Nimeridhika kabisa: Mbwana Samatta hakuwa msaada kwa Aston Villa, Watkins ameonesha utofauti mkubwa

Laki mbili na nusu! Nina digrii huku Samatta akiwa kaishia kidato cha nne tu! Ndiyo sababu namheshimu na kuwapuuza wale wote wanao mchukulia kama mtu wa kawaida katika kipengele chochote kile, akiwemo huyo Mrs Petro hapo juu.
Ukishobokea hela uta abudu watu, ridhika na unacho kipata , wewe huna hela nyingi una elimu, yeye hana elimu kubwa ana hela nyingi mzani ume balance tuliza moyo wako
 
Huu mjadala tuufunge. Naona unanichosha tu. Nisije nikawa nabishana na mke wa mtoa mada humu! maana jina lako halijafungamana na jinsia yoyote ile na kwa namna unavyonitolea maneno ya dharau na maudhi, inanipa walakini.
Mnaofikiria kitopian huwa akili zenu kama kamasy. M.f
 
Kwa kiwango chake, ufungaji wake, kazi yake, umakini wake na mchango wake kwa timu mchezaji mpya wa Aston Villa Ollie Watkins amedhihirisha kuwa mshambuliaji Mbwana Samatta hakuwa msaada wowote kwa timu hiyo.

Watkins ambaye amefunga mabao matatu katika kipigo cha mbwakoko alichokipata Liverpool ambaye ni bingwa mtetezi leo cha mabao 7-2, ni wazi kuwa Samatta alikuwa mzigo kwa Aston Villa.

Ukweli usemwe, Samatta hakuwa na kiwango cha kuwika Premier League na kuwa msaada kwa Aston Villa. Labda awike huko Uturuki alipo. Watkins ni moto!
samatta ligi zote anacheza pale avfc alikuwa hapewi pasi stahili za kuscore hadi akatafute huko tofauti na watkins
 
Ndo mana huwa nilitamani sana bahati aliopata samatta angepata msuva angekua zaidi ya pale alipo samatta sasa hivi!!!

Msuva ni fighter hata uchezaji wake katika timu ya taifa mnauona kuliko huyo samatta!
Kwann unaita bahati, Msuva anacheza ligi ya Morocco angekua na uwezo huo hata timu za Spain au French zingeshamuona
 
Samara kilichomtibulia pale ni Corona pale ulipoingia mara ya kwanza ligi iliposimama ......lakini kabla ya hapo sama goal alifanya vizuri tu ndani ya timu ikumbukwe aliwafunga goli Liverpool wakiwa full mkoko....na pia kama sikosei aliifungia goli Villa dhidi ya man city...
Kipindi analetwa samata timu ile haikua ktk hali nzuri na ndio kisa analetwa yeye sasa kaivusha timu imemtoa kwa mkopo majeruhi wake wamerudi na wamesajili timu imebadilika kiasi eti inaonekana samata hakua msaada la hasha
Washabiki wa Yanga sasa hivi nao wanasema kwa Yanga hii molinga angefunga sana!....lkn kipindi hicho thamani yake haikuonekana
Naamini hata sasa samata akirudi ndani ya timu hiyo atafanya makubwa tu
 
Samara kilichomtibulia pale ni Corona pale ulipoingia mara ya kwanza ligi iliposimama ......lakini kabla ya hapo sama goal alifanya vizuri tu ndani ya timu ikumbukwe aliwafunga goli Liverpool wakiwa full mkoko....na pia kama sikosei aliifungia goli Villa dhidi ya man city...
Kipindi analetwa samata timu ile haikua ktk hali nzuri na ndio kisa analetwa yeye sasa kaivusha timu imemtoa kwa mkopo majeruhi wake wamerudi na wamesajili timu imebadilika kiasi eti inaonekana samata hakua msaada la hasha
Washabiki wa Yanga sasa hivi nao wanasema kwa Yanga hii molinga angefunga sana!....lkn kipindi hicho thamani yake haikuonekana
Naamini hata sasa samata akirudi ndani ya timu hiyo atafanya makubwa tu
Wewe ndio kocha ungemrudisha??
 
Back
Top Bottom