Nimepanga kwenda kuishi Msituni/Porini sana

Hizo ni stress za kukutana na uliopiga nao kitabu mjini wapo levo nyingine. Sasa hiyo kitaalamu inaitwa kujicoumoflage kwa kukaa na nyani ambao hawatakuuliza “Sasa hivi upo wapi” kila ukipishana nao
😀😁😂🤣
 
Mimi nami nina mpango wa kuhamia porini,kijijini.

Mnapajua Chato?Kila siku watu walikuwa hawaishi kupaponda kwasababu jiwe alisababisha wapaponde.

Basi bwana,kule kuna maeneo poa sana na soon ninahamia kule.Kwanza 90% ya Chato imezungukwa na Ziwa Victoria, na mimi nimejenga nyumba yangu kule kandokando ya ziwa Victoria.Kuna misitu mizuri,hewa safi na ardhi nzuri kwa kilimo.

Nyumba yangu haiko mbali sana na hifadhi nzuri za Rubondo na Burigi/Biharamulo kwa namna fulani. I love nature vibaya mno.

Mwendazake keshaenda sasa tuzungumzie positively fursa zilizoko huku.
 
Kila mtu katika maisha kuna kitu anapenda, kila mtu ana tafsiri yake ya maisha na jinsi ya kuyafurahia maisha. Toka nimerudi kutoka South Afrika Kama kuna kitu natamani kufanya kwenye maisha yangu hapa Bongo na kitanipa furaha ya kweli, basi ni kwenda kujenga na kuishi Msituni,nilijikuta napenda kuishi kwenye misitu ya Iringa, Njombe au Mbeya.

Miaka 3 toka nimerudi nilianza maandalizi ya kulifikia hili, nilishanunua Shamba Kijiji Kimoja huko Njombe la Ekari 20, Nilichofurahi katikati ya hili shamba kuna bwawa kubwa la Maji. Niliona pia Africa Kusini wazungu wengi wamejenga mbali kabisa nje ya Miji. Mm nakwenda Msituni kabisa.

Halafu Msituni kuna utulivu wa aina yake. Napenda kile Kijaniii. Nimeshapanda mazao mbalimbali ya kudumu. Mwaka huu nimeanza kufuga pia. Nilinunua Water Pump na nilishajenga vyumba vyangu viwili. Shamba zima nimezungushia Miti ya Milingoti kama uzio wa shamba langu. Katikati nimepanda Parachichi na Apples nyinyi. Ukweli mazingira yanavutia sana. Kwenye Bwawa nimeanza kufuga Samaki. Pia nina Mizinga ya Nyuki 20 tayari.

Ukweli mjini nimeona mambo ni mengi sana, hakuna utulivu kabisa, presha ya maisha ni kubwa mno. Kila kona ni siasa tu, nimechoka siasa za nchi hii, Kila Kijana Mjini mwanasiasa. kwenye mitandao utakutana na maisha tu ya Mastaa na vituko vyao.

Maisha yangu ya Porini nimepanga kufanya Kilimo na Ufugaji tu, Siku moja moja nitatafuta Kanya au Tshepiso wangu wa Kijijini nakujitafunia. Sitaki Siasa wala negativity ya aina yoyote. Ndoto zangu za Baadae ni kujenga nyumba kubwa Shambani, Kununua Trekta na Mashine nyengine. Siku za Baadae kama nitamiss kuona Mkusanyiko wa watu wengi na Maghorofa basi nitarudi Mjini, nitakwenda moja kwa moja mpaka Airport.

Nitapanda ndege mpaka Ulaya, Marekani, au Asia Nitapumziko huko miezi na miezi halafu nikitosheka narudi porini kwangu Njombe. Mwakani naanza kuvuna Parachichi zangu na Apples. Karibuni sana. Nitajitahidi kuwa narudi hapa Jukwaani kuwapa Mrejesho wa maisha ya porini, faida na changamoto zake.
Kila la kheri mkuu ..
 
Mzazi maisha ya wazungu Kuishi porini yasikudanganye nakwambia wale hata wakipatwa na tatizo chopa hii hapa .sasa wewe nenda ukaishi porini uone show ilivyo ya kibabe unaweza kujikuta unaingia himaya ya wachawi
Mapori yetu sio rafiki kabisa,nakushauri nenda ukaishi kijijini na sio porini
 
moja ya changamoto kubwa sana ya kujitenga na kuishi peke yako mbali na jamii ni usalama (vyote mali na wewe) nilitaka kutumia neno ukiingiliwa lakini ngoja nitumie ukivamiwa, hakuna msaada wa haraka. lazima ujipange sana kwenye hili na usilipuuze. Mguu wa kuku lazima uwe nao kiunoni 24/7.
 
Mwamba big up Mimi na wewe tupo sawa ki idea halafu Tena maeneo yale Yale aisee Njombe ni sehemu moja amaizing sana Kama unataka uishi maisha Kama hayo yaani unatengeneza bustani yako saaaaafi kabisaaa Kama paradiso flani hivi amaizing
Yaaaa I get you nigga, keep big up meeen You know!
(in Lemutuz voices)
😄😄😅😅😂
 
Haya maisha ninayatamani sana. Nunua wheel barrow hili litakusaidia kusafirishia vitu kati ya nyumbani na shambani. Hasa wakati wa mavuno.

Shoka unaihitaji kwa shughuli za kila siku. Kama utaweza kupata chainsaw kwa kukata miti ukipanua shamba hata miti ya ujenzi wa mabanda.

Kama una bwawa fuga na bata, kwenye bwawa mradi uwawekee sehemu za chakula na kutagia haya yanakua mabanda kwani mvua ikinyesha pumba zisinyeshewe.

Kama ukipata na grinder ndogo ya mahindi huhitaji vitu vingi.

Gari ni muhimu kwaajili ya kufuata mahitaji mjini mara moja kwa mwezi na kupelekea mazao sokoni.
Asisahau na solar power hata ya 200W inatosha sana.
 
Wako baadhi watakuona wa ajabu kuishi porini, hususani mkoa wa dar waliozoea kwenda sehemu za starehe, madisco, cinema, vilabu n.k.. hawa viumbe hata uwaambie nini hawatakuelewa.. ..hakuna life nzuri kama porini, especially napenda sana.. ..ukilala utasikia sauti za wanyama🦌🦌🦓🐃🐂🐄🐏🐸, ukiamka asubuhi utasikia sauti za ndege wa aina tofauti🦃🐔🐓🐣🐤🐦🕊🦅🦆🦢🦉🦜🐢.. ..raha sana 😃



🇦🇷🇦🇷🇦🇷🔥🔥
 
Kila mtu katika maisha kuna kitu anapenda, kila mtu ana tafsiri yake ya maisha na jinsi ya kuyafurahia maisha. Toka nimerudi kutoka South Afrika Kama kuna kitu natamani kufanya kwenye maisha yangu hapa Bongo na kitanipa furaha ya kweli, basi ni kwenda kujenga na kuishi Msituni,nilijikuta napenda kuishi kwenye misitu ya Iringa, Njombe au Mbeya.

Miaka 3 toka nimerudi nilianza maandalizi ya kulifikia hili, nilishanunua Shamba Kijiji Kimoja huko Njombe la Ekari 20, Nilichofurahi katikati ya hili shamba kuna bwawa kubwa la Maji. Niliona pia Africa Kusini wazungu wengi wamejenga mbali kabisa nje ya Miji. Mm nakwenda Msituni kabisa.

Halafu Msituni kuna utulivu wa aina yake. Napenda kile Kijaniii. Nimeshapanda mazao mbalimbali ya kudumu. Mwaka huu nimeanza kufuga pia. Nilinunua Water Pump na nilishajenga vyumba vyangu viwili. Shamba zima nimezungushia Miti ya Milingoti kama uzio wa shamba langu. Katikati nimepanda Parachichi na Apples nyinyi. Ukweli mazingira yanavutia sana. Kwenye Bwawa nimeanza kufuga Samaki. Pia nina Mizinga ya Nyuki 20 tayari.

Ukweli mjini nimeona mambo ni mengi sana, hakuna utulivu kabisa, presha ya maisha ni kubwa mno. Kila kona ni siasa tu, nimechoka siasa za nchi hii, Kila Kijana Mjini mwanasiasa. kwenye mitandao utakutana na maisha tu ya Mastaa na vituko vyao.

Maisha yangu ya Porini nimepanga kufanya Kilimo na Ufugaji tu, Siku moja moja nitatafuta Kanya au Tshepiso wangu wa Kijijini nakujitafunia. Sitaki Siasa wala negativity ya aina yoyote. Ndoto zangu za Baadae ni kujenga nyumba kubwa Shambani, Kununua Trekta na Mashine nyengine. Siku za Baadae kama nitamiss kuona Mkusanyiko wa watu wengi na Maghorofa basi nitarudi Mjini, nitakwenda moja kwa moja mpaka Airport.

Nitapanda ndege mpaka Ulaya, Marekani, au Asia Nitapumziko huko miezi na miezi halafu nikitosheka narudi porini kwangu Njombe. Mwakani naanza kuvuna Parachichi zangu na Apples. Karibuni sana. Nitajitahidi kuwa narudi hapa Jukwaani kuwapa Mrejesho wa maisha ya porini, faida na changamoto zake.
Mwenzio huyo hapo alishawahi huko msituni....
IMG_20210122_234023.jpg
 
Binafsi nafikiria kuhamia Rungwe, Lushoto au Mufindi ila sitokaa msituni napendelea kuishi eneo lililo pembezoni kidogo ya miji. Nilienda kufanya utafiti maeneo haya nimepapenda zaidi Brooke Bond - Mufindi na eneo jirani na Daraja la Mungu, KK - Rungwe. Ni maeneo yenye mandhari nzuri ya asilia.

Mfano mzuri ni kama Swiss farm cottage Lushoto.

unser-chalet-von-oben.jpg


it-was-good-to-be-here.jpg


our-farm.jpg


photo5jpg.jpg


a-view-from-the-top.jpg


photo2jpg.jpg


swiss-farm-cottage.jpg
 
Back
Top Bottom