MK254
JF-Expert Member
- May 11, 2013
- 31,745
- 48,385
Kiukweli Afrika aidha hiki kitu kinatukosa kosa au kuna sababu zingine za kisayansi ambapo mpaka sasa hakijaonyesha makucha huku, kimetunusia tu, labda Waafrika weusi wawili ndio wameaga dunia, na hata hao wawili walikua na mambo mengine yanayowaathiri.
Wacha tuone hii show, ila nikitazama yanayotokea Italy taifa lenye uwezo mkubwa mara elfu zaidi yetu ila kinawatesa hadi wamepoteana, napata uwoga sana, tuendelee kuomba.
Nimepitia sehemu kwenye mtandao wa kijamii, wazungu wanashangaa sana kwanini hiki kitu kwa Afrika hakionekani kufanya lolote, wengine wanasema kipo huku tena sana ila ni vile hatuna uwezo wa kupima, nimewabishia sana maana kama ingekuwa kweli, basi tungekuwa tunaumwa wengi na kuanguka anguka japo bila ya kujua nini kinatuangusha maana uwezo wa kupima Corona haupo sana huku, ila wengi tunapeta tu mbona.
Wacha tuone hii show, ila nikitazama yanayotokea Italy taifa lenye uwezo mkubwa mara elfu zaidi yetu ila kinawatesa hadi wamepoteana, napata uwoga sana, tuendelee kuomba.
Nimepitia sehemu kwenye mtandao wa kijamii, wazungu wanashangaa sana kwanini hiki kitu kwa Afrika hakionekani kufanya lolote, wengine wanasema kipo huku tena sana ila ni vile hatuna uwezo wa kupima, nimewabishia sana maana kama ingekuwa kweli, basi tungekuwa tunaumwa wengi na kuanguka anguka japo bila ya kujua nini kinatuangusha maana uwezo wa kupima Corona haupo sana huku, ila wengi tunapeta tu mbona.