#COVID19 Nimepata Chanjo ya Corona nchini Marekani, puuzeni uzushi

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,550
8,643
Nimefanikiwa kupata chanjo ya Corona hapa napoishi na kufanya kazi Dallas, Texas. Nimepata dose mbili za sindano kwenye bega ya kwanza tarehe 5 mwezi wa pili na ya pili tarehe 4 mwezi wa tatu. Nimepata chanjo kutoka kampuni ya Moderna. Nilivimba kidogo kwenye bega kwa mara zote lakini sijapata homa kama watu wengine wanapata homa kwenye sindano ya pili.

Chanjo ni muhimu na zinaokoa maisha hasa kwa wale wenye au ambao waliwahi kuwa na pumu, kisukari, wazee, wenye magojwa ya moyo na wamegundua pia wenye type A ya damu nao wanaumwa sana wakipata corona. Asilimia 90% ya watu wakipata hawazidiwi hivyo inawezekana hata wewe umeshapata Corona bila kujua. Lakini baada ya siku 90 unaweza kupata tena na inaweza kuwa mbaya zaidi maana mwili unakuwa hauna nguvu sana. Kwasababu kirusi cha corona kimekaa zaidi ya mwaka kinabadilika ili kiweze kuingia kirahisi kwenye miili yetu hii kitaalamu wanaita variant. Hivyo mpaka sasa kuna variant ya South Africa, England, Brazil na ili ya China. Ya South Africa ndiyo kali kuliko zote na ndiyo imeingia Tanzania kwa sasa na kusababisha watu kufa na kuumwa sana kulinganisha na ile ya mwanzo.

Kwenye kinga kuna kinga nyingi sana cha maana ni upatikanaji, usalama na chanjo kufanya kazi. Kuna vipimo vikubwa viwili vya kuzingatia cha kwanza ni kinga ya chanjo yaani ambayo inazuia mtu kupata Corona lakini cha pili je mtu akipata corona ambaye ana chanjo ataumwa kiasi cha kulazwa au kuzidiwa?. Hii ya south Africa inaonyesha kinga haifanyi kazi vizuri hasa kwa hii chanjo ambayo nchi za Africa inauziwa za Oxford Astrazenica au AZD1222. Hawajatoa data kuonyesha je mtu akiumwa inakuwaje au kinga inakuwaje. Lakini chanjo ya Johnson and Johnson imeonyesha inakinga ya corona ya south Africa kwa asilimia 57% lakini hata ukipata corona ni karibu 100% hautazidiwa. Lakini mpaka sasa HAKUNA MTU ALIYEPATA CHANJO YEYOTE POPOTE NA KUUMWA NA KUZIDIWA KIASI CHA KULAZWA. Hii ina maana gani ni kwamba inawezekana kinga ikawa ndogo lakini watu nhawatapoteza maisha ambao wana chanjo

Tanzania wanaogopa chanjo kama hii niliyopewa kwasababu inatumia technologia ya mRNA ambayo ni ya DNA na wanaogopa eti DNA zetu wazungu watabadilisha. Wakati nimeenda kupata chanjo kulikuwa na wazungu wengi wamepewa chanjo kama yangu sasa sijui hizi habari ni za wapi?!!!. Lakini kuna chanjo ambazo zina technologia kama chanjo za zamani mfano Sputnik V ambayo ni ya Urusi inatumia technologia ya zamani ya chanjo na sasa wamefanya utafiti unaonyesha inakinga aslimia 90%. Lakini hii ina order nyingi hasa huko South America itachukua muda kuipata.

Hivyo ushauri wangu ni kwa serikali kutumia chanjo yeyote kasoro ile ya China ambayo haina data ambazo watu wamezionana kusema zipo sawa. Lakini hii wenzetu wa Kenya, Nigeria, Ghana wamepata chanjo yenyewe inawezekana kinga ni ndogo kwa hii ya south Africa lakini ukipata chanjo corona itakuwa kama mafua ya kawaida haitakuuwa kama sasa hivi. Hivyo nashauri bado ni bora sana kuliko kukaa na kutokufanya maamuzi yeyote. Tukiweza kuweka order hii ya J&J ni zuri kwasababu ni sindano mmoja na inahitaji jokofu la kawaidia kuifadhi.

Tatizo serikali inaweza kusema wataalamu wanachukungaza lakini mpaka sasa hakuna habari yeyote uchunguzi umefika wapi, nani yupo kwenye hiyo team inawezekana ni maneno tu.
 
Nimefanikiwa kupata chanjo ya Corona hapa napoishi na kufanya kazi Dallas, Texas. Nimepata dose mbili za sindano kwenye bega ya kwanza tarehe 5 mwezi wa pili na ya pili tarehe 4 mwezi wa tatu. Nimepata chanjo kutoka kampuni ya Moderna. Nilivimba kidogo kwenye bega kwa mara zote lakini sijapata homa kama watu wengine wanapata homa kwenye sindano ya pili.

Chanjo ni muhimu na zinaokoa maisha hasa kwa wale wenye au ambao waliwahi kuwa na pumu, kisukari, wazee, wenye magojwa ya moyo na wamegundua pia wenye type A ya damu nao wanaumwa sana wakipata corona. Asilimia 90% ya watu wakipata hawazidiwi hivyo inawezekana hata wewe umeshapata Corona bila kujua. Lakini baada ya siku 90 unaweza kupata tena na inaweza kuwa mbaya zaidi maana mwili unakuwa hauna nguvu sana. Kwasababu kirusi cha corona kimekaa zaidi ya mwaka kinabadilika ili kiweze kuingia kirahisi kwenye miili yetu hii kitaalamu wanaita variant. Hivyo mpaka sasa kuna variant ya South Africa, England, Brazil na ili ya China. Ya South Africa ndiyo kali kuliko zote na ndiyo imeingia Tanzania kwa sasa na kusababisha watu kufa na kuumwa sana kulinganisha na ile ya mwanzo.

Kwenye kinga kuna kinga nyingi sana cha maana ni upatikanaji, usalama na chanjo kufanya kazi. Kuna vipimo vikubwa viwili vya kuzingatia cha kwanza ni kinga ya chanjo yaani ambayo inazuia mtu kupata Corona lakini cha pili je mtu akipata corona ambaye ana chanjo ataumwa kiasi cha kulazwa au kuzidiwa?. Hii ya south Africa inaonyesha kinga haifanyi kazi vizuri hasa kwa hii chanjo ambayo nchi za Africa inauziwa za Oxford Astrazenica au AZD1222. Hawajatoa data kuonyesha je mtu akiumwa inakuwaje au kinga inakuwaje. Lakini chanjo ya Johnson and Johnson imeonyesha inakinga ya corona ya south Africa kwa asilimia 57% lakini hata ukipata corona ni karibu 100% hautazidiwa. Lakini mpaka sasa HAKUNA MTU ALIYEPATA CHANJO YEYOTE POPOTE NA KUUMWA NA KUZIDIWA KIASI CHA KULAZWA. Hii ina maana gani ni kwamba inawezekana kinga ikawa ndogo lakini watu nhawatapoteza maisha ambao wana chanjo

Tanzania wanaogopa chanjo kama hii niliyopewa kwasababu inatumia technologia ya mRNA ambayo ni ya DNA na wanaogopa eti DNA zetu wazungu watabadilisha. Wakati nimeenda kupata chanjo kulikuwa na wazungu wengi wamepewa chanjo kama yangu sasa sijui hizi habari ni za wapi?!!!. Lakini kuna chanjo ambazo zina technologia kama chanjo za zamani mfano Sputnik V ambayo ni ya Urusi inatumia technologia ya zamani ya chanjo na sasa wamefanya utafiti unaonyesha inakinga aslimia 90%. Lakini hii ina order nyingi hasa huko South America itachukua muda kuipata.

Hivyo ushauri wangu ni kwa serikali kutumia chanjo yeyote kasoro ile ya China ambayo haina data ambazo watu wamezionana kusema zipo sawa. Lakini hii wenzetu wa Kenya, Nigeria, Ghana wamepata chanjo yenyewe inawezekana kinga ni ndogo kwa hii ya south Africa lakini ukipata chanjo corona itakuwa kama mafua ya kawaida haitakuuwa kama sasa hivi. Hivyo nashauri bado ni bora sana kuliko kukaa na kutokufanya maamuzi yeyote. Tukiweza kuweka order hii ya J&J ni zuri kwasababu ni sindano mmoja na inahitaji jokofu la kawaidia kuifadhi.

Tatizo serikali inaweza kusema wataalamu wanachukungaza lakini mpaka sasa hakuna habari yeyote uchunguzi umefika wapi, nani yupo kwenye hiyo team inawezekana ni maneno tu.
Same here. Nimechanja ya kwanza ya Pfizer, baada ya wiki tatu nitachanja ya pili. USA.

Sikuumwa kichwa wala kupata homa.

Watanzania wengi waliopo Tanzania wanajazwa ujinga na serikali inayohoji chanjo kwa sababu za kisiasa.

Serikali ingesema tu haina hela za kuwapa wananchi chanjo, watu wangeisaidia.

Ajabu ni kuona watu wanaogopa chanjo halafu wengine wanavaa mpaka chupi za mtumba hawajui zimepakwa nini!

Dawa wanazotumia hawatengenezi wao, maji yanasafishwa na kemikali za ku import, karibu kila kitu tuna import. Na uwezo wetu wa kuhakiki viwango ni mdogo sana.

Halafu mtu anashikia bango chanjo!
 
Same here. Nimechanja ya kwanza ya Pfizer, baada ya wiki tatu nitachanja ya pili. USA.

Sikuumwa kichwa wala kupata homa.

Watanzania wengi waliopo Tanzania wanajazwa ujinga na serikali inayohoji chanjo kwa sababu za kisiasa.

Serikali ingesema tu haina hela za kuwapa wananchi chanjo, watu wangeisaidia.

Ajabu ni kuona watu wanaogopa chanjo halafu wengine wanavaa mpaka chupi za mtumba hawajui zimepakwa nini!

Dawa wanazotumia hawatengenezi wao, maji yanasafishwa na kemikali za ku import, karibu kila kitu tuna import. Na uwezo wetu wa kuhakiki viwango ni mdogo sana.

Halafu mtu anashikia bango chanjo!


Mie natamani sana hao wanaokataa chanjo waugue....huu ugonjwa mie naweza kesha siku nzima nikihadithia jinsi unavyotesa... unanyong'onyeza mno kwa muda mrefu nowonder wazee inawaonda mapema sana..ni mateso makali sana
 
Mie natamani sana hao wanaokataa chanjo waugue....huu ugonjwa mie naweza kesha siku nzima nikihadithia jinsi unavyotesa... unanyong'onyeza mno kwa muda mrefu nowonder wazee inawaonda mapema sana..ni mateso makali sana
Kwani lazima kila mtu achanjwe?! Hata chanjo ikiletwa si lazima kila mtu achanjwe. Ukijisikia kuchanjwa sawa,asietaka sawa.
Dawa au chanjo isio ya lazima siitaki mwilini mwangu.
 
Haya Kiranga na wengine mlio huko majuu mtatusaidiaje na sisi tupate anagalau hiyo mnasema unachomwa sindano moja tu[ j&J]? Huku hali tete, Jiwe anasema yeye anaamini BUBIJI itatuponya na wapambe wake wakina Msukuma ndio hao wanajenga NYUNGU vijijini kwao!!!
 
Kwani lazima kila mtu achanjwe?! Hata chanjo ikiletwa si lazima kila mtu achanjwe. Ukijisikia kuchanjwa sawa,asietaka sawa.
Dawa au chanjo isio ya lazima siitaki mwilini mwangu.
Anahoji kwanini serikali haitaki chanjo huku watu wanapoteza maisha.

Ulivyo na Ego mbaya huoni tunavyopoteza maprof, padres, doctors, lawyers etc kwa mijitu mibinafsi kama nyie.

Black is misfortune, I can agree.
 
Anahoji kwanini serikali haitaki chanjo huku watu wanapoteza maisha.

Ulivyo na Ego mbaya huoni tunavyopoteza maprof, padres, doctors, lawyers etc kwa mijitu mibinafsi kama nyie.

Black is misfortune, I can agree.
Ego my foot, unanipangia? Sio kila mtu atafanya unavyopenda wewe. Subiri serikali wakujibu kwanini hawaleti ila hata wakileta kama ni hiari sichanji.
 
Haya Kiranga na wengine mlio huko majuu mtatusaidiaje na sisi tupate anagalau hiyo mnasema unachomwa sindano moja tu[ j&J]? Huku hali tete, Jiwe anasema yeye anaamini BUBIJI itatuponya na wapambe wake wakina Msukuma ndio hao wanajenga NYUNGU vijijini kwao!!!
Wewe naona sasa unataka kutupa kesi za uhujumu uchumi na habari za kupimwa mkojo na mkemia mkuu.
 
Kwani lazima kila mtu achanjwe?! Hata chanjo ikiletwa si lazima kila mtu achanjwe. Ukijisikia kuchanjwa sawa,asietaka sawa.
Dawa au chanjo isio ya lazima siitaki mwilini mwangu.
Chanjo sehemu nyingi duniani siyo lazima. Ila baada ya muda itakuja kukulazimu (kumbuka siyo lazima) kuchanjwa. Nahisi kwa watu wanaosafiri nje ya nchi/kwenda kwenye shughuli maalum wanaweza kukwama kama hawajachanjwa. Chukulia mfano wa Hija. Pia pengine kuna nchi zitataka uwe na cheti cha chanjo kabla hujaingia kwenye hizo nchi, kama ilivyo yellow fever. Siyo lazima, lakini unalazimika.
 
Hii
IMG-20210308-WA0003.jpg
 
Tulia dawa ikuingieeee hata miezi suta bado unabwabwaja we umeshachoma instosha sie tuacheee
 
57 Reactions
Reply
Back
Top Bottom