Nimepanga kwenda kuishi Msituni/Porini sana

Hakuna raha kama kuishi hizo area....kuna kijiji kiko Moro vijijini unaweza dhani ni mbinguni..kijani throughout the year
2.kuna kijiji ninaenda sana hakuna suala la magari wala mikelele...yaan kumepoa..hakuna heka heka kbs sijui huyu apite na gari utamani hakuna...yaan maisha rahisiii...unaingia ziwani unaomba samaki unaenda pika unalala unaamka fresh kbs..i like that too!.all the best!
Mimi napenda mlimani
 
Kila mtu katika maisha kuna kitu anapenda, kila mtu ana tafsiri yake ya maisha na jinsi ya kuyafurahia maisha. Toka nimerudi kutoka South Afrika Kama kuna kitu natamani kufanya kwenye maisha yangu hapa Bongo na kitanipa furaha ya kweli, basi ni kwenda kujenga na kuishi Msituni,nilijikuta napenda kuishi kwenye misitu ya Iringa, Njombe au Mbeya.

Miaka 3 toka nimerudi nilianza maandalizi ya kulifikia hili, nilishanunua Shamba Kijiji Kimoja huko Njombe la Ekari 20, Nilichofurahi katikati ya hili shamba kuna bwawa kubwa la Maji. Niliona pia Africa Kusini wazungu wengi wamejenga mbali kabisa nje ya Miji. Mm nakwenda Msituni kabisa.

Halafu Msituni kuna utulivu wa aina yake. Napenda kile Kijaniii. Nimeshapanda mazao mbalimbali ya kudumu. Mwaka huu nimeanza kufuga pia. Nilinunua Water Pump na nilishajenga vyumba vyangu viwili. Shamba zima nimezungushia Miti ya Milingoti kama uzio wa shamba langu. Katikati nimepanda Parachichi na Apples nyinyi. Ukweli mazingira yanavutia sana. Kwenye Bwawa nimeanza kufuga Samaki. Pia nina Mizinga ya Nyuki 20 tayari.

Ukweli mjini nimeona mambo ni mengi sana, hakuna utulivu kabisa, presha ya maisha ni kubwa mno. Kila kona ni siasa tu, nimechoka siasa za nchi hii, Kila Kijana Mjini mwanasiasa. kwenye mitandao utakutana na maisha tu ya Mastaa na vituko vyao.

Maisha yangu ya Porini nimepanga kufanya Kilimo na Ufugaji tu, Siku moja moja nitatafuta Kanya au Tshepiso wangu wa Kijijini nakujitafunia. Sitaki Siasa wala negativity ya aina yoyote. Ndoto zangu za Baadae ni kujenga nyumba kubwa Shambani, Kununua Trekta na Mashine nyengine. Siku za Baadae kama nitamiss kuona Mkusanyiko wa watu wengi na Maghorofa basi nitarudi Mjini, nitakwenda moja kwa moja mpaka Airport.

Nitapanda ndege mpaka Ulaya, Marekani, au Asia Nitapumziko huko miezi na miezi halafu nikitosheka narudi porini kwangu Njombe. Mwakani naanza kuvuna Parachichi zangu na Apples. Karibuni sana. Nitajitahidi kuwa narudi hapa Jukwaani kuwapa Mrejesho wa maisha ya porini, faida na changamoto zake.

View attachment 1775171
Njombe kijiji gani?
 
Hayo ndio maisha ya ukweli mzee, unaambiwa kiishia katika miji ambayo tayari imesha jenga na kuendelezwa basi unaishi katika mipangi ya wengine , lakini kwa style yako mzee ulimwengu ni wako a utafurahia uumbali wa mungu ki halisia kabisa
 
42 Reactions
Reply
Back
Top Bottom