwa na hasira ya kukusanya za mwisho mwisho ni wakati wa kusahau gari kuanzia tar 20 mpka tareh 1/7 kuepuka kulipa RL week moja kabla haijafutwa rasmi..
 
mimi niko nje ya nchi kwa miaka 3 sasa nadaiwa mpaka basi na nilikua nikija nyumbani napanda daladala tu maana nafiria kuipia gari laki 6 kwa kuipanda wiki moja tu aaaa wapi bora nipande mwendo kasi na daladala.... ila sasa aaaa nikirudi naiwasha kabisa japo tayari inabidi niifanyie service ya kufa mtu, at the end ndio yale yale ila for the future nimeipenda sana kwa upande wangu ambae naitumia hiyo road wiki mbili kwa mwaka

Sheria inaanza kutumika tar moja julai 2017. Deni la nyuma ya hapo lipo palepale sema tu halitaongezeka wala kuwa na riba. Kwenye TIN yako limewekwa tayari ingawa kuendesha gari utaendesha ila deni ulilokuwa nalo halitafutwa kwa kuwa lilikuwepo kwa mujibu wa sheria iliyopo
 
Jamani,

Mimi nime-renew Motor Vehicle license yangu wiki moja kabla ya bajeti kusomwa, tena ni shs. 230,000/=.

Sasa bajeti imesomwa nasikia kwamba kuanzia July 01, 2017 hazitafanya kazi. Maana yake nimeingia hasara.

Je, nitarudishiwa hela yagu nikienda TRA.

Nasema ni hasara kwa sababu wengi ambao renewals zao ni mwezi huu bada ya kusikia bajeti wako radhi kuweka magari nyumbani hadi July 01.

Mimi nilikata kwa sababu tu expiry ilikuwa wiki moja kabla ya bajeti.

Saidia kupata jibu na haki yangu.
Ndugu, wewe umetimiza wajibu wako kisheria, kutembea na gari haina hivyo vibali kabla ya terehe 1 July ni kuwatafutia Traffic Ulaji.
Kuna sehemu utakuja kuwa compansated tu.
 
Back
Top Bottom