Nimekutana na mwanamke wa ajabu, naanza kuingiwa na hofu walimwengu nisaidieni

Ingekuwa huyo jini ana uwezo wa kuingikia mawasiliano ya kupitia teknonoljia ya kisasa kama simu basi angekuja kumtisha jamaa hata hapa kweye JF, wote tinaosoma uzi tungetumiwa ujumbe sijui PM kwamba wewe fulani na wote kwenye jukwaa la JF minajisumbua. Ingekuwa kama mlivyotishwa kwenye simu ktk kisa cha huyo jamaa yako.

Tena jini libgetutaja kwa majina yetu halisi kuonesha linajua kola kitu hatuwezi kilikwepa.
JF imezindikwa mkuu,hawezi kuiingia kifalafala namna hiyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baba hiyo ni Live na siku nikiwa ofisin sina hata hela ya lunch ghafla Tigopesa inasoma..yani mbwa hawa wanajua kila kitu, mkibishana kwenye sms au ukimletea jeuri siku nzima inaharibika..hata ukiwa bar nilikua nahisi napigwa viwembe na kunyolewa nywele yani nakua uncomfortable mpaka naacha kunywa pombe, kumwambia mtu siwezi yani aarrghhh zile heka heka hapana kwakweli mpaka nikiwa club namuhisi basi naanza kumtukana kwamba flani acha mambo ya kis** nge maana sometimes unahisi **** inashikwa livee!
Yechu yechu ati nini inashikwa live
 
Relax..na atakufanya marafiki wote wakukimbie, time will tell..na hata ukimblock atatumia namba nyingine..mungu akulinde, amenisababishia at this age 28 sitaki mwanamke yeyote nahisi kama nae atakua wale wale tu
Bro hii kitu rahisi sana.. kimbilia kanisani. Nenda ecg church makongo au efatha... hutokosa msaada wasimulie. Na pia waombe wakipe sala za rehema na za damu ya yesu. Sali kila siku
 
Kama huamini usilazimishe na wengine wasiamini.
Hata mambo yapoo.Ila kwa kuwa Wewe bado kukukuta Ndo mana.
Ila subiri ikitoka kwa huyo Kaka zamu yako mana anakusoma .Wana uwezo wa kuona hata anayebishabisha kwenye huu Uzi.
Hii chai unaweza dhani ni kweli ,maana mleta maada ana I'd mbili kwahy anajijibu yy mwenywe kukoleza sukari chai iwe tamu!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeskia mara nyingiz izi simulizi.
Ukimtegemea MUngu haya yote yatapita.
Sala ni muhimu vijana.
 
Samahani ndugu yetu.Acha kabisa no.ya simu kwa MTU unayemwamini kidogo hapa Jf ili tusipokuwa tunakuona tena hapa upatiwe msaada.
Halo huyo usiichukulie kirahisi.
Wapo hapa watu wa kusaidia nasikoa Mshana Jr sijui au Daby wanaweza kutafuta suluhisho
Kuna vitu vinashahabiana...niombeeni kesho niwe vyema...niweze kuendelea. Nitakuwa chizi Sasa hv. Nina was was muda wote

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekuelewa.

Nna ndugu yangu pia hapati madhara ya wachawi mashamba ya waganga na wachawi anaiba tu vijiweni zikija stori za kichawi anawatukana kabsaa na kuwataka wamloge.
Mwambie nenda sumbawanga kaibe kwa mtu mwenye uchawi alafu akirudi salama uje utuhabarishe.

Kuna vijana watu walikwenda kuiba miwa kwa babu fulani wakajua hakuna shida, baada ya siku mbili kupita babu akatangaza walioiba waende wakamuombe samahani lakini hawakwenda.

Siku 5 zilipita baada ya lile tangazo kisha akatoa nafasi ya mwisho na akasema asije akalaumiwa lakini bado hawakwenda.

Baada ya wiki kuisha tangu wizi utokee mmoja wa wale vijana alidonolewa mguuni na kuku aliyetotoa vifaranga kisha mguu ukaanza kuoza ikabidi ukakatwe na hadi leo ni kilema napo alipona baada ya kwenda kumuomba msamaha mzee wa watu.

Kijana mwingine alipata ugonjwa,macho yalivimba hadi yakatoka nje na yakawa yanatoa maji. Alikwenda kufanyiwa upasuaji wa macho lakini hakuchukua muda akafa.

Watatu alikua ni binti kati ya miaka 18-20 yeye yeye inasemekana alikula tu lakini hakubeba miwa kwenda nayo popote lakini aliugua ugonjwa wa ajabu kama mtu mwenye polio.

Mwili wake ulikonda sio kawaida, mguu mmoja ulikua mwembamba kama fimbo kuanzia paja hadi karibu na unyayo pote palikua sawa na mguu mmoja ulikua kama mwenye matende na alikua akikojoa mkojo sisimizi wanajaa muda huo huo mahali alipokojoa.

Ndugu wakampeleka hospitali kubwa wakampima magonjwa yote hadi kisukari lakini hawakuona kitu. Baadaye wakaenda kwa waganga na mganga akawaambia hana uwezo wa kutibu labda aende alikofanya wizi kwa mzee fulani (akataja jina) ndio akaombe samahani ndipo atapona.

Basi wakaenda kwa yule babu wakaomba samahani na babu akawaeleza kuwa wamechelewa hawezi lakini atajaribu, binti alipigwa kofi zito na kuambiwa toka hapa na ukome kuiba kisha akawaeleza nendeni. Usiku bimti alikua akitokwa jasho sana na baada siku tatu mwili ukaanza kurudi hadi akapona kabisa.

FANYA JEURI USIKUTANE NA KONKODI UTAKUA SALAMA LAKINI UKIKUTANA NA CHAWI HALISI UMEKWISHA.

Karibu Sumbawanga haurogwi bila kupewa nafasi ya kujitetea.
Jeuri zako ndio kaburi lako, unaambiwa ukaombe samahani na ukienda hana shida tena na wewe lakini ukidharau wanatuma makombora ya Atomic popote yanakufikia hata uwe nje ya nchi

Mkorintho wa 6
 
Back
Top Bottom