Nimemkuta Mheshimiwa Rais Mikumi!

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Rais Jakaya Kikwete ameamua kwenda Mikumi National Park kwa mapumziko. Naambiwa na wahusika kuwa Rais amekuwa ndani ya mbuga hiyo kwa siku kadhaa sasa. Jana mchana nikiwa ndani ya mbuga hiyo nilikutana na msafara wake ( Pichani). Naam. Mh. Rais ameamua kujichanganya na watalii wengine akiwa kwenye gari la wazi la kitalii na nyuma landrover ya FFU. Huko mbugani, kama watalii wengine, naye amehangaika kutafuta simba walipo ndani ya mbuga hiyo. Na juma lijalo atakuwa kule Butiama, huko anatarajiwa kuunguruma na kutoa maamuzi ya kutikisa nchi. Labda Mheshimiwa Rais anahitaji kuutafuta ujasiri wa simba na tembo wa Mikumi katika kuunguruma na kutikisa ardhi! Angalia picha zaidi na soma maoni: http://mjengwa.blogspot.com
 
Sio mbaya kuwepo hapa wa thread hii.
Kunawezekana kukawa na mitizamo miwili tofauti hapa:
  1. Akitembelea mbuga yaweza kuwa hamasa kwa watz, ila pia anahitaji kupumzika (si watu wanamwita Vasco Da Gama akienda nje?)
  2. Kwamba anaacha kushughulikia matatizo ya msingi ndani ya nchi yake na kwenda 'kutanua' mbugani. Yapo mengi yanayohitaji utashi na maamuzi yake.
All in all, JK is normal human being, anahitaji mapumziko.
 
....ni habari hii pia..ni rais wetu...but all in all rais wetu amezidi kupenda mapumziko ..nafikiri kila mwezi anajipa ka off...inabidi kaka pinda afanye kazi sana kama msimamizi wa serikali..maana rais wetu hata kabla tulijua anapenda raha zake[mtoa hoja hajatuambia kama amemuona ameambatana na mama au kama kawaida akiwa off yupo single and available...maana mama juzi alikuwa lindi......

mwaka huu pekee ameshapuymzika mwanza,serengeti,arusha..na bado mapumziko ya easther inaonekana ameyaanza mapema sana......

lakini pia its a good gesture kukuza utalii wa ndani!!
 
Rais Jakaya Kikwete ameamua kwenda Mikumi National Park kwa mapumziko. Naambiwa na wahusika kuwa Rais amekuwa ndani ya mbuga hiyo kwa siku kadhaa sasa. Jana mchana nikiwa ndani ya mbuga hiyo nilikutana na msafara wake ( Pichani). Naam. Mh. Rais ameamua kujichanganya na watalii wengine akiwa kwenye gari la wazi la kitalii na nyuma landrover ya FFU. Huko mbugani, kama watalii wengine, naye amehangaika kutafuta simba walipo ndani ya mbuga hiyo. Na juma lijalo atakuwa kule Butiama, huko anatarajiwa kuunguruma na kutoa maamuzi ya kutikisa nchi. Labda Mheshimiwa Rais anahitaji kuutafuta ujasiri wa simba na tembo wa Mikumi katika kuunguruma na kutikisa ardhi! Angalia picha zaidi na soma maoni: http://mjengwa.blogspot.com

Asante Maggid kwa hii story,

Unajua juzi wakati Tanesco inatangaza kuwa bei ya umeme itapanda kwa asilimia mia mbili nilijiuliza hili swali kuwa hivi Kikwete yupo wapi? Nyakati kama hizi ndipo maraisi wa nchi huja kutoa matamko na kuwatuliza wananchi kuwa mambo yatakuwa ok.

Nimesubiri kwa siku kadhaa na kuona kimya.. kumbe Mkwere yuko Mikumi anaenjoy maisha kama hana akili? Huyu Kikwete jamani hata roho huna? Watanzania wanaumia kwa bei za umeme wewe uko Mikumi unakula vekesheni zako kama kawa!?!?!??!?

Shame on you Kikwete! muogope MUNGU maana unakoipeleka hii nchi ni kubaya kuliko hata kuzimu kwenyewe. Shame on you!
 
Jamani Raisi ni binadamu kama sisi tu na habari kama hii ina umuhimu wake,its always good to know Rais alipo na kile anachokifanya, asante Maggid kwa kutujulisha. Mbona wenzetu mlioko bongo mnakula shushu from friday to monday na hamuoni kuwa hili ni tatizo? Hata hivyo naamini Raisi yupo kazini wakati wowote, hata kama ni personal holiday, his job is all about giving instructions and decision making and we all know how that can be done haswa ukizingatia jinsi technology ilivyokua kwa sasa.
 
...mambo mengine's all about Positive Mental attitude. Si (Watanzania) tunataka kukuza Utalii?

PRESIDENT OF TANZANIA H.E. JAKAYA MRISHO KIKWETE NAMED HONORARY GLOBAL CHAIR OF 2ND WORLD TOURISM MARKETING SUMMIT Beijing, China, October 28-30, 2007
August 3, 2007 in Events

(Forimmediaterelease.net) (August 3, 2007–Vancouver, Canada) – The President of the United Republic of Tanzania, H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, was named Honorary Global Chair of the 2nd World Tourism Marketing Summit(WTMS), which will take place in Beijing, China, October 28-30, 2007. The announcement was made by Sujit Chowdhury, Secretary General, of the Canada-based World Trade University(WTU), organizer of the Summit. The Summit, hosted by the Beijing Tourism Administration of the People's Republic of China, will bring together more than 400 travel and tourism industry leaders from around the globe

...hii nayo imetulia, it's all about PROMOTION kwa vitendo!

Kikwete to grace Arusha tourism meet in May

2008-03-05 09:12:26
By Judica Tarimo

President Jakaya Kikwete is set to grace an international tourism meeting expected to attract high-profile foreign personalities scheduled for Arusha in May, this year.

The forum, planned to take place at the Arusha International Conference Centre, paves way for extensive exposure of the country`s vast tourism potentials and attractions.

Big Up Mr Prez!...
 
....ni habari hii pia..ni rais wetu...but all in all rais wetu amezidi kupenda mapumziko ..nafikiri kila mwezi anajipa ka off...inabidi kaka pinda afanye kazi sana kama msimamizi wa serikali..maana rais wetu hata kabla tulijua anapenda raha zake[mtoa hoja hajatuambia kama amemuona ameambatana na mama au kama kawaida akiwa off yupo single and available...maana mama juzi alikuwa lindi......

mwaka huu pekee ameshapuymzika mwanza,serengeti,arusha..na bado mapumziko ya easther inaonekana ameyaanza mapema sana......

lakini pia its a good gesture kukuza utalii wa ndani!!

PM,

Kikwete ameamua kutumia solution ya Kichaka... kukiwa na tatizo nchini, kaa kimya usiliongelee ukitegemea kuwa litakwisha lenyewe. Tatizo la umeme ni kubwa sana na watu wanaumia ila JK ndio hivyo yeye anakula vekesheni na kukaa kimya tu.

Unajua Kichaka hapa marekani ndio amechukua vekesheni kuliko raisi yoyote wa marekani (according to the news). Inaonekana JK anafanya kila kitu anachofanya Kichaka na wanaoumia ni wale wanaotumia zaidi ya nusu ya mapato yao kulipia umeme na usafiri.

shame on you JK! unawezaje kulala wakati wananchi wako wanaumia?
 
akiwa mikumi then??????ulitaka je kupungua hewa iringa,,
na kama ina umuhimu mbona kwenye blog yako umeshindwa
kuiweka au huku kuna vilaza wengi wa kushabikia
unyoronyoro kijana koma tena usirudie mwache ajipumzzishe tena
yuko na mwenzake mwingine nani sijui labda anaweza kuwa dada yako uliza hapo vizuri,,,,,,,,,,,,
pasaka njema
 
akiwa mikumi then??????ulitaka je kupungua hewa iringa,,
na kama ina umuhimu mbona kwenye blog yako umeshindwa
kuiweka au huku kuna vilaza wengi wa kushabikia
unyoronyoro kijana koma tena usirudie mwache ajipumzzishe tena
yuko na mwenzake mwingine nani sijui labda anaweza kuwa dada yako uliza hapo vizuri,,,,,,,,,,,,
pasaka njema

...Samahani, lakini mbona sioni kosa la ndugu Mjengwa kuweka habari yake hapa? Naomba kuuliza, je, unaugonvi binafsi na bwana Mjengwa?!
 
akiwa mikumi then??????ulitaka je kupungua hewa iringa,,
na kama ina umuhimu mbona kwenye blog yako umeshindwa
kuiweka au huku kuna vilaza wengi wa kushabikia
unyoronyoro kijana koma tena usirudie mwache ajipumzzishe tena
yuko na mwenzake mwingine nani sijui labda anaweza kuwa dada yako uliza hapo vizuri,,,,,,,,,,,,
pasaka njema

lugha chafu ya nini tena...... ?
 
Asante Maggid kwa hii story,

Unajua juzi wakati Tanesco inatangaza kuwa bei ya umeme itapanda kwa asilimia mia mbili nilijiuliza hili swali kuwa hivi Kikwete yupo wapi? Nyakati kama hizi ndipo maraisi wa nchi huja kutoa matamko na kuwatuliza wananchi kuwa mambo yatakuwa ok.

Nimesubiri kwa siku kadhaa na kuona kimya.. kumbe Mkwere yuko Mikumi anaenjoy maisha kama hana akili? Huyu Kikwete jamani hata roho huna? Watanzania wanaumia kwa bei za umeme wewe uko Mikumi unakula vekesheni zako kama kawa!?!?!??!?

Shame on you Kikwete! muogope MUNGU maana unakoipeleka hii nchi ni kubaya kuliko hata kuzimu kwenyewe. Shame on you!

Sasa hivi bei yetu ya umeme katika Afrika ya mashariki na kati kama sikosei ndiyo ya juu kuliko nchi nyingine yeyote. Wakiongeza hiyo asilimia mia mbili ndio utakuwa haushikiki kabisa na labda umeme wetu ndio utakuwa wa bei kubwa duniani kuliko nchi nyingine yeyote. Athari yake itakuwa viwanda vingi vitafunga virago kwenda 'kuwekeza' kwenye nchi ambazo umeme ni bei poa ukilinganisha na wa Tanzania.

Miti ndiyo itazidi kukatwa ili kutengenezea mkaa na kuifanya Tanzania iongeze speed kubwa sana kuelekea kuwa jangwa. Watanzania wengi kutokana na mishahara duni umeme hawataweza kuumudu basi watarudi katika maisha ya mwaka 47 ya kutumia mishumaa, vibatari au chemli. Sijui maisha bora aliyoyaahidi Muungwana yako wapi, labda alitaka kusema maisha magumu kwa kila Mtanzania.

Halafu bado wakisafiri nchi za nje wanawaambia Watanzania walio nje warudi nyumbani maana sirikali inaboresha hali ya maisha ili warudi na pia 'wawekeze' Tanzania. Nani anataka kurudi kuja kuishi maisha ya mwaka 47! Kama kuna Watanzania waliokuwa wanafikiria kufungasha na kurudi Tanzania, basi asilimia kubwa watakuwa wamebadilisha mawazo yao
 
kujilusha Bilicanas?! hatakuwa ameanza leo. Uliza upewe nyeti za Kikwete kila mara akija marekani ndio utagundua kuwa kwenda Bilicanas ni cha mtoto!

Hivi Rais wa nchi kwenda kujirusha kaa bwana mdogo wa miaka 25 ni jambo la kujivunia?

Tulicheza naye disco MH huyu pale Tazara, watoto wadogo walipolivamia wengine tulijihuzuru, mwenzetu Kikwete ambaye kwa umri ni braza etu bado anajirusha?
 
Sasa hivi bei yetu ya umeme katika Afrika ya mashariki na kati kama sikosei ndiyo ya juu kuliko nchi nyingine yeyote. Wakiongeza hiyo asilimia mia mbili ndio utakuwa haushikiki kabisa na labda umeme wetu ndio utakuwa wa bei kubwa duniani kuliko nchi nyingine yeyote. Athari yake itakuwa viwanda vingi vitafunga virago kwenda 'kuwekeza' kwenye nchi ambazo umeme ni bei poa ukilinganisha na wa Tanzania.

Miti ndiyo itazidi kukatwa ili kutengenezea mkaa na kuifanya Tanzania iongeze speed kubwa sana kuelekea kuwa jangwa. Watanzania wengi kutokana na mishahara duni umeme hawataweza kuumudu basi watarudi katika maisha ya mwaka 47 ya kutumia mishumaa, vibatari au chemli. Sijui maisha bora aliyoyaahidi Muungwana yako wapi, labda alitaka kusema maisha magumu kwa kila Mtanzania.

Halafu bado wakisafiri nchi za nje wanawaambia Watanzania walio nje warudi nyumbani maana sirikali inaboresha hali ya maisha ili warudi na pia 'wawekeze' Tanzania. Nani anataka kurudi kuja kuishi maisha ya mwaka 47! Kama kuna Watanzania waliokuwa wanafikiria kufungasha na kurudi Tanzania, basi asilimia kubwa watakuwa wamebadilisha mawazo yao

Kuendelea kukaa kimya kwa rais kuhusu suala la umeme ni dalili moja kubwa kwamba kazi tuliyo mpa ya kuongoza nchi imegeuka kuwa zigo zito la kumlemea.

Tumejikaanga kwa mafuta yetu wenyewe.
 
Rais Jakaya Kikwete ameamua kwenda Mikumi National Park kwa mapumziko. Naambiwa na wahusika kuwa Rais amekuwa ndani ya mbuga hiyo kwa siku kadhaa sasa. Jana mchana nikiwa ndani ya mbuga hiyo nilikutana na msafara wake ( Pichani). Naam. Mh. Rais ameamua kujichanganya na watalii wengine akiwa kwenye gari la wazi la kitalii na nyuma landrover ya FFU. Huko mbugani, kama watalii wengine, naye amehangaika kutafuta simba walipo ndani ya mbuga hiyo. Na juma lijalo atakuwa kule Butiama, huko anatarajiwa kuunguruma na kutoa maamuzi ya kutikisa nchi. Labda Mheshimiwa Rais anahitaji kuutafuta ujasiri wa simba na tembo wa Mikumi katika kuunguruma na kutikisa ardhi! Angalia picha zaidi na soma maoni: http://mjengwa.blogspot.com

THANK U MAGGID,KUTUJULISHA,SI VIBAYA SISI KUJUA MR PRESIDENT ALIKO AFTER ALL HE IS MORTAL CREATURE AS U N' ME HAKUNA NOMA ON THAT.NINALOMWOMBA MR PRESIDENT NI HILI:-Kuna tatizo sugu la maji pale mikumi ambalo lilimshinda Lowassa,Makamba, Karembo na wengine. Kuna 200million toka WORLD BANK huenda zimeliwa.Then aulize kuna somebody ZUNDA is very stubborn na huyu ndo hao waheshimiwa wamemshindwa. Naamini mzee kwa kuwa yupo pale akikohoa hakuna litakaloshindikana.
 
Rais akiwa kimya tunasema serikali ina usiri mkubwa tukijulishwa tunasema haina umuhimu na mustakabali wa taifa letu, inabidi akapumzishe kichwa baada ya kupeleka vijana wetu kwenye operation ya kumtoa Bacar madarakani, unafikiria ni decision ndogo hiyo?
 
Back
Top Bottom