Nimemtia mimba mzazi mwenzangu akiwa kwenye ndoa yake ya miaka 7. Nifanye nini?

Kweli SINGLE MAZA sio wa kuoa..
#YNWA
Miaka 9 iliyopita nilimtia mimba Mwanachuo wa mwaka wa 2 akajifungua mtoto wa kiume. Hatukuweza kuoana maana na mimi ndiyo kwanza nilikuwa nina mwaka mmoja mtaani sina mbele wala nyuma.

Hivyo kila mtu alishika 50 zake na kutafuta mwenza wake mpya wa maisha. Lakini malezi ya mtoto niliyabeba kama baba.

Yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kumpata mwenza wake wa maisha. Alimpata miaka 7 iliyopita na sasa wana watoto 2 ndani ya ndoa yao

Mimi nilichelewa kidogo kwasababu ya kujipanga kimaisha, ndoa yangu ndiyo kwanza ina miaka 2 na nina mtoto wa miezi 7.

Miezi 2 iliyopita nilienda semina mahali fulani. Nikakutana na mzazi mwenzangu naye akiwa ni mshiriki wa semina ile. Kwa kuwa mke wangu ana katoto kachanga ka miezi 7, na kwakuwa huyu mzazi mwenzangu tumekutana mazingira mapya ya semina, na kwakuwa jicho lilimtamani kwa jinsi alivyo nawiri na kustawi basi semina ilienda vizuri.

Juzi nimepigiwa simu na mzazi mwenzangu akidai ana mimba yangu na mumewe amegoma kuikubali.

Sasa mabibi na mabwana, nawauliza suala hili nilishughulikie vipi?
  • Nikubali ama niikatae mimba hii?
  • Nikiikataa itakuwaje endapo mtoto atafanana na mm na mumewe anaijua chapa yangu kupitia mtoto wangu wa kwanza?
  • Je, nikikubali mke wangu patakalika?
Naombeni suluhisho la suala hili pasipo kuvuruga ndoa yangu changa.
 
Kwa sababu mzazi mwenzio amemshirikisha mume wake, na mume akaikataa, basi na wewe mshirikishe mkeo mpya, na yeye akiikataa hiyo mimba basi ngoma droo.
 
Nyie ndo mnawatia doa wanawake walioolewa wakiwa na watoto, ule usemi kua baba mtoto atakuja kupasha kiporo ndio huu sasa.
 
Nenda kwny uzi wa kula tunda kimasihara utagundua hakuna uhusiano wowote wa kiwa na mtoto na kupasha kiporo demu akiamua kuliwa analiwa tu..
Umalaya tabia ya mtu mnawaonea bure ma single maza
Nyie ndo mnawatia doa wanawake walioolewa wakiwa na watoto, ule usemi kua baba mtoto atakuja kupasha kiporo ndio huu sasa.
 
hata kuandika hawezi kwa mfumo huu jiandae na wewe kupewa mimba na darasa lako la MEMKWA
 
Ana kazi nzuri na mshahara mnene kuliko mm mkuu. Fedha anayo, nadhani anaweza kujitenga endapo mumewe atazingua.
Kama ni hivyo basi mshauri atoke kwa jamaa aanze kujiyegemea kabisa .....ili uwoga na mashaka kwako vipungue maana yule sasa hivi akidhuriwa kwa lolote ujue na wewe lazima uhusishwe tu hakuna namna
 
Kuna muda huwa nawaza hv hii mikasa ni ya kweli ama kuna kampeni maalum ya kuwachafua hawa singo maza? Nawahurumia sana kiukweli sina tu namna ya kuwasaidia!
 
Kuna muda huwa nawaza hv hii mikasa ni ya kweli
Mikasa hii ni ya kweli mkuu. Isipokuwa wanaJF kwa weledi wao huwa wanabadilisha kidogo ili wahusika wasielewe kuwa ndiyo wao wanazungumziwa.

Lkn pia wanaJF huwa wanaepuka kutaja maeneo (mitaa/miji/mikoa/majiji) yalikotokea matukio haya kwa lengo la kuwachanganya wahusika. Usikute kisa hiki kinakuhusu mkuu.
 
sema mtatisha sana...mtoto wa kwanza na wa nne baba mmoja halafu wa pili na tatu baba mmoja
 
The blood will fall u wereva! Acha upoyoyo! Accept the price of your desire
 
Miaka 9 iliyopita nilimtia mimba Mwanachuo wa mwaka wa 2 akajifungua mtoto wa kiume. Hatukuweza kuoana maana na mimi ndiyo kwanza nilikuwa nina mwaka mmoja mtaani sina mbele wala nyuma.

Hivyo kila mtu alishika 50 zake na kutafuta mwenza wake mpya wa maisha. Lakini malezi ya mtoto niliyabeba kama baba.

Yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kumpata mwenza wake wa maisha. Alimpata miaka 7 iliyopita na sasa wana watoto 2 ndani ya ndoa yao

Mimi nilichelewa kidogo kwasababu ya kujipanga kimaisha, ndoa yangu ndiyo kwanza ina miaka 2 na nina mtoto wa miezi 7.

Miezi 2 iliyopita nilienda semina mahali fulani. Nikakutana na mzazi mwenzangu naye akiwa ni mshiriki wa semina ile. Kwa kuwa mke wangu ana katoto kachanga ka miezi 7, na kwakuwa huyu mzazi mwenzangu tumekutana mazingira mapya ya semina, na kwakuwa jicho lilimtamani kwa jinsi alivyo nawiri na kustawi basi semina ilienda vizuri.

Juzi nimepigiwa simu na mzazi mwenzangu akidai ana mimba yangu na mumewe amegoma kuikubali.

Sasa mabibi na mabwana, nawauliza suala hili nilishughulikie vipi?
  • Nikubali ama niikatae mimba hii?
  • Nikiikataa itakuwaje endapo mtoto atafanana na mm na mumewe anaijua chapa yangu kupitia mtoto wangu wa kwanza?
  • Je, nikikubali mke wangu patakalika?
Naombeni suluhisho la suala hili pasipo kuvuruga ndoa yangu changa.
Mwambie asiwazee
 
Back
Top Bottom