Nimemkumbuka Ex wangu

Nebuchadinezzer

JF-Expert Member
Oct 1, 2018
1,403
2,545
Habari zenu humu ndani.
Mwenzenu leo sina furaha sana maana akili yangu yote inamuwaza Hajir mpenzi wangu tuliyeachana nae kama miezi zaidi ya minne sasa.

Sema ukweli nilikuwa nampenda sana Hajir wangu. Tangu tuachane nimejaribu kuingia kwenye mahusiano mapya kama mara tatu hivi lakini wapi, sipati furaha kama niliyokuwa nayo nilipokuwa na Hajir.

Nakumbuka tulipoachana nilifuta namba yake ili nikate mawasiliano naye kabisa. Hili halikusaidia maana namba take imo kichwani mwangu.

Anyway, kama yumo humu naomba anisamehe kwa niliyomtendea anisamehe tuishi kama zamani. Niliyokufanyia ilikuwa ni hasira tu Hajir mpenzi wangu. Nakupenda sana.
 
Aalaaaaahhh mweeeeehh huu uzi nilijua ni wa mtoto wa kike.. kumbe dume zima
 
Back
Top Bottom