Buza Kwa Mpalange
JF-Expert Member
- Apr 15, 2020
- 268
- 156
Moja kwa moja kwenye mada,
Hii kampuni ya kuitwa TTCL Customer Care imekuwa hawajali kabisa wananchi wa kipato cha chini kabisa.
Mwanzo walikuwa na vifurushi rafiki sana, Watanzania tukaanza kuwaamini tukaona ndio wanatutoa kwenye mikono ya utawala wa kinyonyaji wa mabeberu akina VodaCom, Airtel, Halotel, Tigo, Smart na Smile.
Tukaanza kuambiwa TURUDI NYUMBANI KUMENOGA, tukaamua kurudi, tukarudi kweli. Tarehe kama ya 27 Julai 2020 unajua kilichotokea? Watu bado tupo kwenye majonzi ya kuondokewa na mpendwa wetu Rais Mstaafu Mkapa na TTCL si wakaamua kutuongezea kilio zaidi
Ile tumetoka kuzika tukaona tujifariji hata kuingia mtandaoni kupata habari, tunajaribu kupiga *148*30#
TOBOA NIGHT hakuna
BANDUKA BANDUA holaa
Tukapiga *150*71# kucheki BANDO TAMTAM ndio hakuna kitu
Nikasema ngoja nikachungulie UNI PACK kule ndio kabisaaa.
Kuanzia leo mimi sitatumia tena mtandao wa TTCL, kama mkataa kwao ni mtumwa bora niende ugenini niwe mtumwa ila nipate huduma nzuri.
Hawana SMS za kuchombeza wateja, yaani hata kutuma sms ya kumkumbushia kama kuna huduma mpya.
Costomer Care wana lugha mbovu, majibu ya nyodo na dharau juu mpaka unapata hasira.
Wanaosajili laini mitaaani ndio hatuwaoni kabisa.
Muda wa kurudi HALOTEL na VodaCom ndiyo huu.
Halotel, VodaCom, Tigo na Zantel nisameheni sana shetani alinishawishi nirudi nyumbani kumenoga kumbe alinidanganya.
Ulaaniwe sana shetani.
Hii kampuni ya kuitwa TTCL Customer Care imekuwa hawajali kabisa wananchi wa kipato cha chini kabisa.
Mwanzo walikuwa na vifurushi rafiki sana, Watanzania tukaanza kuwaamini tukaona ndio wanatutoa kwenye mikono ya utawala wa kinyonyaji wa mabeberu akina VodaCom, Airtel, Halotel, Tigo, Smart na Smile.
Tukaanza kuambiwa TURUDI NYUMBANI KUMENOGA, tukaamua kurudi, tukarudi kweli. Tarehe kama ya 27 Julai 2020 unajua kilichotokea? Watu bado tupo kwenye majonzi ya kuondokewa na mpendwa wetu Rais Mstaafu Mkapa na TTCL si wakaamua kutuongezea kilio zaidi
Ile tumetoka kuzika tukaona tujifariji hata kuingia mtandaoni kupata habari, tunajaribu kupiga *148*30#
TOBOA NIGHT hakuna
BANDUKA BANDUA holaa
Tukapiga *150*71# kucheki BANDO TAMTAM ndio hakuna kitu
Nikasema ngoja nikachungulie UNI PACK kule ndio kabisaaa.
Kuanzia leo mimi sitatumia tena mtandao wa TTCL, kama mkataa kwao ni mtumwa bora niende ugenini niwe mtumwa ila nipate huduma nzuri.
Hawana SMS za kuchombeza wateja, yaani hata kutuma sms ya kumkumbushia kama kuna huduma mpya.
Costomer Care wana lugha mbovu, majibu ya nyodo na dharau juu mpaka unapata hasira.
Wanaosajili laini mitaaani ndio hatuwaoni kabisa.
Muda wa kurudi HALOTEL na VodaCom ndiyo huu.
Halotel, VodaCom, Tigo na Zantel nisameheni sana shetani alinishawishi nirudi nyumbani kumenoga kumbe alinidanganya.
Ulaaniwe sana shetani.