Mondela
JF-Expert Member
- Aug 20, 2021
- 2,570
- 3,763
Habari zenu? Kunakipindi nilileta uzi huu, Ndugu zangu nashindwa kuwaelewa
Baada ya kuvuta jiko niliishi na mke wangu, mwezi wa 11/2021 tulibahatika kupata mtoto na mke wangu, sikuwa na hiyana niliona japo ndugu zangu walinikosea kiasi fulani acha niwataarifu japo mke wangu alipata PPH (Postpartum Haemorrhage) nusura afe niliwataarifu pia kuhusu hayo matatizo lakini hawakujali na wala mke wangu hakupigiwa simu wala kuulizwa chochote.
Baadae nilisema isiwe kesi acha niendelee kutulia kimya nikaamua kutokuwatafuta tena, pia japo nilifiwa na baba niliandika kwenye uzi hiyo link juu, baada ya kutoka msibani hakukuwa na mtu aliyekuja kunipa pole hasa mama yangu mdogo wala wajomba zangu hakuna na wala eti waulizie kuhusu mtoto wangu anaendeleaje hakuna.
Baada ya kuona hivyo nilitulia tulii, juzi kati mamdogo wangu ananipigia na kunilazimisha nimpeleke mke wangu na mtoto wangu kwake, pia naambiwa mtoto wa mjomba anafunga ndoa mwaka huu hivyo nijiandae kirohoni nikajisemea hivi hawa wananichukuliaje?
Nimepata msiba hawajaja na baadhi yao hajanipigia simu kunipa pole, haya mke wangu alijifungua na akapata matatizo na niliwataarifu hakuna aliye toa pole na wala kujali.
Nawasilisha wakuu, hiyo ni sahihi?
Pia kuna mambo mengi tu sema siwezi andika Wakuu
Baada ya kuvuta jiko niliishi na mke wangu, mwezi wa 11/2021 tulibahatika kupata mtoto na mke wangu, sikuwa na hiyana niliona japo ndugu zangu walinikosea kiasi fulani acha niwataarifu japo mke wangu alipata PPH (Postpartum Haemorrhage) nusura afe niliwataarifu pia kuhusu hayo matatizo lakini hawakujali na wala mke wangu hakupigiwa simu wala kuulizwa chochote.
Baadae nilisema isiwe kesi acha niendelee kutulia kimya nikaamua kutokuwatafuta tena, pia japo nilifiwa na baba niliandika kwenye uzi hiyo link juu, baada ya kutoka msibani hakukuwa na mtu aliyekuja kunipa pole hasa mama yangu mdogo wala wajomba zangu hakuna na wala eti waulizie kuhusu mtoto wangu anaendeleaje hakuna.
Baada ya kuona hivyo nilitulia tulii, juzi kati mamdogo wangu ananipigia na kunilazimisha nimpeleke mke wangu na mtoto wangu kwake, pia naambiwa mtoto wa mjomba anafunga ndoa mwaka huu hivyo nijiandae kirohoni nikajisemea hivi hawa wananichukuliaje?
Nimepata msiba hawajaja na baadhi yao hajanipigia simu kunipa pole, haya mke wangu alijifungua na akapata matatizo na niliwataarifu hakuna aliye toa pole na wala kujali.
Nawasilisha wakuu, hiyo ni sahihi?
Pia kuna mambo mengi tu sema siwezi andika Wakuu