Nimepata ujauzito, nishaurini jinsi ya kukabiliana na mabadiliko ya hali ya mwili

Ushauri
Nenda cliniki utapewa ushauri jinsi yakutunza ujauzito, kuhusu kunya soda kila mara jitahidi kunya juisi na matunda kwa afya ya mwanao tumboni usimshindilie chemical zisizo na maana yeyote. Kama ujauzito wako ni chini ya miezi mitatu jiepushe na kazi ngumu za kuinama kama kudeki, kufua kwa muda mrefu, kupanda pikipiki, na kadhalika ili kujiepusha na kutoka kwa mimba.
Usitumie dawa yeyote bila kuruhusiwa na daktari hata kama ni pain killer mf. hedex ,nk
Kubali hali yako kuwa unakua mama sasa achana na second thoughts jiamini, Tena jiamini yote yanawezekana.
Mwisho Nenda clinic wewe na mwenza wako.
Asante kwa ushauri! Umenifanya nifikirie kiumbe aliyekua tumboni!!
 
Back
Top Bottom