Nimepata kazi kwenye NGO, nianze na kipi?

Mwana Ukoo

JF-Expert Member
Nov 21, 2016
252
422
Wakuu nimepata kazi katika NGO fulani ambayo Roughly nitakunja kama 1m hivi take home niko around 20s age. Sitegemewi na familia maana bado wana kazi, nilisoma uzi fulani wa kijana mwenzangu ambaye alipata kazi katika umri mdogo tu na kujikuta anatumbukia kwenye starehe sitaki kufanya makosa

Wakuu nipe ushauri nifanye nini katika miaka mitano ambapo plan zangu ni kuacha kazi baada ya miaka kumi, makaka, Mababa, baba na mama nishaurini Nianzie wapi mdogo wenu sina ushamba kiivo na starehe nina exposure kimtindo

Mlionitangulia nahitaji kujifunza kupitia nyinyi
 
Haya ndo madhara makubwa aliyoyafanya meko vijana wadogo tayari washachanganyikiwa, na kutokana na kukosa kazi vijana wanakuwa na msongo wa mawazo, kijana tafuta kazi yoyote ile hata kubeba mizigo Kariakoo pale.

Achana na hizi ndoto zako za JF.
 
Wakuu nimepata kazi katika NGO fulani ambayo Roughly nitakunja kama 1m hivi take home niko around 20s age. Sitegemewi na familia maana bado wana kazi, nilisoma uzi fulani wa kijana mwenzangu ambaye alipata kazi katika umri mdogo tu na kujikuta anatumbukia kwenye starehe sitaki kufanya makosa

Wakuu nipe ushauri nifanye nini katika miaka mitano ambapo plan zangu ni kuacha kazi baada ya miaka kumi, makaka, Mababa, baba na mama nishaurini Nianzie wapi mdogo wenu sina ushamba kiivo na starehe nina exposure kimtindo

Mlionitangulia nahitaji kujifunza kupitia nyinyi
Haya ndo madhara makubwa aliyoyafanya meko vijana wadogo tayari washachanganyikiwa, na kutokana na kukosa kazi vijana wanakuwa na msongo wa mawazo, kijana tafuta kazi yoyote ile hata kubeba mizigo kariakoo pale.

Achana na hizi ndoto zako za JF.
What's going on....
 
Haya ndo madhara makubwa aliyoyafanya meko vijana wadogo tayari washachanganyikiwa, na kutokana na kukosa kazi vijana wanakuwa na msongo wa mawazo, kijana tafuta kazi yoyote ile hata kubeba mizigo kariakoo pale.

Achana na hizi ndoto zako za JF.
Hahahahhahaha
 
Wakuu nimepata kazi katika NGO fulani ambayo Roughly nitakunja kama 1m hivi take home niko around 20s age. Sitegemewi na familia maana bado wana kazi, nilisoma uzi fulani wa kijana mwenzangu ambaye alipata kazi katika umri mdogo tu na kujikuta anatumbukia kwenye starehe sitaki kufanya makosa

Wakuu nipe ushauri nifanye nini katika miaka mitano ambapo plan zangu ni kuacha kazi baada ya miaka kumi, makaka, Mababa, baba na mama nishaurini Nianzie wapi mdogo wenu sina ushamba kiivo na starehe nina exposure kimtindo

Mlionitangulia nahitaji kujifunza kupitia nyinyi
Kama nimekuelewa, basi nikushauri kwanza utafute eneo ndani ya mkoa ambao unatamani kuja kuishi na kisha nunua kiwanja.
Baada ya hapo tunza pesa bank hadi uone umefikisha kiasi ambacho walau kitakutosha kuanzisha ujenzi wa nyumba ya kisasa, na baada ya hapo kama Mungu akikujaalia ukafanikiwa kumaliza ujenzi usikimbilie kuoa, kwanza angalia biashara unayo weza ukafanya na ikakuingizia kipato cha ziada.

Mwisho kabisa nakushauri kama utakua bado unayo ajira, tafuta usafiri wako mzuri kwasababu kwa maisha ya leo kumiliki gari ni moja ya hitaji la msingi ili kurahisisha usarifi wa wewe kwenda na ratiba zako daily.

Kwasasa, jitahidi kua mwenye nidhamu ya kazi na pia heshimu kila mtu unaefanya nae kazi (hata kama ni cleaner). Hakikisha unaongeza bidii kwenye kazi na ingia kazini kwa wakati na ikiwezekana jaribu kuwahi kufika walau dakika 5-10 kabla ya mudawa kazi kuanza.
Usiwe mbishi pindi unapo agizwa na mkubwa wako wa kazi (hata kama amekutuma kitu cha kijinga kabisa), na usipende kunung'unika ama kutanguliza kuomba malipo ya ziada ikiwa umehitajika kufanya kazi hata kwa muda wa ziada.

Ukiyazingatia hayo, hakika utafika mbali na Nakuombea kheri na fanaka, na Mungu akujaalie ufanikiwe katika malengo na mipago yako.
 
Kama nimekuelewa, basi nikushauri kwanza utafute eneo ndani ta mkoa ambao unatamani kuja kuishi na kisha nunua kiwanja.
Baada ya hapo tunza pesa bank hadi uone umefikisha kiasi ambacho walau kitakutosha kuanzisha ujenzi wa nyumba y kisasa, na baada ya hapo kama Mungu akikujaalia ukafanikiwa kumaliza ujenzi usikimbilie kuoa, kwanza angalia biashara unayo weza ukafanya na ikakuingizia kipato cha ziada.

Mwisho kabisa nakushauri kama utakua bado unayo ajira, tafuta usafiri wako mzuri kwasababu kwa maisha ya leo kumiliki gari ni moja ya hitaji la msingi ili kurahisisha usarifi wa wewe kwenda na ratiba zako daily.

Nakuombea kheri na fanaka, na Mungu akujaalie ufanikiwe katika malengo na mipngo yako.
Mkuu nashukuru sana kwa ushauri huu
 
Wakuu nimepata kazi katika NGO fulani ambayo Roughly nitakunja kama 1m hivi take home niko around 20s age. Sitegemewi na familia maana bado wana kazi, nilisoma uzi fulani wa kijana mwenzangu ambaye alipata kazi katika umri mdogo tu na kujikuta anatumbukia kwenye starehe sitaki kufanya makosa

Wakuu nipe ushauri nifanye nini katika miaka mitano ambapo plan zangu ni kuacha kazi baada ya miaka kumi, makaka, Mababa, baba na mama nishaurini Nianzie wapi mdogo wenu sina ushamba kiivo na starehe nina exposure kimtindo

Mlionitangulia nahitaji kujifunza kupitia nyinyi
Mihemko ikipungua njoo uulize tena hilo swali, kula bata kwanza miezi 2-3 ya mwanzo then ndo utajua kama hiyo pesa itatosha kwenye milango yako mingine
 
Haya ndo madhara makubwa aliyoyafanya meko vijana wadogo tayari washachanganyikiwa, na kutokana na kukosa kazi vijana wanakuwa na msongo wa mawazo, kijana tafuta kazi yoyote ile hata kubeba mizigo Kariakoo pale.

Achana na hizi ndoto zako za JF.
Huo ni zaidi ya msongo wa mawazo, kijana kabla hata hajaanza kazi tayari amesha kuwa na plan ya kuacha kazi!!
Matokeo ya juhudi za kimaisha ya mwanadamu hupatikana usiku wa siku husika. Muda wa miaka kumi ya utafutaji wa mwandamu kimaisha kama itakuwa kinyume na matarajio itakuwa sawa na wiki mbili za umri wa mtoto aliyetoka kuzaliwa... Anajua kunyonya na kulia tu... Sad.
 
Wakuu nimepata kazi katika NGO fulani ambayo Roughly nitakunja kama 1m hivi take home niko around 20s age. Sitegemewi na familia maana bado wana kazi, nilisoma uzi fulani wa kijana mwenzangu ambaye alipata kazi katika umri mdogo tu na kujikuta anatumbukia kwenye starehe sitaki kufanya makosa

Wakuu nipe ushauri nifanye nini katika miaka mitano ambapo plan zangu ni kuacha kazi baada ya miaka kumi, makaka, Mababa, baba na mama nishaurini Nianzie wapi mdogo wenu sina ushamba kiivo na starehe nina exposure kimtindo

Mlionitangulia nahitaji kujifunza kupitia nyinyi
1. Kaa mbali na mademu. Usikimbilie kuoa.

2. Hakikisha unawekeza kwenye KU SAVE PESA.

3. Kaa mbali na mikopo ya benki kwa sasa.

4. Nunua kiwanja kwa kutumia savings zako.

5. Jiweke karibu na Mungu.

6. Usiwe na papara, sio kila iphone ikitoka unataka uwe nayo.

7. Anza kujiuliza "nikifukuzwa kazi nitafanya nn?" ...namaanisha anza kutafuta plan B.

8. Kuwa kauzu. Sio kila ndugu akiomba pesa uwe unatoa tu (ukizembea hapa jiandae kusaga meno badae). NAMAANISHA SAIDIA KWA KIASI.

Nimemaliza kwa sasa.
 
Wakuu nimepata kazi katika NGO fulani ambayo Roughly nitakunja kama 1m hivi take home niko around 20s age. Sitegemewi na familia maana bado wana kazi, nilisoma uzi fulani wa kijana mwenzangu ambaye alipata kazi katika umri mdogo tu na kujikuta anatumbukia kwenye starehe sitaki kufanya makosa

Wakuu nipe ushauri nifanye nini katika miaka mitano ambapo plan zangu ni kuacha kazi baada ya miaka kumi, makaka, Mababa, baba na mama nishaurini Nianzie wapi mdogo wenu sina ushamba kiivo na starehe nina exposure kimtindo

Mlionitangulia nahitaji kujifunza kupitia nyinyi
Mshahara wako wa kwanza ulete niufanyie matambiko pesa mwanakharamu mipango sio matumizi
 
Back
Top Bottom