Nimemuona Hassan Mwakinyo akipigana, maoni yangu ni haya

Niwe tu muwazi kwamba mimi si mtaalamu wa mambo ya boxing ila ni mfuatiliaji na mshabiki wa mchezo huu toka enzi za akina Tyson za kuamka alfajiri kusubiri pambano na Lewis. So ni shabiki wa mchezo ila si mwenye taalum nalo.

Jana majira ya saa nne usiku kulikuwa na pambano la masumbwi lililowakutanisha mtanzania mwenzetu Hassan Mwakinyo mwenye umri wa miaka 24 na muajentina Sergio Gonzales mwenye miaka 40.

Binafsi nililisubiri sana kwa hamu pambano hilo kutokana na ukweli kwamba nilikuwa sijawahi kushuhudia pambano la mtanzania mwenzangu Mwakinyo akipigana live zaidi ya kuona vipande tu vya youtube.

Jana nikatoka zangu mihangaikoni mapema kurudi nyumban kuona ndondi.

Ndondi zilikuwa za round 8 katika pambano ambalo halina mkanda. Lilianza round ya kwanza kwa kusomana mchezo baina ya wapinzani hawa wawili.

Kwa muda mfupi niliona kitu kwamba yule mzungu japo alikuwa umri umeenda lakini yupo makini sana ukimlinganisha na ndugu yetu ambaye mara zote alikuwa anarusha ngumi upepo bila kufika target.

Kwa mtu aliyeona pambano atakubaliana na mimi kwamba Mwakinyo alikuwa anapigwa sana ngumi za uso mpaka akaanza kupanic.

Hii ilimpelelea kuanza kurusha ngumi hovyo kabsa ndio zile zikawa znampiga jamaa mabegani na tumboni.

Mpaka round ya tano ambayo mzungu amekaa chini ni zile jamaa kampiga begani mkono ukashindwa kufanya kaz mwamuzi akaamua kuahirisha pambano kwa mahesabu ya TKO.

Maoni yangu ni kwamba the guy ni mzuri sana endapo atapata kocha mzuri atafika mbali maana umri bado unaruhusu ndio kwanza ana miaka 24. Lakini pia mwili wake umefanana na huu mchezo ambapo ndio credit kubwa pia.

Hassani bado hajaiva kuwa bingwa wa dunia wa kuweza kuhimili mikiki ya walimwengu kwenye uwanja wa boxing.

Kwa upiganaji wa jana kama angekutana na mtu mwenye ngumi nzito basi pambano lingeisha round ya tatu kwa yeye kupigwa.

Ongeza sana bidii ya mazoezi hasa upande wa kucheza na sura ya mpinzani wako.

Uzuri ni kwamba umekuja kipindi ambao nchi ina mwamko kwenye michezo na mambo mengine hivyo support unaipata, wenzio wakina Matumla walipigana kipindi hata google hakuna achana na whatsapp, facebooka au instagram.

Kila la kheri katika maisha yako ya michezo.
Nilifurahia mpambano wa wale wadada, mmoja wa kenya na mwingine wa Zambia. Mwakinyo sikufurahia pambano lake, sikulielewa, nadhani nikiangalia pambano linguine ndo nita m judge
 
mwakinyo ana uwezo wa kumpiga antony joshua
Hapa kwa uandikaji wa siku hizi, wachache utaelewana nao. Una maana "ana uwezo" katika maana ya "he is able" au "hana uwezo" katika maana "he is unable"???? Kwa sababu hiyo "h" kukosekana au kuwepo, inaleta maana mbili tofauti kabisa. Please clarify, ni "ana" au "hana"???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna pambano moja la mwakinyo alimpiga mzungu kwa KO, alichotumia ni kushambulia kwa kurusha ngumi nyingi mfululizo hadi mzungu akalemewa. Nadhani siyo technique nzuri sana ukikutana na bondia mwenye physique nzuri na ngumi nzito, kwa sababu unaporusha ngumi nyingi sana ambazo hazilengi target unakosa concentration katika kujilinda na possibly unaweza kuchoka mapema
 
Marehemu Thomas Mashali, Mbwana Matumla hawa ndio walikuwa maboxer, Marehemu Mashali alikosa discipline ya maisha akapotea.. Kwa sasa namuona Dullah Mbabe anakuja vizuri huyu Mwakinyo amepata promota au management nzuri inambeba lakini ni wa kawaida sana..

Watanzania wenzangu michezo ni fursa hebu wale wenye vipato mjaribu kuchukua management ya hawa watu kuanzia boxing, football na basketball.. Uwekezaji kwenye tasnia ya sports unalipa..na Tanzania vipaji viko vingi tatizo havifikiwi na hakuna watu serious wakuendesha hii biashara.. Nawaona maboxer wengi sana uswahilini huko ambao kama wanapata bahati ya kuingia kwenye ring za USA na EUROPE ni biashara kubwa sana..
Hao kina Dulla Mbabe ndo hamna kitu kabisa, wanapigana kama ameatur, rejea pambano lake na Cheka. Mwakinyo kidogo anaonesha utofauti, japo ana tatizo la defence, akirekebisha hilo atafika mbali maana kurusha ngumi kali anaweza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna pambano moja la mwakinyo alimpiga mzungu kwa KO, alichotumia ni kushambulia kwa kurusha ngumi nyingi mfululizo hadi mzungu akalemewa. Nadhani siyo technique nzuri sana ukikutana na bondia mwenye physique nzuri na ngumi nzito, kwa sababu unaporusha ngumi nyingi sana ambazo hazilengi target unakosa concentration katika kujilinda na possibly unaweza kuchoka mapema
Akikutana na mtu wa jamii ya Mayweather atachoka mapema, maana akirusha ngumi zake 20 zinaweza kumpata mbili tu tena dhaifu kwa jinsi jamaa anavyojua kukwepa, matokeo yake atachoka mapema na kupigwa kirahisi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niwe tu muwazi kwamba mimi si mtaalamu wa mambo ya boxing ila ni mfuatiliaji na mshabiki wa mchezo huu toka enzi za akina Tyson za kuamka alfajiri kusubiri pambano na Lewis. So ni shabiki wa mchezo ila si mwenye taalum nalo.

Jana majira ya saa nne usiku kulikuwa na pambano la masumbwi lililowakutanisha mtanzania mwenzetu Hassan Mwakinyo mwenye umri wa miaka 24 na muajentina Sergio Gonzales mwenye miaka 40.

Binafsi nililisubiri sana kwa hamu pambano hilo kutokana na ukweli kwamba nilikuwa sijawahi kushuhudia pambano la mtanzania mwenzangu Mwakinyo akipigana live zaidi ya kuona vipande tu vya youtube.

Jana nikatoka zangu mihangaikoni mapema kurudi nyumban kuona ndondi.

Ndondi zilikuwa za round 8 katika pambano ambalo halina mkanda. Lilianza round ya kwanza kwa kusomana mchezo baina ya wapinzani hawa wawili.

Kwa muda mfupi niliona kitu kwamba yule mzungu japo alikuwa umri umeenda lakini yupo makini sana ukimlinganisha na ndugu yetu ambaye mara zote alikuwa anarusha ngumi upepo bila kufika target.

Kwa mtu aliyeona pambano atakubaliana na mimi kwamba Mwakinyo alikuwa anapigwa sana ngumi za uso mpaka akaanza kupanic.

Hii ilimpelelea kuanza kurusha ngumi hovyo kabsa ndio zile zikawa znampiga jamaa mabegani na tumboni.

Mpaka round ya tano ambayo mzungu amekaa chini ni zile jamaa kampiga begani mkono ukashindwa kufanya kaz mwamuzi akaamua kuahirisha pambano kwa mahesabu ya TKO.

Maoni yangu ni kwamba the guy ni mzuri sana endapo atapata kocha mzuri atafika mbali maana umri bado unaruhusu ndio kwanza ana miaka 24. Lakini pia mwili wake umefanana na huu mchezo ambapo ndio credit kubwa pia.

Hassani bado hajaiva kuwa bingwa wa dunia wa kuweza kuhimili mikiki ya walimwengu kwenye uwanja wa boxing.

Kwa upiganaji wa jana kama angekutana na mtu mwenye ngumi nzito basi pambano lingeisha round ya tatu kwa yeye kupigwa.

Ongeza sana bidii ya mazoezi hasa upande wa kucheza na sura ya mpinzani wako.

Uzuri ni kwamba umekuja kipindi ambao nchi ina mwamko kwenye michezo na mambo mengine hivyo support unaipata, wenzio wakina Matumla walipigana kipindi hata google hakuna achana na whatsapp, facebooka au instagram.

Kila la kheri katika maisha yako ya michezo.


Hili tatizo analo tangu pambano na sam, ingawa ameimprove kidogo, lakini swala la ulinzi inabidi alifanyie kazi...... maana kuna mijitu ina technik za kudokoa sura balaa....... asipolewa sifa, atafika mbali kwa kuwa ana ngumi zinazoumiza
 
Mwakinyo ngumi zake utasema anasomea Youtube, ukweli kinachomrudisha nyuma sasa hivi ni kocha mzuri tu, uwezo anao na nia ya kua bora anayo, kinachomuangusha kupata kocha anayeelewa ngumi vizuri ka bongo ni kazi sana. Na jamaa life bado halijamyookea kivile, akijua technique vizuri anaweza fika mbali.
 
Hao kina Dulla Mbabe ndo hamna kitu kabisa, wanapigana kama ameatur, rejea pambano lake na Cheka. Mwakinyo kidogo anaonesha utofauti, japo ana tatizo la defence, akirekebisha hilo atafika mbali maana kurusha ngumi kali anaweza

Sent using Jamii Forums mobile app

Kama kweli unazijua ngumi sidhani kama unaweza kumsifia Mwakinyo kwa mapambano mawili aliyopigana ambayo yote hayakuwa ya ubingwa wowote zaidi ya kuwa mapambano ya utangulizi, pambano la juzi Nairobi amepigana na Muargentina mwenye miaka 41 na anaonekana kabisa yuko dhaifu..

Binafsi mapambano mawili ya namna ile huwezi kuniambia jamaa ni good boxer kiasi ya kumpa sifa tunazompa.. Rashidi Matumla, Mbwana Matumla walipambana mapambo mengi ya ubingwa walileta mikanda hivyo walistahili sifa kubwa...

Mwakinyo apambane na mabondia baadhi wa nyumbani ili adhihirishe ni bondia bora Tanzania, huwezi kusema ni bondia bora Tanzania wakati hakuna hata bondia mmoja wa ndani aliye bora ambaye umempiga zaidi kushinda mapambano ya utangulizi mawili..

Rashidi Snake boy kila mtu anamjua alivyowakarisha akina Maneno mtambo wa gongo, Cheka nk, Mbwana pia anajulikana alivyowakarisha mabondia wengi wa ndani kiasi cha kufikia namba tatu duniani WBC kwenye uzito wake..

Mwakinyo anapewa Umaarufu ambao hastahili kwenye boxing lakini bondia wa kawaida sana sana.. na tukiendelea kumpa kichwa hivi tutampoteza AFANYE MAZOEZI APIGANE MAPAMBANO MENGI YA UBINGWA NA YANAYOTAMBULIKA NA VYAMA VYA NGUMI, WBC, WBA, IBF nk kama wenzie maarufu waliomtangulia..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom