Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Hebu tuchukulie kwamba, umeoa, na ndoa yenu ina miaka 6. Katika ndoa yenu mmebahatika kupata mtoto mmoja wa kiume ambaye ndio anatimiza miaka 4. katika kipindi chote cha maisha yenu ya ndoa, mlikuwa mkiishi kwa amani na upendo wa hali ya juu. Kuna wakati mlikuwa mnatofautiana lakini yalikuwa ni mambo madogo ambayo mlikuwa hamyapi uzito.
Lakini ghafla siku moja unarudi kutoka kazini unamkuta mkeo anafungasha mizigo yake akidai anaondoka kwenda kuanza maisha mapya mahali pengine. Unapomdadisi sababu ya kufanya hivyo, anadai kuwa amekuvumila sana kwa miaka yote mliyoishi pamoja na anaanza kutoa mlolongo wa malalamiko chungu mzima akikutuhumu kwa mambo mengi ambayo yalikuwa yanatokea katika kipindi chote cha ndoa yenu lakini kamwe hakuwahi kulalamika zaidi ya kukaa kimya tu. Unapomuuliza, kwa nini hakuwahi kulalamikia hali hiyo, anajibu kwamba alikuwa anaogopa kutofautiana na wewe kwa kuwa wewe ni mbishi sana, una ghubu, mbabe na unajifanya unajua kila kitu.Unajitahidi kumsihi akae ili mzungumzie tofauti zenu na ikiwezekana mmalize na kuanza maisha mapya lakini mwenzio anasisitiza kuwa huo ndio uamuzi wake wa mwisho na hatarajii kubadilisha kwani amevumilia sana lakini sasa ameamua kuondoka ili awe huru na maisha yake.Hebu niambie kama ni wewe ungefanya nini?
Lakini ghafla siku moja unarudi kutoka kazini unamkuta mkeo anafungasha mizigo yake akidai anaondoka kwenda kuanza maisha mapya mahali pengine. Unapomdadisi sababu ya kufanya hivyo, anadai kuwa amekuvumila sana kwa miaka yote mliyoishi pamoja na anaanza kutoa mlolongo wa malalamiko chungu mzima akikutuhumu kwa mambo mengi ambayo yalikuwa yanatokea katika kipindi chote cha ndoa yenu lakini kamwe hakuwahi kulalamika zaidi ya kukaa kimya tu. Unapomuuliza, kwa nini hakuwahi kulalamikia hali hiyo, anajibu kwamba alikuwa anaogopa kutofautiana na wewe kwa kuwa wewe ni mbishi sana, una ghubu, mbabe na unajifanya unajua kila kitu.Unajitahidi kumsihi akae ili mzungumzie tofauti zenu na ikiwezekana mmalize na kuanza maisha mapya lakini mwenzio anasisitiza kuwa huo ndio uamuzi wake wa mwisho na hatarajii kubadilisha kwani amevumilia sana lakini sasa ameamua kuondoka ili awe huru na maisha yake.Hebu niambie kama ni wewe ungefanya nini?