Nimemuheshimu rasmi David kafulila, Mbatia usikubali uteuzi kama wewe si mamluki

Ndugu,

Ukitaka kumuua nyoka kwa urahisi mti upake mafuta. Japo Shida yangu si tu chumvi iliyoko jikoni bali pia kuna hata sukari. Walamba chumvi/sukari wakiwekwa karibu na jiko sio kwamba yatabaki makopo tu ila wageni watakosa chai. Kwenye kampeini yalisemwa tukasema ...Mh anatafuta kura, Mh Kafulila alisema tukasema anataka uwenyekiti! Mafuta bado yapo tupake miti mingine????
 
NCCR Mageuzi kwa ujumla sio chama cha upinzani tangu kilipoanzishwa, lengo lake lilikuwa kuwadhoofisha wapinzani wa CCM, Jaribu kuwakumbuka waanzilishi wake, kuna Masumbuko Lamwai, Stephen Wasira (Tyson) Mabere Marando na wengineo jinsi wanavyofanya kazi, katika hao mmoja yuko CDM, Ni hatari kweli!

Professor Baregu Mwesiga naye alikuwa NCCR na hata kuingizwa kwake kwenye tume ya katiba, nahisi ni bao kwe wana mageuzi!!!!
 
Hapo kwenye red kwa Mbatia itakuwa ngumu kwani udenda ulikuwa unamtoka kwa kukosa ubunge hadi akafungua kesi ya kumpinga Halima Mdee leo hii kapewa aukataee itakuwa ngumu sana. Mbatia sio mwana demokrasia ni ndumila la kuwili ama naweza kusema ni kibaraka wa CCM ndani ya upinzani.
Wewe umemjua leo, huyo tangu enzi za Mzee wa Kiraracha aliyetimuliwa NCCR kwenda TLP ndivyo alivyo, yuko kikazi zaidi analipwa fadhila sasa!!!!!

 
nani alikwambia Raisi akikuteua kuwa Mb unakataa??? wewe si unajua kuwa NCCR ilisambaratishwa na baadhi ya walioitwa vibarua, hata hao wa kigoma sijui hawajui chama gani, kwa mfano Mbatia akiwa M/kiti na Mb wa ikuteuliwa na Rais atakataa kupiga kura ya kumpongeza aliyemchagua, Mwaego ngd Mbatia jiimbie ka wimbo ketu " Chama Chetu Cha Mapinduzi chajenga nchi" uendelee kula.
 
Asipokubali uteuzi atakua anatukana sisi watanzania amabo tunahitaji msaada wake kwani tangu mwanzo si alikua anatafta kuwa mwakilishi wa wananchi,,sasa kapata nafasi sisi huo uwakilishi wake tutaupima kwasababu haendi kufanyia uwakilishi wake ahera bali ni pale mjengoni km atakuwa tofauti na wengine tutaona tu so acha tumpe mda wa kuingia bungen kwa kutumia hiyo nafasi aliyopewa na mkuu wa kaya....naunga mkono hoja ya rasi kwa kmteua
Mteule yeyote wa rais hawajibiki kwa wananchi bali anawajibika moja kwa moja kwa aliyemteua(Rais),
kwa hiyo basi kama dhana ya upinzani ni kuchallenge chama kilichopo madarakani basi kwa NCCR, hiyo imekufa, hataweza kupinga kwa dhati kabisa maovu yatakayofanywa au kuidhinishwa na watu wa CCM. kumbuka kwamba Mbatia kama mteule wa Rais itambidi anyenyekee kwa RAIS kuliko hata wabunge wa ccm wenyewe. Huo ni usaliti wa hali ya juu kabisa kwa upinzani nchini na kama kuna mwana NCCR yeyote mwenye uchungu na watanzania japo kodogo kama chembe ya haradani basi namuomba arudishe kadi ya chama. Kama wafuasi wote wa NCCR wanajua tangu mapema kwamba mwenyekiti wao ni mamluki mwrenye lengo la kuua upinzani waendelee na chama chao cha mamluki, Lakini hawataweza kuzuia mabadiliko.
 
Back
Top Bottom