Nimemtafuna mke wake...!

sinafungu

JF-Expert Member
Feb 13, 2010
1,524
863
Kwa fitina na taarifa potofu anazotoa juu yangu, nami ni rafiki yake muda mrefu na tuko wote kampuni moja,kila nikimtaka tukae tujadili kuhusu mambo anayonizushia huku akisahau tulikotoka.

Huku amesahau mimi ndiye msuruhishi mkuu wa ndoa yake ambayo mara zote yeye ndiye mkorofi.

Nikaona dawa ni kukubali nafasi nilipewa na shemeji wangu muda mrefu , niliikataa kwa kuheshimu mahusiano yetu, ndugu yangu utanisamehe sana.
 
Kwahiyo umeona ndio njia sahihi yakumkomoa rafiki yako?Ila tambua kuwa malipo ni hapahapa mkuu
 
sinafungu, ni kwa nini u rule out kuwa wewe siye mkosaji kwa yale ambayo yametokea na kusababisha mshindwe kuonana kama matakwa yenu?

Kitendo cha wewe kutumia upenyu ulikuwa nao kulala na mkewe inatoa picha hata katika shughuli na hali ya kawaida wewe si wa kuaminika. Pengine anakukwepa kwa tabia zako fulani ambazo kwake hazimfurahishi, na pengine haya yote unayosema umemsaidia si wewe peke yako; kuna wengine wamefanya zaidi yako.

Inasikitisha sana kuwa siku zinavyozidi kwenda mbele jamii inakuwa ikichekelea yale ambayo huonekana ni kinyume na maadili ya kawaida ya kila siku. Umeona haitoshi wewe kutembea na mkewe ila pia ulitangaze kwa watu wengine.

Nakusihi angalia sana nyenendo zako, unaweza kuona kana kwamba yale unayofanya unakomesha kumbe unajikomesha mwenyewe. What goes around comes back around.
 
Ujiandae kuliwa nawewe.........Ongea na mwanaumme mwenzako mrekebishe yaliyokaa hovyo badala ya kujitafutia kesi ya mwizi wa mke wa mtu!!!
 
sinafungu wewe ni fungu la kukosa je kama mke wake ana mchepuko na mchepuko wake hapo sijahesabu upande wa rafiki yako utapona kweli
 
Last edited by a moderator:
My sis AshaDii miss you more my sis
Bora nikuone one humu kwa muda inatia moyo kuwa tuko pamoja
Kibaya kafanya kosa na anajisifia kwa kujitangaza kosa alilolifanya na hebu jiweke kwenye viatu vya rafikio aliyekuamini licha ya mapungufu yake na matatizo yake kujua kuwa umetembea na mke wake
 
Last edited by a moderator:
sinafungu wewe ni fungu la kukosa je kama mke wake ana mchepuko na mchepuko wake hapo sijahesabu upande wa rafiki yako utapona kweli
 
Last edited by a moderator:
mke wa mtu ni sumu.... ukiona unakolea kwenye penzi la mke wa rafiki yako ..... chonde chonde nenda sambamba na kufanya mazoezi ya kushika ukuta soon utashika ukuta mkuu...
 
My sis AshaDii miss you more my sis
Bora nikuone one humu kwa muda inatia moyo kuwa tuko pamoja
Kibaya kafanya kosa na anajisifia kwa kujitangaza kosa alilolifanya na hebu jiweke kwenye viatu vya rafikio aliyekuamini licha ya mapungufu yake na matatizo yake kujua kuwa umetembea na mke wake


R' nimewamiss pia. Tupo pamoja sasa, hata kama ni hapa na pale si consistently ila nipo my dear.

Vijana siku hizi wanaona ni sifa kutangaza ovyo hasa tabia/vitendo kama hivi. Swali linabaki, alivyolala na mke wake kaongeza nini? Katatua tatizo lile lililo kuwepo awali? Anasema siku zote alikuwa ni rafiki mwema kwake na hapo hapo anasema kaamua kulala na mkewe (aliyempa nafasi muda mrefu); angekuwa ni mwema kwa rafiki yake basi toka hapo kitambo angemweleza rafiki yake amkanye mkewe nyenendo zake (or angemkanya mwenyewe).

Nahisi alikuwa na nia hiyo toka kitambo na hii ni justification tu ili asisikie guilty (ikiwa kweli ana utu).
 
R' nimewamiss pia. Tupo pamoja sasa, hata kama ni hapa na pale si consistently ila nipo my dear.

Vijana siku hizi wanaona ni sifa kutangaza ovyo hasa tabia/vitendo kama hivi. Swali linabaki, alivyolala na mke wake kaongeza nini? Katatua tatizo lile lililo kuwepo awali? Anasema siku zote alikuwa ni rafiki mwema kwake na hapo hapo anasema kaamua kulala na mkewe (aliyempa nafasi muda mrefu); angekuwa ni mwema kwa rafiki yake basi toka hapo kitambo angemweleza rafiki yake amkanye mkewe nyenendo zake (or angemkanya mwenyewe).

Nahisi alikuwa na nia hiyo toka kitambo na hii ni justification tu ili asisikie guilty (ikiwa kweli ana utu).


Sijaona urafiki hapa AshaDii ila naona tuu uzinzi unapewa kipaumbele. Ameona nyendo za mke wa rafiki yake muda mrefu na badala hata ya kumweleza hilo the so called friend kaamua kukaa kimya na mwishowe kafanya kile ambacho hakupaswa kufanya
Na by the way inaonyesha walianza siku nyingi sana kutengeneza mazingira haya na hii ya matatizo na kutokuelewana kati yake na rafikiye imekuwa justfication tuu ya kuionyesha walichodhamiria
 
Last edited by a moderator:
kwa fitina na taarifa potofu anazotoa juu yangu, nami ni rafiki yake muda mrefu na tuko wote kampuni moja,kila nikimtaka tukae tujadili kuhusu mambo anayonizushia huku akisahau tulikotoka. huku amesahau mimi ndiye msuruhishi mkuu wa ndoa yake ambayo mara zote yeye ndiye mkorofi. nikaona dawa ni kukubali nafasi nilipewa na shemeji wangu muda mrefu , niliikataa kwa kuheshimu mahusiano yetu, ndg yangu utanisamehe sana

Muosha huoshwa!!
 
AshaDii mambo? Missed you.
Huyu kijana anaamini ataonekana mwanaume zaidi kwa kutangaza upuuzi kama huu...wewe puuza tu...na mimi nimepuuza.
 
Last edited by a moderator:
hiyo ndo njia uliyoona ni sahihi kusolve tatizo? na unachekelea dah!!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom