Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,445
Dah! Wakuu, mitihani ni mingi jamani hawa wanawake zetu hawa. Niko mbali na home umeme umeisha, bint/slay queen anatuma msg LUKU imeisha.
Yeye kashinda home toka asubuhi yaani anashindwa nunua umeme kweli hadi apige simu. Hivi wadada mbona mko hivi? Ujue mnajidhalilisha? Aisee!
Haya nimenunua umeme sasa kaa uangalie TV hapo sebuleni. Hapa jana tu kaniomba 50k na ana kazi eti utanilipa hela yangu wakati hiyo hela nimempa mimi jana.
Kiukweli nimemwambia sawa nitakupa hela yako, sasa sijui kanunua umeme wa Tsh. ngapi, ngoja nirudi home nione. Aisee! Slay queens mna kazi
Ila wakuu kuishi na mtu ni kibarua kigumu sana, inataka moyo sana. Sina gubu kama baadhi yenu mnavyosemaga nataka kuonyesha tu jinsi gani hawa wenzetu itakua ngumu kufikia maazimio ya Beijing
"Ishini na mademu zenu kwa akili"