Nimemsikiliza Mzee Butiku dakika 45 za ITV na Radio One ameongea mengi, ila haya ndiyo yameonyesha kwanini Yeye ni Hazina ya Fikra Kubwa Tanzania

Umefanya vizuri kuyaweka kwenye mtiririko wa orodha.

2. "Tunataka Katiba Mpya" itakayowezesha kila mtu kuwajibishwa kwa mujibu wa katiba hiyo. Hii ya sasa kuna watu wapo juu yake, hawawezi kuwajibishwa kutokana na katiba hii.

3. Tanzania sasa ina watu wanafiki kila sehemu, na hii ni kutokana na siasa za kuleana zilizopo ndani ya CCM. Watu wanaogopa kuwa wakweli, kwa sababu maslahi yao yote wamewekeza kwenye chama. Ondoa chama hicho, watu wataanza kuwa huru na kuwa wakweli.
4. Vijana? Watakuwaje majasiri huku wakijua maslahi yao yapo ndani ya chama. Watapozwa pozwa na kusahau kwamba nchi watakayoirithi ni mzoga.

5. Viongozi wanaotishia watu, wanajuwa vyombo vinavyotakiwa kulinda haki za wananchi hao vimo mifukoni mwao. Bila kuwa na uhakika huo, kammwe hawawezi kumtishia yeyote.

6. Vyombo vya habari? Oooh, nchi hii ina vyombo vya habari tena? Kila mtu anatafuta upendeleo wa kuteuliwa au kufanikishwa katika shughuli zake na hao hao wanaosababisha matatizo yote ya nchi hii, CCM.

7. Ni wapi waliowekwa madarakani. Wote wamejiweka madarakani kwa nguvu.

Mzee Butiku na Mzee Warioba wamebaki kuwa sauti za nyikani tu, hawasikilizwi na hao watawala wala hawawanyimi usingizi. Wamekuwa ni watu wa kupuuzwa tu!
Mtawala katili kama huyu hawezi sikiliza kitu chochote
 
1. Tanzania bado ina Viongozi Waonevu na bahati mbaya tena wengine bado tu wanarandaranda Mitaani na sijui kwanini hawagusiki na wanaogopwa na wenye Kuwawajibisha.

2. Tunataka Katiba Mpya je, yale yaliyopo Katiba iliyoko tumeyatekeleza hata kwa 75%?

3. Taifa letu sasa lina Watu Wanafiki ambao wakiwa Vichochoroni wananung'unika ila wakiwa mbele ya Viongozi wao wananyamaza.

4. Vijana wa Leo nchini Tanzania ni Waoga watupu.

5. Viongozi wanaotishia Watu wanaowakosoa ni Wasaliti wa Katiba yetu na kamwe hawatufai.

6. Vyombo vya Habari vya Tanzania siku hizi haviibui Mambo ya Kuwaamsha Wananchi kuhusu nchi yao, bali vinaibuliwa Mambo na Watawala kwa yale wayatakayo Wao.

7. Tujitahidi sana Kuwaheshimu Viongozi ( Watawala ) wetu hata kama kuna wanaotukwaza kwani ni Sisi hawa hawa ndiyo tumewaweka Madarakani walipo na kama tukitaka Kuwakosoa basi tuwakosoe kwa Staha na huu ndiyo umekuwa ( uwe ) Ustaarabu wa Watanzania.

Ninakuombea Uhai mrefu Mzee Butiku.
Hiyo point ya 7 sikubaliani nayo. Hivi kweli uchaguzi iliyofanywa na Tume ya Mahela kwa maelekezo toka juu.... Huyu mzee bado anataka kutuaminisha kuwa ni sisi ndiyo tuliowaweka madarakani....!! Seriously....!!
 
Hata Lisu ni muog tu ndiyo maana alijificha kwenye ubalozi na kisha kukimbiza ubawa wake Ubelgiji.
At least yeye ana sababu ya kuogopa baada ya kunusulika na kifo. Pia anachoogopa yeye ni kifo ila haogopi kusema...... Ila wengi wetu kusema tu tunaogopa!!
 
Umezuiwa kuanzisha Uzi unaomhusu Slaa? Yeye kapenda maelezo ya Butiku na ana sababu ambazo Wenye busara ndani ya JF wanajua Kwa nini!! Wewe kama unaona aliyoongea Slaa yana uzito anzisha Uzi wako watu wachangie.
'Genius' kama Wewe Mkuu na Rafiki yangu mkubwa hapa JamiiForums unapata wapi muda wa kuppteza Kumjibu huyo 'Certified Fool' aitwae KING KIGODA?

Ukiona GENTAMYCINE namnyamazia Mtu ambaye ama amenikwaza au amenichokoza hapa JamiiForums jua ya kwamba nakuwa 'nimeshamdharau' kwa Kiwango cha Kumfananisha na Kinyesi cha Uharo na Kinachonuka kwa Kutukuka.

Hata hivyo Heko tu kwa Kumpa makavu.
 
Mbona watanzania wote wanajua kuwa Tanzania miaka 60 bado ni maskini kwa sababu ya ufisadi na ubadhirifu Mali ya umma?
Maendeleo yanaletwa na Matumizi Bora ya rasilimali za nchi, Kodi ya Nchi, uzalendo, utawala Bora na haki za binadamu ambazo zinawezekana ki rahisi Sana ktk Taifa ambalo watu wameamua kuishi kijamaa!

Ujamaa ni nguzo halisi ya maendeleo!

CCM inajinasibu kuwa chama ni Cha kijamaa, na serikali ni ya kijamaa lakini uhalisia ni kwamba Tanzania hatujawahi kuwa wajamaa

Taifa la kijamaa halina uhujumu uchumi, kubambikiana kesi, kunyanyasa Raia, hakuna rushwa wala wizi wa kura, kukanyaga Katiba, hakuna muungano wa serikali mbili Bali serikali moja, hakuna vyama vingi vya siasa, hakuna kikosi Cha wasio julikana, hakuna mifumuko ya Bei holela n.k

Munaotukana ujamaa, hamuujui ujamaa! Tanzania hatujawahi kuishi ujamaa,

Wanadamu Wana mioyo ya ubinafsi, hawatakuja kuishi ktk ujamaa!

Ujamaa utabaki kwenye serikali ya mbinguni tu
Ujamaa/Socialism upo wa aina nyingi sana hapa duniani.
1. Kuna ule Ujamaa wa Kimarksi (Marxism) ambao ulikuwepo Urusi, Uchina na Afrika.
2. Kuna ule Ujamaa wa Kidemokasia (Social-Democracy) ambao kule kwenye nchi za Scandinavia.
3. Kuna ule Ujamaa wa kiparadiso (Utopian Socialism) ambao uko kwenye vitabu vya dini kama Biblia.

Wewe unauongelea Ujamaa upi huo ambao unalinda haki za binadamu: Kama unazungumzia Ujamaa wa Kimarksi, umechanganya mambo. Maana Karl-Marx na wafuasi wake kama Lenin, Stalin, Mao, Nyerere na Nkurumah hawaamini katika haki za binadamu (Individual and Basic Rights), wanasema zinaigawa jamii, wenyewe huamini katika haki za kiuchumi (Economic Rights) kama zile za kutoa elimu na afya bure.

Kiufupi msingi mzima wa hii falsafa ni uchumi wa vitu (Materialism) tu, ambapo wanaamini kabisa ukidhibiti Uchumi wa nchi kinguvu na kugawanya rasilimali za ummah, basi matatizo yote ya binadamu yataisha. Lakini, kuna ukweli wowote hapa ??? Binafsi nimeusoma UJAMAA kwa miaka zaidi ya kumi na nimeona matatizo yake makubwa.....

Ujamaa wa Scandinavia ni ule wa ambao umejengwa kwenye msingi wa Demokrasia ya kimagharibi (Western Democracy), Usawa kihaki na kifursa kwa wanajamii wote (Egalitarianism) na Muingilio wa moja kwa moja wa serikali katika kuwainua wananchi (The Welfare State). Huku mbali na Uchumi wa vitu, wanazingatia mambo mengi ya msingi ambayo yako kimaadili.....

Ujamaa wa kiparadiso sasa ndiyo ule wa Mbingu-Mpya na Nchi-Mpya ambao Adamu na Hawa waliishi kule Bustani ya Eden. Hakuna dhambi, hakuna umasikini, wanadamu wote sawa, hakuna serikali, hakuna magonjwa n.k Yani mambo bwelele. Hata Karl Marx anavyoandika kuhusu Ujamaa wake aliiga huu Ujamaa wa kwenye Biblia.

Haya sasa: Mkuu wewe unauzungumzia Ujamaa upi hapa, ili twende sawa ???
 
1. Tanzania bado ina Viongozi Waonevu na bahati mbaya tena wengine bado tu wanarandaranda Mitaani na sijui kwanini hawagusiki na wanaogopwa na wenye Kuwawajibisha.

2. Tunataka Katiba Mpya je, yale yaliyopo Katiba iliyoko tumeyatekeleza hata kwa 75%?

3. Taifa letu sasa lina Watu Wanafiki ambao wakiwa Vichochoroni wananung'unika ila wakiwa mbele ya Viongozi wao wananyamaza.

4. Vijana wa Leo nchini Tanzania ni Waoga watupu.

5. Viongozi wanaotishia Watu wanaowakosoa ni Wasaliti wa Katiba yetu na kamwe hawatufai.

6. Vyombo vya Habari vya Tanzania siku hizi haviibui Mambo ya Kuwaamsha Wananchi kuhusu nchi yao, bali vinaibuliwa Mambo na Watawala kwa yale wayatakayo Wao.

7. Tujitahidi sana Kuwaheshimu Viongozi ( Watawala ) wetu hata kama kuna wanaotukwaza kwani ni Sisi hawa hawa ndiyo tumewaweka Madarakani walipo na kama tukitaka Kuwakosoa basi tuwakosoe kwa Staha na huu ndiyo umekuwa ( uwe ) Ustaarabu wa Watanzania.

Ninakuombea Uhai mrefu Mzee Butiku.
Butiku hawezi kutuambia kuhusu haki hasa baada ya kuwadhurumu watoto wa Mwalimu wakati baba yao akiwa hai na kuwafanya wawe hivyo walivyo sasa.
 
Umezuiwa kuanzisha Uzi unaomhusu Slaa? Yeye kapenda maelezo ya Butiku na ana sababu ambazo Wenye busara ndani ya JF wanajua Kwa nini!! Wewe kama unaona aliyoongea Slaa yana uzito anzisha Uzi wako watu wachangie.
Asinge mtaja basi kwa chochote humu!.
 
'Genius' kama Wewe Mkuu na Rafiki yangu mkubwa hapa JamiiForums unapata wapi muda wa kuppteza Kumjibu huyo 'Certified Fool' aitwae KING KIGODA?

Ukiona GENTAMYCINE namnyamazia Mtu ambaye ama amenikwaza au amenichokoza hapa JamiiForums jua ya kwamba nakuwa 'nimeshamdharau' kwa Kiwango cha Kumfananisha na Kinyesi cha Uharo na Kinachonuka kwa Kutukuka.

Hata hivyo Heko tu kwa Kumpa makavu.
Popoma mnafiki slaa voice.
 
Huyu Butiku angekuwa na busara angesikika na kuonya wakati JIWE anakiuka katiba kwa maanuzi yake yaliyowakandamiza wananchi.

Enzi yake Jiwe alijitahidi sana kuonekana kuwa anafuata nyayo za Mwalimu kumbe alikuwa chui tu aliyevaa ngozi ya kondoo na Watu kama Butiku wakamuamini Kuwa alikuwa anafuata nyayo za Mwalimu hasa pale alipolazimisha kuhamia DODOMA hata bila matayarisho!! Kutumika Jina la mjomba wake kukamfunga mdomo!

Je, Butiku alikuwa wapi wakati Jiwe anawatisha wananchi na kuwanyima uhuru wao kwa kutumia vyombo vya dola kuwathibiti?

Kwani ni vijana tu wanaotakiwa kunung'unika na wazee sio sehemu ya jamii inayotakiwa kuonesha ujasiri pale haki inapopokwa?

Butiku anajitokeza sasa ili nae aonekane Kuwa yupo lakini hana faida kwa sasa kwa maendeleo ya Taifa hili. Ana jukumu la kuisaidia familia ya mwalimu ambayo inahitaji sana msaada wake kwa hivi sasa kwani Ukoo una VITUKUU!
Umendika nilichotaka kiqndika. Wakati wanaosema wanaminywa kusema. Butiku anawalaumu hao hao kuwa ni waoga.
Anaishi Tanzania tofauti na tunayoishi. Tatizo ni hilo gorofa analonyonya kidogo kidogo hapo Sokoine Drive
 
26 Reactions
Reply
Back
Top Bottom