CIC malema
Member
- Apr 23, 2021
- 10
- 29
Mimi ni kijana/mwanaume ninayeishi na VVU kwa muda mrefu sasa hivi nimekua nina mahusiano na binti asiye na maambukizi na kwa sasa kwa hakika ninashuhudia mapenzi ya dhati katika historia ya maisha yangu.
Changamoto; kwa muda amekuwa akitaka mimi na yeye tukutane kimwili nikawa namtolea nje sasa nahisi imefika hatua ataanza kuhisi mimi sina uwezo wa jogoo kupanda mtungi, shida ni kwamba hajui hali yangu ilivyo na kukutana nae faragha ni kitu ambacho kwangu sioni tatizo kwa sababu tunaweza tumia kinga.
Lakini kinachonipa mawazo ni kwamba yeye anasema hapendi kutumia kondomu kwa sababu zinapunguza ladha na Mimi moyo wangu na akili yangu vinasita sana naogopa sana kumuambukiza na TUNAPENDANA SANA.
NIFANYE NINI KWENYE HIKI KISANGA?
Changamoto; kwa muda amekuwa akitaka mimi na yeye tukutane kimwili nikawa namtolea nje sasa nahisi imefika hatua ataanza kuhisi mimi sina uwezo wa jogoo kupanda mtungi, shida ni kwamba hajui hali yangu ilivyo na kukutana nae faragha ni kitu ambacho kwangu sioni tatizo kwa sababu tunaweza tumia kinga.
Lakini kinachonipa mawazo ni kwamba yeye anasema hapendi kutumia kondomu kwa sababu zinapunguza ladha na Mimi moyo wangu na akili yangu vinasita sana naogopa sana kumuambukiza na TUNAPENDANA SANA.
NIFANYE NINI KWENYE HIKI KISANGA?