Nimeridhika kabisa: Mbwana Samatta hakuwa msaada kwa Aston Villa, Watkins ameonesha utofauti mkubwa

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,174
25,446
Kwa kiwango chake, ufungaji wake, kazi yake, umakini wake na mchango wake kwa timu mchezaji mpya wa Aston Villa Ollie Watkins amedhihirisha kuwa mshambuliaji Mbwana Samatta hakuwa msaada wowote kwa timu hiyo.

Watkins ambaye amefunga mabao matatu katika kipigo cha mbwakoko alichokipata Liverpool ambaye ni bingwa mtetezi leo cha mabao 7-2, ni wazi kuwa Samatta alikuwa mzigo kwa Aston Villa.

Ukweli usemwe, Samatta hakuwa na kiwango cha kuwika Premier League na kuwa msaada kwa Aston Villa. Labda awike huko Uturuki alipo. Watkins ni moto!
 
Leo pia nimeweka historia mpya kwamba Liverpool alifungwa kwa mara ya mwisho bao 7 mwaka 1963 na Tottenham,pia mara ya mwisho bingwa mtetezi kufungwa bao 7 ilikuwa mwaka 1993 pale Arsenal alipochapwa na ''''''''::::: hii ligi inalaana ,yote kwa yote pole Samata lakini hongera pia kwa kuondoka mapema maana ni balaaaaaa
 
Samata alikua mzito ukiangalia speed ya EPL ilivyo...lakini umeandika kumkandamiza sana Samata.

Aston Villa yote ilikua down msimu uliyopita,hata Samata alipelekwa kama Kui rescue timu...angekuwepo hata sasa angefunga goli mbili tatu Vila imechanganya Kule mbele sa hvi...hata hivyo Watkins ni dope...dribbling... Shootings... Positioning.

Mpumzisheni Samatta acheze mpira kashatoka Aston Villa...alipofeli inabidi iwe starting point kwa wachezaji watu badala ya kushinda kumkejeli mchana na usiku.
 
Samatta ni wa kawaida sana

Wewe ni wa tofauti! Mwenzako salary inasoma kila wiki. Wewe kila wiki uko mahakamani kuvizia watuhumiwa wa uhujumu uchumi ili upate chochote.

Unazingua Wakili msomi. Tusimkatishe tamaa mtu ambaye ni mpambanaji kuliko sisi. Ni Mtanzania wa kwanza kati ya Watanzania karibia milioni 60 kucheza EPL, kucheza GENK, Ligi ya Mabingwa Ulaya, Europa Ligi! Nk.

Halafu unasema Samatta ni wa kawaida sana!! Sikubaliani na wewe.
 
Kwa kiwango chake, ufungaji wake, kazi yake, umakini wake na mchango wake kwa timu mchezaji mpya wa Aston Villa Ollie Watkins amedhihirisha kuwa mshambuliaji Mbwana Samatta hakuwa msaada wowote kwa timu hiyo.

Watkins ambaye amefunga mabao matatu katika kipigo cha mbwakoko alichokipata Liverpool ambaye ni bingwa mtetezi leo cha mabao 7-2, ni wazi kuwa Samatta alikuwa mzigo kwa Aston Villa.

Ukweli usemwe, Samatta hakuwa na kiwango cha kuwika Premier League na kuwa msaada kwa Aston Villa. Labda awike huko Uturuki alipo. Watkins ni moto!
Vivyo hivyo samata amefiti kwa fernerbahec au hujaona
 
Wewe ni wa tofauti! Mwenzako salary inasoma kila wiki. Wewe kila wiki uko mahakamani kuvizia watuhumiwa wa uhujumu uchumi ili upate chochote.

Unazingua Wakili msomi. Tusimkatishe tamaa mtu ambaye ni mpambanaji kuliko sisi. Ni Mtanzania wa kwanza kati ya Watanzania karibia milioni 60 kucheza EPL, kucheza GENK, Ligi ya Mabingwa Ulaya, Europa Ligi! Nk.

Halafu unasema Samatta ni wa kawaida sana!! Sikubaliani na wewe.
Hoja hapa ni kiwango cha uwanjani cha Samatta kama mcheza soka. Hakuna haja ya kuzungumzia kipato na kazi za watu. Mkuu, tujadili kiwango cha Samatta cha uwanjani na kuacha mambo mengine yasiyohusika hapa. Kumbuka, kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake.
 
Wewe ni wa tofauti! Mwenzako salary inasoma kila wiki. Wewe kila wiki uko mahakamani kuvizia watuhumiwa wa uhujumu uchumi ili upate chochote.

Unazingua Wakili msomi. Tusimkatishe tamaa mtu ambaye ni mpambanaji kuliko sisi. Ni Mtanzania wa kwanza kati ya Watanzania karibia milioni 60 kucheza EPL, kucheza GENK, Ligi ya Mabingwa Ulaya, Europa Ligi! Nk.

Halafu unasema Samatta ni wa kawaida sana!! Sikubaliani na wewe.
Hahahahahah nimecheka kweli .

Wakati Samata analamba milioni 120

Yeye anagonja milioni 1 yenya Makato ya mkopo .
 
23 Reactions
Reply
Back
Top Bottom