Nimeponyeka kutapeliwa na rafiki wa facebook

Aisee hii kitu imenitokea wiki iliopita lakin mim nilimkaushia sikumpa namba yangu ya WhatsApp. Kwa sababu kuna ndugu yangu alinielezea juu ya utapeli wao Kwa hiyo nilishtuka mapema
Hata mm ilinitokezea kuna mmoja aliingia na kunitumia ujumbe wa salam nikamjibu mwisho akahitaji namba yangu ya watsap nikamkaushia.
 
"Mwanamke mmoja wa kizungu aliniomba urafiki huko Facebook, nikakubali na akaruka inbox siku hiyo hiyo.

Alijitambulisha kwa jina la Dkt.Christina kutoka London, Uingereza. Akasema yeye ni daktari bingwa wa magonjwa ya watoto katika hospital kubwa huko London. Pia anapenda kumtumikia Mungu katika kufariji na kutoa misaada kwa wenye hali ya chini.

Pia akasema akipata likizo basi atakuja Tanzania kwa ajili ya kufanya utalii, hivyo nitakuwa mwenyeji wake na angependa kufikia nyumbani kwangu (hakujua Kama mimi ni baharia naishi chumba kimoja na mtungi wa gesi ndani).

Nikajibu karibu sana. Akaomba kunifahamu kiufupi, nikamueleza na kuanzia hapo tukawa marafiki.

Basi akaniachia email yake hapo messenger kwa maana alisema kuwa sio mtumiaji sana wa Facebook hivyo nitumie email kuwasiliana nae.

Tukawa tunawasiliana kwa njia ya email. Badae akafuta picha na akaunti ya Facebook. Siku moja akaniambia kuwa walikuwa na kikao Cha wafanyakazi hapo hospital na baadhi ya wafanyakazi waliofanya vizuri walipewa zawadi. yeye alikuwa ni mmoja wao. Alipewa zawadi za laptop Hp 2, smartphone (iPhone) 1, na TV LG 1. Kwa maana yeye hakuwa na uhitaji wa vitu, basi akapata wazo la kunitumia mimi Kama zawadi ya kudumisha urafiki wetu.

Nilifurahi sana nikajua ghetto langu linakuja kunoga.

Siku moja akasema amepata dharura na anaenda Hawaii hivyo hatokuja Africa. Lakini zawadi zangu amempa rafiki yake anayeenda Senegal, ambaye ni mtumishi aliyemtaja kwa jina la Sister Janneth. Akanipa na email ya huyo Janneth ili niwasiliane nae jinsi ya kupata zawadi zangu. Janneth alikuwa akija Senegal na jopo lake kwa ajili ya kuhubiri injili na kutoa misaada.

Niliwasiliana na Janneth na akaniambia nimtumie post address yangu ili atume mzigo. Utata ulikuja pale aliponiambia kuwa nimtumie $150 kupitia benki ya Western Union ili aweze kuusafirisha huo mzigo.

Daah nilijiuliza maswali mengi sana, sasa Kama hawa wanagawa misaada wameshidwaje kunilipia gharama za kuusafirisha huo mzigo? nikapata jibu kuwa hawa Ni matapeli wa kizungu. Nikamjibu kuwa hiyo hela sina, kama vipi uza laptop moja halafu hela ya mauzocha ya parcel itumie kutuma huo mzigo utakaobaki.

Kuanzia siku hiyo hakunitafuta tena

Chanzo: Watu Na Story
🏃🏃🏃🏃kuna dogo hapa kitaaa alitengenezwa hivo hivo hadi akatumiwa picha ya parcel imeandikwa anuani na majina yake nkamwambia ww unaibiwa akabisha matokeo akatuma usd 120 kwa westernunion afu bilabila alikwapua hela dukani kwao akijua mzigo ukiingia Anauza iphone X moja tu kila kitu byeee🙄🙄🙄🙄🙄🙄🙄🙄
 
Mkuu hawa wamekuwa wengi sana mimi mwenyew kanitumia mapicha ya laptop, i
I phone, galaxy anasema kuna.mzigo katuma ethiopia ukifika ethiopia atacheki ndege ya mizigo inayokuja tz ahaaa na tumefahamiana juzi tu. matapeli ni wengi now
IMG-20230706-WA0019.jpg
IMG-20230706-WA0017.jpg
IMG-20230706-WA0016.jpg
Screenshot_20230707_103537.JPG
 
Nakumbuka ilikua live macho macho na TAPELI kampala sehemu moja Garden city/Jinja road alinikosa kidogo. Kisha akaniambia ur very lucky my friend.
 
Nami nilipona kutapeliwa na mtu wa aina hii huko Twitter akanitumia ujumbe kujitambulisha kwamba yeye ni Daktari yuko Ujerumani ila huwa anasaidia watu wenye shida kwani aliachiwa fedha nyingi za urithi na wazazi wake na kwamba hana familia, anaona ni vema azitumie kuwasaidia wenye shida kama alivyoachiwa maagizo na Baba yake ya kuwajali wenye shida.

Akajieleza kwamba anakuwa busy na kazi za utabibu hivyo muda mzuri wa kuwasiliana ni baada ya kutoka kazini na tuwasiliane kwa email

Kwanza aliuliza historia ya maisha yangu nikamweleza akasema yeye ni Mwanamke na anapenda kusaidia wanawake wajane akaomba niwatafute wajane wenzangu kila mtu aeleze matatizo yake, kilichofuata baada ya hapo tunaambiwa tumeni pesa tuwatumie mizigo yaani zawadi kutoka Ujerumani.

Nilishtuka kuona kajichanganya kanitumia email kwamba tuwasiliane ni tafaouti na alonitumia siku ya kwanza nikafungua email nyingine nikajitambulisha kwa jina lingine nikijifanya ni mtu mwingine nikauliza juu ya Shirika la kusaidia wenye shida ya matibabu akasema yeye si Daktari wala hajishughulishi kutoa msaada.

Tangia siku hiyo nikakata mawasiliano na sijawahi kumtafuta wala hajanitafuta, nikawaeleza wale wenzangu tukaachana na mpango wa kutuma pesa na kupenda misaada.







Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe ulikosea. Ungemwambia akutumie kitambulisho chake ili umtumie pesa. Akituma hapo ndo ungejua kumbe wala si mzungu. Anakutumia kitambulisho chake na pesa haumtumii. Halafu unamwambia unakwenda kumshitaki.
Wengine hutuma hadi passport zao kabisa
 
Back
Top Bottom