Nimeonana na Mzee Pascally Mayenga,nikampa moyo,tukafurahi.

matongo manawa

JF-Expert Member
Apr 6, 2011
336
79
Kama kunamwandishi aliyeandika makala nyingi za kumshauri Rais Kikwete ni mzee Mayenga,
Nikwasababu hiyo nilipomwona moyo wangu ukanipigia yowe ukisema nenda hata msalimie mzalendo huyu.
Nami nilitii bila kinyongo nilijongea alipokaa eneo la Break point nilimpa heshima yake nikamwambia "
mzee tunashukuru kwa makala kwa kweli tunapata chakula cha kutosha naye akajibu kwa tabasamu pana asnte tunashukuru kwa kutuunga mkono"

Haraka haraka nilichukua gazeti la Tanzania daima,na wiki hii kaandika"Rais wangu Kikwete:Nchi yangu kwanza
iwe salaam ya kitaifa"

Uandishi wake ni ule unaozingatia itifaki ya heshima,lkn kinachonishangaza pamoja na ushauri wake murua kwa
mpendwa raisi hajawahi kusikilizwa ushauri wake,mzee huyu amekuwa akifanya kazi Kama ya kutwanga maji kwenye
kinu.

Je ni lini serikali sikivu ya kinadharia itakuwa sikivu kwa vitendo ili isikie ushauri huu?

Mzee Mayenga songa mbele mbegu unayopanda haipotei bure
kama si leo itaota kesho.

Mungu akufungilie zaidi.
 
Kama kunamwandishi aliyeandika makala nyingi za kumshauri Rais Kikwete ni mzee Mayenga,
Nikwasababu hiyo nilipomwona moyo wangu ukanipigia yowe ukisema nenda hata msalimie mzalendo huyu.
Nami nilitii bila kinyongo nilijongea alipokaa eneo la Break point nilimpa heshima yake nikamwambia "
mzee tunashukuru kwa makala kwa kweli tunapata chakula cha kutosha naye akajibu kwa tabasamu pana asnte tunashukuru kwa kutuunga mkono"

Haraka haraka nilichukua gazeti la Tanzania daima,na wiki hii kaandika"Rais wangu Kikwete:Nchi yangu kwanza
iwe salaam ya kitaifa"

Uandishi wake ni ule unaozingatia itifaki ya heshima,lkn kinachonishangaza pamoja na ushauri wake murua kwa
mpendwa raisi hajawahi kusikilizwa ushauri wake,mzee huyu amekuwa akifanya kazi Kama ya kutwanga maji kwenye
kinu.

Je ni lini serikali sikivu ya kinadharia itakuwa sikivu kwa vitendo ili isikie ushauri huu?

Mzee Mayenga songa mbele mbegu unayopanda haipotei bure
kama si leo itaota kesho.

Mungu akufungilie zaidi.
Ila ana nikeraga anapomsifu Lowasa!
 
Ila ana nikeraga anapomsifu Lowasa!

Huo ni mtazamo wake... Kwake yeye Lowassa anafaa kwako hafai. Mzee Mayega hunifanya nisubiri Jumatano kwa hamu kubwa sana. Yeye sio mnafiki anasema kweli, tena kweli tupu. Historia itamkumbuka sana Mzee huyu. Nawashauri pia tafuteni kitabu chake Mwalimu Mkuu wa Watu
 
huo ni mtazamo wake... Kwake yeye lowassa anafaa kwako hafai. Mzee mayega hunifanya nisubiri jumatano kwa hamu kubwa sana. Yeye sio mnafiki anasema kweli, tena kweli tupu. Historia itamkumbuka sana mzee huyu. Nawashauri pia tafuteni kitabu chake mwalimu mkuu wa watu
kila mtu ana mapungufu hata mm namsoma sana huyu mzee lakini kumsifia marakwa mara lowasa mh!
 
  • Thanks
Reactions: SG8
Anze kumshauri Liwalo na Liwe....maana huyo mwingine ni pasua..
 
kibanda kashariharibu gazeti hilo..guess mauzo yake yatapungua sana,..ansbert gurumo apewe nafasi ya mchumia tumbo kibanda..
 
Mayega rafiki yake Lowassa,labda na yeye hawajakutana barabarani tutajuaje?Kibanda naye wiki mbili anamtetea Kinana kuwa ni kamanda!Yote maoni tu maana kila mtu na vionjo vyake,lakini ukitumia mas media kumsifia mtu ukaacha kuuchambua mfumo mzima unakuwa kama na fikra ziisizokuwa pana vile?
 
Huyu mzee humsifia Lowassa kwa yale mazuri aliyofanya akilinganisha na huyu asiye fisadi mtoto wa mkulima!
 
Kama kunamwandishi aliyeandika makala nyingi za kumshauri Rais Kikwete ni mzee Mayenga,
Nikwasababu hiyo nilipomwona moyo wangu ukanipigia yowe ukisema nenda hata msalimie mzalendo huyu.
Nami nilitii bila kinyongo nilijongea alipokaa eneo la Break point nilimpa heshima yake nikamwambia "
mzee tunashukuru kwa makala kwa kweli tunapata chakula cha kutosha naye akajibu kwa tabasamu pana asnte tunashukuru kwa kutuunga mkono"

Haraka haraka nilichukua gazeti la Tanzania daima,na wiki hii kaandika"Rais wangu Kikwete:Nchi yangu kwanza
iwe salaam ya kitaifa"

Uandishi wake ni ule unaozingatia itifaki ya heshima,lkn kinachonishangaza pamoja na ushauri wake murua kwa
mpendwa raisi hajawahi kusikilizwa ushauri wake,mzee huyu amekuwa akifanya kazi Kama ya kutwanga maji kwenye
kinu.

Je ni lini serikali sikivu ya kinadharia itakuwa sikivu kwa vitendo ili isikie ushauri huu?

Mzee Mayenga songa mbele mbegu unayopanda haipotei bure
kama si leo itaota kesho.

Mungu akufungilie zaidi.
MUNGU akubariki mpendwa mwana mwema tushirikiane kumshauri Rais wetu.Sisi wana mwl forum motto yetu ni nhi yangu kwanza karibuni mwalimu forum.
 
Ila ana nikeraga anapomsifu Lowasa!

Hata kwenye maandiko imeandikwa mti wenye matunda ndio utupiwa mawe sijawahi kumsifia Edward Lowasa ila nimesema kweli na nitasema kweli daima, mbona ninapomsifu magufuli hamlalamiki?Je unataka kunichagulia maadui na marafiki? Je ungalipenda niwe mnafiki kwa taifa langu? TAFUTA KITABU CHA MWALIMU MKUU WA WATU,Ndipo utaelewa nimesimamia wapi.Siku zote uvivu nisawa na pesa;haukifu. ndani ya kichwa cha mtu mvivu ndimo ilimo karakana ya shetani. Na mtu mvivu ni sawa na jiwe lilopakwa mavi mvivu hana haki ya kula chakula. Natumaini utanielewa sasa Alamsiki. Mwalimu Mkuu
 
Mayega rafiki yake Lowassa,labda na yeye hawajakutana barabarani tutajuaje?Kibanda naye wiki mbili anamtetea Kinana kuwa ni kamanda!Yote maoni tu maana kila mtu na vionjo vyake,lakini ukitumia mas media kumsifia mtu ukaacha kuuchambua mfumo mzima unakuwa kama na fikra ziisizokuwa pana vile?

Sina urafiki na mtu yeyote pale unapo kosea nitasema kweli daima na unapofanya vema nitasema kweli je ninapo msifia Dr Slaa ni rafiki yangu? au mtasema mkatoliki mwenzangu? na kama umesoma makala yangu leo sijamsifu mtu ila nimekumbusha mungu anataka tufanye nini duniani
 
Ila ana nikeraga anapomsifu Lowasa!


Huwa namsoma sana Mzee huyu. Kwanza nimpe hongera zake kwa kufikisha miaka 60. Kusema kweli uandishi wake ni wakipekee sana. Kwangu, ni mwandishi namba moja! Ama kwa habari za Lowassa sidhani kama anamsifia. Huyu anaandika facts. Kwamba Lowassa kafanya mazuri na yakaonekana. Leo hii badala ya kuendelea kujenga taifa watu wanafanya upuuzi wa kuitana mafisadi ndani ya chama chao kwa ufisadi wanaojuana wenyewe! Tena ukisoma kwa makini ni kama vile anaonesha swala la Lowassa halikuwa 'handled' sawasawa na toka hapo tumeingia katika matatizo mpaka sasa. Mzee huyu ni mwandishi bora sana.
 
  • Thanks
Reactions: SG8
Makala yake ya wiki iliyopita alinifurahisha sana kuhusu kugombea uraisi. Anasema kama raisi ana mtu wake halafu anamficha basi hafai. Bangi ndio hufichwa! Haramu hufichwa! Sasa iweje raisi anasema hana kundi halafu mkewe na mwanae wampigie kampeni mtu mmoja? What a logic!
 
  • Thanks
Reactions: SG8
Hakuna anayeweza nunua uzalendo wa mtu na mamaye na ndio maana kila mara nasema mama yangu TANZANIA
Mwalimu Mkuu....Kama ni wewe kweli, ubarikiwe sana. Nimesoma makala yako ya leo umesema umetimiza miaka 60. Ubarkiwe sana. Niliposema inaweza kuleta sura ya kununulika sikumaanisha wewe umenunuliwa. Nilimaanisha kwamba kwa mtazamo wa baadhi ya watu unaporudia kila mara kumsifia mtu wanaweza kudhani umenunuliwa. Nafahamu kwamba Pascally Boniface Mayega...Mwandishi wa "Mwalimu Mkuu wa Watu" ni mtu mwenye maono ya mbali sana. Kama wewe ndie basi Mungu akuongezee walau miaka 15 hivi ili uendelee kuandika makala kwa ajili ya kutuunganisha watanzania. Nimewahi kukupigia simu mwaka 2010 ukanikaribisha Kongowe bahati mbaya siku ya pili nilikuwa na safari ya kwenda Mkoani. Sasa nipo hapa mjini na ningependa nipate japo saa 1 tu nionane na wewe.
Aidha ningependa kujua ni lini utamalizia ile sehemu ya pili ya Mwalimu Mkuu wa Watu kuhusu Rais ajaye. Kuhusu Lowassa, mimi ni miongoni mwa watu waliobadilisha mtazamo dhidi ya huyu ndugu kupitia maandishi yako. Zamani nilidhani yule Bwana ni fisadi tena fisaid pekee yake. Maandishi yako hasa ulipotoa sura halisi ya Samweli Sitta, Harrison Mwakyembe na Anne Kilango na Reginald Mengi na agenda yao ya ufisadi ilinibidi nitafakari upya. Sasa nipo huru na hata hapa jukwaani mara kadhaa nimesema. Lowassa yuko mbele sana kwenye medani ya uongozi hapa Tanzania....Kama anaongoza kwa ufisadi vile vile anaongoza kwa ukali na kusimamia kile anachokiamini. Madhambi yote ya serikali ya Rais wako yalibebwa na huyu kwani angesema kila kitu pale Bungeni leo ni dhahiri JK asingekuwa Rais...mwalimu (kama ni wewe lakini) Ubarkiwe sana na nitajitahidi sana kukutafuta tena ili nijaribu kuchota hekima na busara zako...
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom