Nimemisi ziara za kushitukiza za Rais; zimeishia wapi?

Kwa mwenye uwezo wa kufikiria zile ziara zilikuwa mahususi kwa ajili ya kuset pace na agenda ya serikali ya tano. Ila sababu wengi hamuwezi kungamua logic ndogo kama hiyo. Hivi wewe kwa akili yako unadhani Raisi angeweza kwenda kila mahali?

Unaposema wengi unamaanisha akina nani??? By the way hao wengi unao sema hawajui kung'amua mambo na wewe usijua kuandika maneno ya kiswahili ni nani bora????

Huwezi kuandika hata neno "kung'amua" huwezi kuandika hata neno rahisi kabisa la kiswahili "Rais"!!! Sasa wewe na hao ni nani anauwezo mdogo wa kung'amua mambo??
 
Hata mimi nimezimiss...siku hizi hata taarifa za habari hatuangalii.
Hakuna jipya zaidi ya Makonda na Sapi kujitutumua.
Habari ya mjini ni UKUTAAAAA
 
Hata mimi nimezimiss...siku hizi hata taarifa za habari hatuangalii.
Hakuna jipya zaidi ya Makonda na Sapi kujitutumua.
Habari ya mjini ni UKUTAAAAA

Hata mim taarifa ya Habari siangalii tena, mana hakuna jipya zaidi ya matamko tu afu kesho kumbe ni utani.
 
Huwezi endesha mambo kwa kutumia akili za kima Barbarosa, wakudadavua,mudawote,lizaboni,msemaji ukweli na aina hii ya manyumbu alafu ukategemea utafika mbali. Ashagota anasikiliza ushauri toka kwa yeyote sasa hivi mshauri wake mkuu ni Barbarosa
 
Watu ''walivyomchoka'' kwa kutumia kigezo cha hisia zako.

Una haki ya kutumia kigezo cha hisia zako kama ilivyo haki ya kuendelea kuwa mjinga.

Hata wajinga wana haki ya kuamua kuwa wajinga pamoja na kwamba ujinga ni mzigo kwa taifa!
20160807_055451.jpg
 
Kuna wawekezaji wa viwanda wamekuja na jana walienda kumwona mkuu, waliweka wazi kuwa kiwanda kitaanza kazi AFTER 40 YEARS jamani ninyi ten months tu mmechoka! Lets wait angalau ipite 39 years then Tz ya viwanda itakuja
hicho kiwanda kinafyatua watu au
 
Kwa mwenye uwezo wa kufikiria zile ziara zilikuwa mahususi kwa ajili ya kuset pace na agenda ya serikali ya tano. Ila sababu wengi hamuwezi kungamua logic ndogo kama hiyo. Hivi wewe kwa akili yako unadhani Raisi angeweza kwenda kila mahali?
Kama haiwezekani kwenda kila mahali kwa nini alikwenda mahali fulani. Kigezo cha kwenda alikokwenda na si huko ambako hakwenda kilikuwa ni nini? Jee wale waliofikwa na ziara hizo na matamko kutolewa si watahisi kuwa walikuwa wameonewa?
 
Nifah Mbona unamtafutia maneno mwenzio Mlaleo Wenzio tumesoma tumepita kimya kimya wewe mpaka umelizia kabisa. Wengi tu mate yamewajaa midomoni mwao wanatafuta pa kwenda kuyatemea!!
 
Huwezi endesha mambo kwa kutumia akili za kima Barbarosa, wakudadavua,mudawote,lizaboni,msemaji ukweli na aina hii ya manyumbu alafu ukategemea utafika mbali. Ashagota anasikiliza ushauri toka kwa yeyote sasa hivi mshauri wake mkuu ni Barbarosa
Kiukweli ushauri wa wana Lumumba ni unafiki na kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa, ndo wanaomdaganya avunje katiba ili kuvunja democrasia huku akisahau aman ya nchi. Akiendelea kusikiliza ushauri wa vichwa vya mwendokasi a.k.a villlaza wa Lumumba nchi itamharibikia mkononi mwake.
 
Nmekaa muda mrefu sijamsikia kwenye vyombo vya habari au kumsoma.
1.Ameshamaliza kufukuza mafisadi wote alioesema atawashughulikia? Je sasa tunaweza pumzika kuwa mafisadi wameisha nchini?
2. Ameshamaliza keri zote zilizokuwepo ndani ya miaka 10 iliyopita?
3. Anajiandaa kutoa tamko gani tena?baada ya kushauri watu wawe wanafyatuka tu?
4. Yupo kweli nchini au ameamua kusafiri kwa kushtukiza kwenda nchini flan?
5. Kwa sasa anamkakati gani au anawaza tena atoke vipi?anaandaa album au single gan kwa sisi wapenda muziki?

Tumekaa mkao wa kula.tunasubiri kusikia ataibuka na jambo gani.watu wake tuna kiu kubwa ya kumwona na kumsikia akifyatua maneno mbalimbali na matamko dhabiti kabisa ya kikakamavu.
 
Back
Top Bottom