mambio
JF-Expert Member
- Mar 4, 2017
- 2,345
- 2,769
Nimejikuta nashawishika kwa mara ya kwanza kuandika uzi humu jukwaani kwani miaka yote nimekuwa msomaji na mchangiaji tu!
Hii ni baada ya jana kupitia uzi wa mkuu TORABORA akiwa haelewi hatma ya maisha yake.
Picha linaanza. Nina elimu ya kawaida ambayo Watanzania wengi wanayo kwa sasa. Sijawahi kuajiriwa kwani ajira haijawahi kuwa kipaumbele ktk maisha yangu.
Tangu nikiwa home kipindi hicho usukani sahani break mkeka (kula bure kulala bure) nilikuwa mtu wa kujichanganya sana kwenye mishe tofauti hadi nikafanikiwa kutengeneza kigheto changu cha kitozi chenye full furniture kwa kipindi hicho nikiwa bado home.
Nikaaga home nikaingia street kupanga. Hapo hasira zikaongezeka mara dufu kila fursa + kazi, zilizopita mbele yangu hazikunipita. Kwa ujumla nilijituma sana na kukubalika sana.
Starehe zangu tangu nikiwa school ni hizi za kawaida yaani ganja sana, mziki, tungi kiaina. Japo kwa sasa nimepunguza sana.
Mungu akazidi kuwa upande wangu nikanunua kiwanja Chanika, nikanunua shamba heka moja Mvuti pia nikafanikiwa kununua eneo lingine Zingiziwa.
Mungu hakuniacha, nikaanza ujenzi Chanika. Mwaka 2016 nikahamia rasmi kwenye banda langu.
Nikakodi fremu mtaani nikafungua duka tigo pesa + gesi na makorakoro kibao.
Hapo ndipo picha kamili likaanza maisha yangu yakawa hayaeleweki mishe zangu haziendi. Yaani kila ninachofanya kinaleta matokeo hasi.
Nimepambana hadi 2019 mwanzoni hali yangu ya uchumi ikazidi kuwa mbaya zaidi. Kiduka nacho kikafilisika japo bado kipo kinachechemea baada ya kumpa mtu wa mshahara.
Mambo yamegoma kwenda, nimepoteza hadi marafiki sababu nadhani hawanielewi nimekuwaje. Nimekuwa mtu wa hofu bila sababu sijiamini kabisa yani.
Kuna kipindi nawaza kuinyofoa roho yangu ila nikiiangalia family nasita kidogo.
Mbaya zaidi nimekuwa mtu wa kushinda ndani muda mwingi sana. Nimekuwa mpweke balaa. Kichwa kimekuwa kizito, ubunifu zero kabisa!
Ni imani yangu kuna mahala nilikosea au kuna shida mahali. Nimelileta kwenu wakuu maana nadhani kwa ukubwa wa jukwaa hili kuna uwezekano kuna waliopitia haya nnayopitia au kuna wenye maono + maoni ya kujua na kushauri kuhusu hili tatizo langu.
Asanteni
Hii ni baada ya jana kupitia uzi wa mkuu TORABORA akiwa haelewi hatma ya maisha yake.
Picha linaanza. Nina elimu ya kawaida ambayo Watanzania wengi wanayo kwa sasa. Sijawahi kuajiriwa kwani ajira haijawahi kuwa kipaumbele ktk maisha yangu.
Tangu nikiwa home kipindi hicho usukani sahani break mkeka (kula bure kulala bure) nilikuwa mtu wa kujichanganya sana kwenye mishe tofauti hadi nikafanikiwa kutengeneza kigheto changu cha kitozi chenye full furniture kwa kipindi hicho nikiwa bado home.
Nikaaga home nikaingia street kupanga. Hapo hasira zikaongezeka mara dufu kila fursa + kazi, zilizopita mbele yangu hazikunipita. Kwa ujumla nilijituma sana na kukubalika sana.
Starehe zangu tangu nikiwa school ni hizi za kawaida yaani ganja sana, mziki, tungi kiaina. Japo kwa sasa nimepunguza sana.
Mungu akazidi kuwa upande wangu nikanunua kiwanja Chanika, nikanunua shamba heka moja Mvuti pia nikafanikiwa kununua eneo lingine Zingiziwa.
Mungu hakuniacha, nikaanza ujenzi Chanika. Mwaka 2016 nikahamia rasmi kwenye banda langu.
Nikakodi fremu mtaani nikafungua duka tigo pesa + gesi na makorakoro kibao.
Hapo ndipo picha kamili likaanza maisha yangu yakawa hayaeleweki mishe zangu haziendi. Yaani kila ninachofanya kinaleta matokeo hasi.
Nimepambana hadi 2019 mwanzoni hali yangu ya uchumi ikazidi kuwa mbaya zaidi. Kiduka nacho kikafilisika japo bado kipo kinachechemea baada ya kumpa mtu wa mshahara.
Mambo yamegoma kwenda, nimepoteza hadi marafiki sababu nadhani hawanielewi nimekuwaje. Nimekuwa mtu wa hofu bila sababu sijiamini kabisa yani.
Kuna kipindi nawaza kuinyofoa roho yangu ila nikiiangalia family nasita kidogo.
Mbaya zaidi nimekuwa mtu wa kushinda ndani muda mwingi sana. Nimekuwa mpweke balaa. Kichwa kimekuwa kizito, ubunifu zero kabisa!
Ni imani yangu kuna mahala nilikosea au kuna shida mahali. Nimelileta kwenu wakuu maana nadhani kwa ukubwa wa jukwaa hili kuna uwezekano kuna waliopitia haya nnayopitia au kuna wenye maono + maoni ya kujua na kushauri kuhusu hili tatizo langu.
Asanteni