Nimemsikiliza kwa umakini Ester Bulaya kisha John Heche, wanasikitisha sana na wanahitaji huruma

Nigrastratatract nerve

JF-Expert Member
Sep 4, 2019
1,395
3,897
Aliyekuwa Mbunge wa Bunda Mjini kupitia CHADEMA ndugu ESTER BULAYA nilimsikiliza kwa umakini sana wakati akiwahutubia wananchi wake.

Alijinasibu kuwa yeye simba jike alijinasibu kuleta maendeleo Bunda mjini ikiwemo maji, madawati, Barabara huku akiiponda serikali ya CCM.

Nilijiuliza sana mbunge huyu ambaye chama chake kila mara kilipiga kura ya kupinga bajeti ya serikali hayo anayoyasema yametekelezwa alipinga, wabunge wa Upinzani akiwemo ESTER BULAYA waliigomea bajeti wazi wazi. Kugomea bajeti maana yake ni kupinga maendeleo ya aina yoyote yasiende Tanzania yakiwemo na majimbo ya Upinzani ndio maana pamoja na kuongea kwa sauti za kiuanaharakati lakini wananchi hawakuonyesha ushirikiano.

Pamoja na kuonyesha bashasha wananchi walijiinamia yaani nguvu iliyotumika it was inversely proportional to the response.

Watu walionekana kujiinamia tu, CHADEMA walisahau kilichowafanya wapendwe na wananchi ni kuwatetea kuwapigania, kuwasemea matatizo yao, kuwaimbia matatizo yao.

Wananchi wa Nyamongo hawajasahau vile CHADEMA walikuwa upande wa Mabeberu wakimsaliti wazi wazi mpiganaji jemedari watu.

Ukipanda pumba utavuna pumba hivi ndivyo CHADEMA wakichokipanda wacha wakivune anguko LA chama hiki litakuwa la karne yaani Nina uhakika hakiwezi kupata hata Diwani mmoja

Magufuli aliimba tuunganeni tuijenge nchi nyie mnang'ang'ana kumshambulia kwa maneno ya kejeli wananchi mlikuwa mnawakera sana.

Hali niliyoieleza kwa ESTER BULAYA imetokea kwa HECHE, yaani wananchi hawana furaha wamenuna

Nawashauri CHADEMA wakitaka washinde walau majimbo machache waeleze Sera waache kumshambulia Magufuli na CCM watapotea kabisa tena hawataoneka

Magufuli na CCM ni tunu ya nchi kwa ss hatuna Budi kumuombea mpakwa mafuta wa bwana..

Jamani fungueni Cilp za Heche na BULAYA mtaona
 
Chadema ya Mlevi Mbowe haina Mbinu za Kisiasa.

Walimpinga na kumtukana sana Shekhe JK hata hivyo ustadhi wa watu alikua mnyenyekevu sana.

Hakuwabagua ,wakapata umaarufu mkubwa kwa kumdhalilisha pamoja na serikali yake. Huo ulikua Mradi wa Mbowe.

Awamu hii wamekutana na Chuma cha pua kwa kukosa Mbinu Chadema ya Mlevi ikaja na Mbinu zilezile za kilevi. Wakafikiria watapata maujiko kama kawaida yao matokeo yake wamepoteza ramani kabisa.

Mbowe nitamlaumu mpaka siku nitakapomsikia ametupwa Gerezani kifungo cha Maisha kwa uhuju uchumi na uchocheze wa kutisha.

Mbowe alihamasisha siasa za kitoto kabisa tena watoto wenye utindio wa ubongo. Kama huyo Mzinzi na Mlevi Mbowe angeacha Demokrasia ishamiri ndani ya Chadema hakika mwaka huu ilikua inapata wabunge zaidi ya 150. Kwa kukosa Hekima na maarifa Mbowe akaendekeza ubabe,ufuska,ulevi, uzushi, chuki dhidi ya makabila mengine tofauti na kabila lake na kuwalazimisha wafuasi na wabunge toka Chadema kuwa kama robot kufuata anachotaka ikiwa ni pamoja na kutoka nje ya bunge na kupinga hata maendeleo ya wazi waliyoyapigania kwa Miaka mingi huku wakiwazomea wabunge wa vyama vungine na kuwafukuza wale waliotumia haki yao ya kikatiba kutoa maoni yao na kuwa huru kumuunga mkono Mh.Rais au kumpinga.

Msanii ,mlaghai na mwizi Mbowe anapiga demokrasia badala ya kuipigania kwa kuwalazimisha wabunge na madiwani wake kufuata anachotaka ikiwa ni pamoja na kususia shughuli za maendeleo hata kama zinafanyika kwenye majimbo yao ( ujinga uliohitimu kwa kiwango cha PhD.)

Sasa ubaya ubaya. Mlevi na Mlevi wake alifikiri kuwa ataitisha Serikali na JPM.
 
Hujui kichokuwa kinagomewa kwenye bajeti, na ilikuwa ni kwa manufaa ya wananchi, bajet inapewa 3% kilimo??? na huku ndiko kundi kubwa lilipo..

Mbunge kazi yake ni kuhakikisha serikali inafikisha huduma zote muhimu kwa wananchi wake, mbunge hakusanyi kodi mkuu jielimishe uelewe namna nchi inavyoendeshwa ili usipotoshe bila kukusudia.
 
Sawa je jimboni kwake kawafanyia mambo gani baada ya kupinga kila kitu miaka 5
Hujui kichokuwa kinagomewa kwenye bajeti, na ilikuwa ni kwa manufaa ya wananchi, bajet inapewa 3% kilimo??? na huku ndiko kundi kubwa lilipo..

Mbunge kazi yake ni kuhakikisha serikali inafikisha huduma zote muhimu kwa wananchi wake, mbunge hakusanyi kodi mkuu jielimishe uelewe namna nchi inavyoendeshwa ili usipotoshe bila kukusudia.
 
Hebu kwanza tuwekee hizo picha za hao wananchi walionuna na kujiinamia kwenye hiyo mikutano wakati wanawasikiliza hao Wabunge wao ili uaminike!

Kinyume na hapo, unastahili kabisa kudharauliwa.
 
Upinzani kote Dunian wanapinga wakiamini mawazo Yao ndio bora

Sasa kama utakuwa unakubali tu mwisho wake unakuwa kama mrema
 
Nimesoma huu uzi nikagundu hauna hoja ya msingi lakini pia alieuleta hajui maana ya kambi ya upinzani bungeni

Endelea.kubudu na kumtukuza yesu

Kambi lasmi bungeni ni kuweka mawazo mbadala au kusahihisha palipo na kosa, na sio kupinga kila kitu.
Sasa unapinga, alafu vinapofanyika unasema ni wewe,
Sasa ulivifanyaje wakati ulipinga?
 
wabunge wa Upinzani akiwemo ESTER BULAYA waliigomea bajeti wazi wazi. Kugomea bajeti maana yake ni kupinga maendeleo ya aina yoyote yasiende Tanzania
Kugomea bajeti haimaanishi kwamba watu wanapinga “maendeleo ya aina yoyote”. Acha upotoshaji

Hawa walikuwa wanapinga specific areas kwenye bajeti ambazo either zilikuwa hazina tija au zilikuwa zimekaa kipigaji.
 
Upinzani kote Dunian wanapinga wakiamini mawazo Yao ndio bora

Sasa kama utakuwa unakubali tu mwisho wake unakuwa kama mrema

Wanapinga kwa akiri na sio mataope kama hawa wa kwenu, jambo la kupinga wanapinga, na jambo la marekebisho wanafanya, na lile ambalo halina ubishi aidha wasapoti au wakae kimya. Huo ndio upinzani.
Lakini hawa wenu wao kila kitu wanapinga sasa lipi watasema wamepeleka kwa wananchi wakati yote walipinga?
 
Haha, wewe jamaa unaongea kama sehemu za siri.dah! Sasa hoja gani hizo? Nina uhakika umeongea ukiwa umekaa kwa tako moja kupisha ushuzi.Dah
 
... Kugomea bajeti maana yake ni kupinga maendeleo ya aina yoyote ...
Iwapo una mawazo kama haya kwamba ukipinga bajeti (hata kama ina madudu) basi maana yake unapinga maendeleo, basi unahitaji kukalishwa mahali patulivu uelimishwe kwanza kabla ya ku.publish
 
Back
Top Bottom