Nimemfumania mume wangu PR Hotel sikia haya

Stream line

JF-Expert Member
Apr 22, 2015
393
239
Baada ya kumfumania mme wangu tarehe 8 Nov 16 PR Hotel uwanja wa taifa na tarehe 12 Nov The Target; nilifanikiwa kumrekodi kwa simu bila yeye kujua akimwambia dada yake kuwa mimi namwekea boda boda kumfuatilia na alipokuwa hotelini nilimkuta akinywa pombe, pia watoto nilionao si watoto wake;

Lakini tarehe 13 Nov nilimrekodi tena akimwambia rafiki yake kuwa nilimfumania hotelini na akakimbia kupitia mlango wa nyuma akaenda mbele kunywa pombe nyingi, Mwanamke ninaye mkuta naye ni mama wa kisukuma kwa jina mama samson.

Ambaye tarehe 26 Nov alimtumia kama mama wa mtoto wake wa nje kwenye arusi ya bintiye wa nje ya ndoa. ingawa mama wa bibi arusi alikuwepo arusini. mimi harusini sikuruhusiwa kwenda.

Kinachonishangaza huyu mama ana umri mkubwa kumpita hata mme wangu. nimemrekodi mara nyingi akimwambia mme wangu kuwa mimi nina waganga watatu wa kienyeji na nimempa mzee wangu limbwata. imefikia sasa nimerekodi anamwambia mzee wangu kuwa mimi ni malaya.

Ushauri tafadhali.
1. nifanye nini na mme huyu niliyekaa naye ktk ndoa kwa miaka 25 na sasa anakaribia kustaafu?
2. Suala la kwamba watoto si wa kwake?
3. Nifanye nini na mama huyu?

Nakaribisha pia PM -Private

EDITED on 15/12/2016.

Nimeongea na wanasheria na wamenishauri kama mzee hawatunzi nidai DNA Test. Ukweli mitoto yote inafanana naye mno. hiyo dna ni kupoteza pesa kwani wanatunzwa

Upande wa mama huyu sijapata ushauri wa kuniridhisha bado.

Juu ya mzee mwenzangu nimepata ushauri mzuri sana nawashukuru nyote.

Ila clip zangu zilikuwa ktk lugha ya kinyakyusa na wachangiaji wangu wa mwanzo akina Ibwe ni wanyakyusa. majibu yao yamo humu, wasomaji wangu mmeiona tabia ya wanaume wa huko nilikoolewa.

Kilichopelekea mimi kumfuatilia kwa kipindi cha mwezi mmoja ni tabia yake ya kurudi nyumbani saa nane za usiku tena bila kulewa na asiulizwe chochote. la sivyo unapata kipigo cha mbwa. Tabia niliyoivumilia hadi sasa watoto wamekua. nikaona ni vema nijue kulikoni. huyo mama ilikuwa bahati mbaya tu kwake. kwani...

Tutaonana nitakapopata mda na kuweka clip za kiswahili mzee alipokuwa anatongoza married WOMEN from a office. within a period of a month akisaidiwa na madereva wa ofisini.
Binafsi huwa sina rafiki kwani alishapitia wote na nimekata tamaa ya urafiki.
 
Miaka 25 ya ndoa ina maana huyo mwanaume ni mtu mzima around 55yrs old hv (nimekadiria alioa akiwa 30yrs), najua mmepitia mengi sana katika ndoa yakimwemo milima na mabonde..

Hebu kaa chini na mumeo mweleze ukweli, kumbuka hakuna atakayewezaz kuwasuluhisha ikiwa ninyi hamko tayari.. Siwezi kushauri kuvunja ndoa kwani sio suluhu hata kidogo. Hebu mkae chini mjadiliane wawili mweleze black and white..
 
-Zile tafiti za sensa naona kama vile zipo sawa....yaani wanawake ni wengi kuliko wanaume Tanzania.. wastani ni mume mmoja kwa wanawake wanne....
-Sasa wewe ukimng'ang'aniza mmeo awe na wewe tu wengine (3) nani atawahudimia.??

-PLEASE!! wakinadada mpendane na ku-share raha za duniani pamoja....

NOTE :-MUDA MWINGINE NAPENDA UPUUZI...
 
punguza kumfatilia...relax usisahau thamani yako..kikubwa muombe sana MUNGU
Huyu sio mke mwema hata kidogo...ila sababu huyo Mme wako ni home boy kutoka Mbeya...najua utapata unachokitafuta mama lugano.

....huwaga hatupendagi ujinga wa hivyo
 
Stream line said:
Baada ya kumfumania mme wangu tarehe 8 Nov 16 PR Hotel uwanja wa taifa na tarehe 12 Nov The Target; nilifanikiwa kumrekodi kwa simu bila yeye kujua akimwambia dada yake kuwa mimi namwekea boda boda kumfuatilia na alipokuwa hotelini nilimkuta akinywa pombe, pia watoto nilionao si watoto wake; lakini tarehe 13 Nov nilimrekodi tena akimwambia rafiki yake kuwa nilimfumania hotelini na akakimbia kupitia mlango wa nyuma akaenda mbele kunywa pombe nyingi, Mwanamke ninaye mkuta naye ni mama wa kisukuma kwa jina mama samson. Ambaye tarehe 26 Nov alimtumia kama mama wa mtoto wake wa nje kwenye arusi ya bintiye wa nje ya ndoa. ingawa mama wa bibi arusi alikuwepo arusini. mimi harusini sikuruhusiwa kwenda.
kinachonishangaza huyu mama ana umri mkubwa kumpita hata mme wangu. nimemrekodi mara nyingi akimwambia mme wangu kuwa mimi nina waganga watatu wa kienyeji na nimempa mzee wangu limbwata. imefikia sasa nimerekodi anamwambia mzee wangu kuwa mimi ni malaya.
Ushauri tafadhali.
1. nifanye nini na mme huyu niliyekaa naye ktk ndoa kwa miaka 25 na sasa anakaribia kustaafu?
2. Suala la kwamba watoto si wa kwake?
3. Nifanye nini na mama huyu?
Nakaribisha pia PM -Private Messages
ilkusikiliza clips hizi tumia earphones.
Baba Lugano yuko sawa....thats how we do.
Banyambala hatutaki ujinga kama huo unaofanya wa kumfanyia mitego ya kijinga
 
mamangu ungetulia haya mambo ukayamaliza chinichini tu kunawakati hapa sio mahala sahihi pakupata suluhu zaidi unaweza kuwa unajichafua tu,kwa umri wa ndoa nikipimo tosha cha kukabiliana na haya makwazo tafuta rafiki wakaribu mnae peana siri zenu au dungu mnaeshibana mweleze utoe kinyongo chako katikati ya ushauri wake utapata njia sahihi ya kwako mwenyewe yakumaliza hilo jambo!!
kumbuka wamtumainio bwana ni kama mlima sayuni
 
Miaka 25 ya ndoa ina maana huyo mwanaume ni mtu mzima around 55yrs old hv (nimekadiria alioa akiwa 30yrs), najua mmepitia mengi sana katika ndoa yakimwemo milima na mabonde..

Hebu kaa chini na mumeo mweleze ukweli, kumbuka hakuna atakayewezaz kuwasuluhisha ikiwa ninyi hamko tayari.. Siwezi kushauri kuvunja ndoa kwani sio suluhu hata kidogo. Hebu mkae chini mjadiliane wawili mweleze black and white..

asante kwa hili.
 
Miaka 25 ya ndoa ina maana huyo mwanaume ni mtu mzima around 55yrs old hv (nimekadiria alioa akiwa 30yrs), najua mmepitia mengi sana katika ndoa yakimwemo milima na mabonde..

Hebu kaa chini na mumeo mweleze ukweli, kumbuka hakuna atakayewezaz kuwasuluhisha ikiwa ninyi hamko tayari.. Siwezi kushauri kuvunja ndoa kwani sio suluhu hata kidogo. Hebu mkae chini mjadiliane wawili mweleze black and white..
The best advice n very positive one!
 
Mh! hapa umeeleza tatizo, ila umeficha kuonesha chanzo. yote hayo yanatokea kuna sababu. umekaa ktk ndoa kwa muda mrefu zaidi yangu kwa miaka 16 mie nina miaka 9 tu ya ndoa. nipe tatizo kwa ufupi inbox(kama ni siri), nikushauri kulingana na ukubwa wa tatizo na chanzo, mwanaume wa umri huo hawezi kuwa hivyo. kati yako na mama samson kuna tatizo pia, nijulishe private tafadhali, hapa umejipendelea sana kuleta hbr nusu yenye taarifa yenye kukupendelea tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom