Nimekutana na mwanamke wa ajabu, naanza kuingiwa na hofu walimwengu nisaidieni

puker

JF-Expert Member
Nov 22, 2018
940
1,847
Habar zenu wadau

Naomba mnisaidie maana nipo njia panda sielewi nifanye nini. Waswahili wanasema mficha maradhi Kifo humuumbua.

Mimi sitaki kusubiri Kifo kinikute. Ileweke nimekuwa humu JF kwa muda mrefu, Mara nyingi nimekuwa msomaji tu, wa matukio ya watu, pamoja na kujielimisha, Mara chache sana nimekuwa nikichangia mijadala pale inapobidi. Hii ndio thread yangu ya kwanza. Hivyo sijaandika kwa ajili ya kuburudisha/kumtisha mtu, ninachokiwasilisha hapa Ni ukweli mtupu. Lengo na madhumuni Ni kupata ushauri na msaada pale inapobidi.

***** ****** ******** ******** ******
Iko hv, Mimi Ni mfanya biashara mdogo ninaejishughulisha na uuzaji wa nguo za kiume katika sehemu Fulani hv hp jijini DSM. Kiufupi Nina maduka mawili ya nguo za kiume, hiyo ndio ajira yangu inayonifanya niishi hapa mjini. Sasa mnamo Tar 27 Dec ya mwaka Jana (2018)nipo ktk moja ya ofisi yangu na endelea na majukumu yangu ya kawaida, tena nakumbuka ilikuwa siku ya alhamisi mida ya Kama saa 7 mchana kuelekea saa 8 hv, alikuwa mteja ambae Ni mwanamke ( Alikuwa mrembo sana, mweupe Ana asili Kama ya kiarabu hv) ila rafudhi Ni yakipemba.

Kama kawaida nikawa namsikiliza, akaniambia nimchagulie nguo nzuri anataka ampelekee mme wake, Yani shati na suruali. Wakati naendelea kumchagulia nikawa namuuliza anavaa size gani? Akacheka akasema yupo Kama wewe, kwa kila kitu. Tena akaongeza na kusema nguo nitakazo zipenda Mimi hata yy atazipenda.

Nikawa namtania, nikamwambia kwa jinsi ulivyomzur hvy nataman mume wako niwe Mimi, akaniuliza Kweli? Nikamwambia hakuna mwanaume chini ya jua anaweza kukukataa msichana mrembo Kama wote tukacheka.
Zoezi la kuchagua nguo likaendelea tukafanikiwa kupata nzuri akazipenda. Tumezoea wabongo tunapenda discount, lkn kwake ilikuwa ni tofauti, akauliza nikiasi gani alipe, nikamwambia akalipia bila kuomba punguzo la Bei Kama tulivyozoea kwa wateja walio wengi. Wateja wa namna hii hutokea ila ni marachache sana, hvy nilifurah maana inakuwaga bingo unapata faida nzur.

Nikiwa namfungia hz nguo, aliniuliza...umeoa? Nikamwambia hapana akacheka akasema, nilijua tu...huwez kuoa mapema 7bu unapenda pombe na wanawake wa aina tofauti tofauti, kifupi we Ni mzinifu. Hii ya pombe ilinistua kidogo, amejuaje mm nakunywa pombe, ila sikutaka kumuonesha hadharani.

Akaniambia, Kuna sehemu anaenda hvy akirudi atauputia mzigo wake, ila nimuhifadhie, akaniuliza huwa nafunga saa ngapi? Nikamwambia, akaniomba namba ya simu Kama sitojali nimpe ili Kama atachelewa anijulishe nisije chelewa kufunga kwa 7bu yake. Nami sikuona Tatizo, kwanza Ni mteja lakini pia Ni mrembo sana Kama tunavyojijua sisi wanaume, basi nikampa namba, akaaga na kuondoka.

************

Hapo ndipo kizazaa kilipoanza. Hata hapa naandika thread hii, Sina amani kabisa. Kufika mida ya Kama saa mbili na robo usiku, sms ikaingia kwenye simu yangu.inasema "Zawadi niliyo kununulia umeipenda"? Mmmh, mm nikahisi itakuwa mtu kakosea namba, coz ilitokea namba mpya, baada ya Kama dk 10 hv, ile namba iliyotuma sms ikawa inanipigia, kupokea nasikia sauti ya msichana, akaniuliza...mbona hujajibu sms yangu hau unapenda zawadi yangu, nikamuuliza unajua unaongea na Nan?

Akasema ndio Ni Fulani (akataja jina langu), nikashangaa nikamwambia mbona hakuna mtu nilimwagiza zawadi akasema, Tena umechagua na kuzijaribisha mwenyewe Mara hii umesahau? Akawa anacheka akaniuliza umeshanikumbuka? Nikamwambia ndio...nikamuuliza umejuaje jina langu wakati sikumtajia, (Nilimdanganya jina) Mara nyingi Sina destruri ya kukwambia jina langu la ukweli mtu nisie mjua, Hilo likanishangaza...nikachekecha akili nikahis labda ameangalia kwenye tigo pesa maana nilimpa namba ya tigo, swali lililozidi kuniumiza akili anawezaje kuja dukani kwangu kuninulia nguo Ikiwa hanifahamu, wakat aliniambia Ni za mumewe?

Nikamuuliza si ulisema unampelekea mumeo? Akaniambia kwani wewe hufai kuwa mume wangu? Akiwa anacheka, akaendelea.....na si ulisema hujaoa au ulinidanganya? Nikabaki na kigugumiz nisiamini ninachokisikia, akaniambia nimeamua kukutunuku. Usiku mwema, nitakuja kukutembelea siku nyingine akakata simu. Nikabaki na maswali chungu nzima, kupiga ile namba ikawa haipatikan...baada ya hapo ndio vitimbi vilipoanza.

Itaendelea.......

NB: Nimechoka kuandika nitaendelea kesho ila kiukweli mwezenu nipo njia panda sielew, mwaka nimeanza na mauzauza

Sehemu ya Pili

Baada ya kujaribu kupiga ile simu Mara kadhaa bila mafanikio, wakati huo Nilikuwa nimekaa nje ya duka na machinga (wanaopanga bidhaa chini) tukipiga story mbili tatu, hvy wakati ile simu naongea nayo wote walikuwa wananisikia, walivyoona nimebadilika Sina furaha tena ikabidi waniulize kulikoni? Sikuwa na haja ya kuwaficha nikaweka wazi kila kitu kilivyokua juu ya Lile sakata.

Basi nikaibua mjadala mzito kila mtu anasema lake, baadhi yao walisema mwanangu Hy Ni bahati ya mtende...we utakuwa umependwa na jini na Mara nyingi majini wa hv, ukienda nao sawa watakupa utajiri wa kufa mtu. Nikabaki nashangaa...wakaendelea kusema, watu wanakesha kwa waganga na kuvaa mipete 10 kwenye vidole ili wawaite majini Hawa, ila ww amekufwata mwenyewe kazi kwako baba. Baada ya kusikia hvy ndo walizidi kunivuruga, walitegemea nitafurah badala yake ndio wameniongezea hofu.

Lakini mmoja alikuja na wazo tofauti na wengine hili kidogo lilinitia Moyo. Akasema huyo msichana itakuwa anakujua vzr na anakufwatilia kitambo, hz anazokufanyia Ni drama tu. Kutakuwa Kuna mtu wako wa karibu Ana mpa taarifa zako muhimu tegemea vingi baadae, nimapema sana kusema Ni jini maana kwa alichokifanya hata binadamu wa kawaida anaweza kukifanya Ni Jambo la kujipanga tu.

Sikutaka kuendelea kuwasikiliza, nikarudi zangu dukani. Muda wa kufunga ulipofika nikawa nafunga, Kuna jamaa mmoja akaniuliza hz nguo alizonunua umeziacha humo dukani nikamjibu ndio, akashauri Ni vyema ukazitoa maana Kama Ni jini Kweli zinaweza kuwa 7bu ya biashara yako kuharibika.

Nikafanya Kama alivyoshauri. Nikiwa kwenye gari kuelekea nyumbani, sio Siri Nilikuwa na mawazo sana, Kama Kweli itakuwa Ni jini kwa Nini aje kwangu? Ikiwa sinaga tabia ya kwenda kwa waganga ya kiufupi mm Ni mkristo kamili sijawah fanya shriki katika maisha yangu..na atakuwa anataka Nini hasa.

Nikafika nyumbn nikafanya majukumu yangu Kama kawaida nikaingia kulala...ila usiku nilipolala nikaota njozi za mwanamke yule yule aliekuja dukani na kununua nguo, hlf hz nguo alizoninunulia ndio Nilikuwa nimezivaa ndotoni..tupo kwenye bustani kubwa nzuri ya mauwa pembeni Kuna mifereji ilikuwa inatiririsha maji masafi sana ila yalikuwa na ubaridi sana, Akawa ananilazimisha tuoge nikamwambia siwez kuoga maji ya baridi hvy, akaniambia utazoea tu, maana hapa tulipo ndio maji tutakayokuwa tunatumia siku zote. Alinilazimisha sana nikakataa...akawaananikimbiza ili niingie humo ndani ya maji,....nikastuka kutoka usingizini Moyo ulikuwa unanienda mbio mno, nimewah ota ndoto nyingi za kutisha lkn ile niliamka Ikiwa Kama Kweli mtu aliyetoka kukimbia nimechoka na mapigo ya Moyo yako juu.

Siku lala tena nikaamka kujiandaa kwa ajili ya kwenda kwenye shughuli zangu maana ilikuwa mida ya Kama saa 12: 40 alfajir na sio kawaida yangu kuamka mapema hvy. Labda niwe na Jambo maalum nataka kufanya. Ile natoka bafuni naangalia simu nakutana na sms namba Ni ile ile ya Jana.

" Pole sn mme wangu najua umechoka, Leo vaa zile nguo nilizonunua Jana najua utapendeza, nitafurah ukiniitii, asubuhi njema mume, nakupenda".

Nikastuka sana, nikapiga ile namba ili Ni mwambie kwa Nini anafanya vitu vya ajabu hvy...na ile pole alionipa ni ya nini? Simu ikawa haipatikan...kiukweli sikutaka kabisa kuvaa zile nguo...nikawa nachagua nguo nyingine kwenye kabati ili nizipasi nivae niondoke..sijamaliza zoez umeme ukakatika. Nikapigwa na butwaa...nilijaribu kuwaza inaweza kuwa ni michezo yake pia...ila nafsi ina kataa kila nguo ninayo iangalia imejikunja haifai...nikawa Sina jinsi, nikavaa zile nguo nilizokuja nazo Jana yake. (Yan alizonunua)

Hapa ndio mateso yakipoanzia...ilikuwa tarehe 28 nakumbuka siku ya ijumaa. Baada ya kuvaa zile nguo...mm huwa natumia perfume inaitwa Michagany kwa wale mnaoifahamu nakumbuka kabisa nimetoka nimejipulizia perfume yangu ya siku zote, ila nilipofika kwenye gari najisikia nanukia harufu tofauti kabisa..Tena Kali, nikawanajiuliza imetoka wapi? Na nikirudisha kumbukumbu ile ile anayotumia yule binti. Hapa ndipo nilipojua Kweli yule sio mwanadamu wa kawaida.

Sikutaka kumshirikisha yoyote juu ya kinachoendelea, siku Hy biashara haikuwa nzur kabisa, mida ya Kama saa 7 hv mchana, akaja mbaba mmoja akanunua nguo za Kama laki mbili na nusu hv...Tena alionekana anaharaka Kama mtu anaetaka kusafir nae hakuomba discount baada tu ya yule baba kuondoka, simu yangu inaita..siku tazama namba kwa makini nikapokea Mara nasikia sauti ya yule mwanamke.
Hakunipa nafasi ya kuongea, alisema hv..." Nimefurah sana Leo mme wangu umependeza sana mpk nataman niwe pembeni yako muda wote nisije nikaibiwa...huku anacheka.. akaendelea kusema nakutumia zawadi yako soon...akanibusu Kisha akakata simu. Kumbuka maneno yote hayo anaongea hakuna hata moja nimejibu, nimebaki kuduwaa tu. Baada ya hapo simu ikawa haipatikan. Jasho lilikuwa linanitiririka Kama maji Ikiwa ofisi yangu ina feni zaidi ya moja na zina nguvu za kutosha. Baada ya Kama dk 5 hv...sms ya tigo pesa ikaingia kwenye simu yangu. Nimetumiwa 320,000 jina la alienitumia Ni Mwanaisha Mohamedi...namba Ni tofauti na ile inayonipigia...kupiga ile namba inaita tu...haipokelew.

Vioja Ni vingi sana...kasheshe ilikuwa tarehe 31 Dec siku ya mkesha wa mwaka mpya. Narudi wacha nipumzike kidogo.

Inaendelea.......

Sehemu ya Tatu

Baada ya sms ile ya tigo pesa...nikajaribu kupiga ile namba iliyotuma pesa simu haikupokelewa. Mwishoni nikaamua kuacha nayo. Nikaona mambo yanazidi kuniwia magumu, nikaona kabisa Tatizo linaenda kuwa kubwa, ikabidi nichukue simu nimpigie mama yangu, nikamuelezea ilivyokuwa kuanzia mwanzo wa tukio mpk hatua tuliyofikia, kiukweli mama yangu aliogopa sana, ingawaje hakuonesha wazi zaidi ya kunitia Moyo na kuniasa nimuombe Mungu bila kuchoka lkn pia, nitafute mtumishi wa Mungu anifanyie maombi maalum.
Ila nilimuonya sana mama yangu, asije akamshirikisha hiyo ishu mtu yoyote mpk nitakapo mpa ruksa ya kufanya hvy, kwa 7bu anaweza ndio Akawa anaongeza Tatizo na sio kulipunguza.

Mama alinielewa, ila akanishauri si vyema kuendelea kukaa dukani kwa kipindi kile yanaweza kunikuta makubwa zaidi ya Yale. Siku hiyo ilikuwa ijumaa nilimpigia simu mdogo wangu anaeishi maeneo ya kigambon aje kunishikia Kuna dharula nimepata, Mara nyingi anakuwaga yy kipindi mm sipo nimetoka kwa mambo yangu mengine. Mpk kufikia mida ya saa 10 jion alikuwa ameshafika nikamkabidhi duka na kurudi zangu nyumban. Sikuwa na furaha siku Hy, nilikuwa nawaza mambo mengi nisiyokuwa na majibu nayo, nikiwa kwenye gari mdogo wangu akanipigia simu kuwa Kuna mgeni wangu pale dukani, nikamuuliza Ni wa kike au wa kiume, akanijibu ni wakike, nikastuka! Nikamuuliza amesema anashida gani, akasema amekuja kuchukua mzigo wake alikuachia ww Jana...akasema umtunzie atakuja kupitia.

Hapo ndio nikachanganyikiwa kabisa, inawezekanaje. Huyu dada atakuwa anataka nini. Niliishiwa pozi, nikakataa simu, baada ya muda kidogo simu ikaita Tena ila sikupokea. Ikumbukwe nguo anazohitaji ndio nimezivaa wakat huo, na niyeye ndie aliesema ameninunulia iweje aje na kuzidai Tena, ina maana Hawa Ni watu tofauti? Je huyu anae nipigia simu Ni Nan? Na maswala ya nguo kayafahamu vp! Nilibaki na mshangao, nikiwa kwenye dimbwi zito la mawazo, sms ikaingia kwenye simu yangu, kuisoma nakuta imeandikwa .." Nakupenda ila usisubutu kuniepuka, Kama unampenda mama yako, fwata nitakacho kwambia, kesho njoo feri saa 7 mchana upande wa kigamboni ukiwa umeziweka hizo nguo kwenye mfuko, uje kunikabidhi nimpelekee niliemkusudia.
Baada ya ujumbe huo, nikastuka sana hapo hapo nikampigia simu mama, nikamuuliza uko salama? Akasema ndio...akaniuliza Kuna nini, nikamjibu hakuna kitu, najua mama yangu anapresha pia ananipenda sana, hapendi kusikia nateseka...ila nikaendelea kumsisitiza juu ya Jambo nililomwambia kuhusu huyo mwanamke anayenifatilia asisubutu kumwambia mtu yoyote. Hii siku niliumia sana...tuwapende sana mama zetu mama alilia sana, akaniambia mwanangu kuwa makini wanataka kukuuwa, nikawa namwambia asijali hawawez niua, naamini Mungu yuko nami. Sikutaka kuendelea kusikia mama yangu akiangua kilio kwa ajili yangu. Niliwaza mambo mengi sana siku Hy, ki ukweli ilikuwa Ni siku mbaya kwangu. Nikamtumia sms mdogo wangu nikamwambia mwambie huyo dada aondoke nitawasiliana nae...akanijibu ameshaondoka muda mrefu amesema atakutafuta kwenye simu nikamjibu poa.

Nilifika nyumbani, nikaingia bafuni kaoga..nilivyorudi nikawa nimejilaza kitandani...nikapitiwa na usingiz mzito sana..nikiwa usingizini nikaota tupo kwenye ile ile bustani ya Jana tuliyokuwa tunalazimishana kuoga, Ila wakat huu haikuwa, hivyo wote tulikuwa tumevaa nguo nyeupe, mm nilivaa mavazi Fulani hv meupe mfano wa kaunda suit na yeye alikuwa amevaa Yale mavazi Kama ya kihindi ila nimeupe kabisa, tulikuwa tunakula na kunywa, yalikuwa ni matunda ndizi, apples, zabibu na vitu Fulani hv mfano wa tende ila ile juice ilikuwa Ni nyekundu Kama mvinyo hvy...

Tukawa tunacheka na kufurah sana, akaniambia Fulani....(Akataja jina langu) akasema Nilikuwa nakupenda kitambo...ila Fulani (Akataja jina la x girlfriend wangu) tuliekuwa tumeachana Kama miez nane iliyopita, kwamba yule ndie aliekuwa akiniekea vikwazo..nikamuuliza kwa nini, akasema alikiwa mtu wa dini sana, (Ni Kweli nikipata mdada alikuwa mlokole na mtu wa maombi sana yeye na kanisa kila wakati) hukumbuki hata sababu ya kuachana kwenu ilikuwa ni pombe alizokuwa anakukataza usinywe lkn pia ukawa unataka mfanye mapenz yy akasema hayuko tyr mpaka mpaka utakapo muoa? Na we ukamwambia hauko tayar kuoa kwa muda huo Ni heri muachane kuliko kuendelea kuwa na mpenzi jina mnaishi Kama kaka na dada, Nikawa nashangaa sikumjibu kitu.....Akacheka sana huku akinibusu kwenye paji la uso...akaniambia we ndio mume wangu mtarajiwa, ila kuanzia Sasa hata mm sitak unywe pombe...sitak uwe na mwanamke mke mwingine tofauti na mm...akaendelea kusema mpenzi mm Nina wivu sana, pia Nina hasira...na hasira zangu Ni mbaya sana, naweza kukuharibia kabisa maisha yako, tafadhali fuata nilichokuwa utanufaika na vingi sana. Sikumjibu kitu pia nikawa nimeshikwa na bumbu wazi akaniambia tusimame Kuna kitu nataka kukuonesha, tukatembea Kama mwendo wa dk tatu....Akaniambia unapaona kule...akanionesha kwa kidole kwa mbali nikamwambia ndio, kuna nyumba nzuri sana zimepakwa rangi Kama ya dhahabu, akaniambia kule Ni kwetu mpenz mm na wewe, tukishakuwa mke na mume tutaishi kwenye zile nyumba kule. Baada ya kuniambia hvy akanikumbatia huku akinibusu maeneo ya shingoni...nikastuta, kuangalia simu ilikuwa ni usiku sana mida ya Kama saa 8 hv usiku. Nikasali sana usiku ule nikalia sana, hafla nikasijikia kichefu chefu na tumbo kunivuruga sana, nikatapika vitu Fulani hv vyeusi sana vinatoa harufu mbaya mno.

Sikupata usingiz mpaka kunakucha, nikawa najiuliza ile ndoto ina maana gani hasa, ina maana nimeshafunga ndoa na jini? Nikaona hapana...alikuwa ananilisha Nini ambacho kilifanana na matunda kupelekea kutapika kiasi kile! Huwez amini nilishikwa na hasira Sana asubuhi ile.

Ikumbukwe siku hiyo ya J.mosi tarehe 29 ndio yule dada anataka tuonane feri nimkabidhi nguo zake ambazo tayari nilikwisha zivaa, tukutane pale saa 7 mchana, nilichoshangaa kwenye ndoto hakuzungumzia kabisa swala lile...nikajiapiza sitomwogopa Tena na tukionana nitamwambia sitaki anifwatikie Kama Ni ele zake sijatumia hata Mia, na Niko tayar kumrejeshea ili mradi aachane na maisha yangu niwe na amani.

Ilipofika mida ya saa 5 hv asubuh safar ya kwenda feri ikaanza nikiwa na mfuko niliweka zile nguo na Wala sikuzifua..nlipofika feri pale posta nikaa sehemu nasubir saa 7 ifike ili nipande panton...nikijaribu kupiga ile namba yake inaita lakini haipokelew, ilipofika Kama saa 7 kasoro dk8 hv, sms ikaingia nimefika njoo nakusubiria. Nikakataa ticket ya kupanda panton kwa ajili ya kuja upande wa pili wa kigamboni....Nilikuwa naangaza macho kila mahali kuangalia Kama yupo karibu yangu...sikumuona, tulipofika wakat tunashuka hamadi nakutana na gari nyeusi aina ya kulga inapiga honi mbele yangu naona mkono umetolewa nje upande wa dereva kuashiria nimpe kitu na Nilikuwa karibu nalo...kuchungulia hv, Ni yule yule mwanamke...alionesha ishara ya kuhitaj ule mzigo nilivyomkabidhi akafunga kioo(vilikuwa tinted)..gari ikaanza kutembea taratibu kuelekea kwenye panton, nilikaa pale getini wanapouzia viatu vya kike nikiwa nachungulia lile gari mpk linaingia kwenye panton, simu yangu ikaita Tena...kuangalia Ni yeye...alisema tu Ahsante mpenzi akawa anacheka, kabla hajakata simu nikamwambia aniache na maisha yangu...nilimtukana sana siku Hy sijui nilikumbwa na Nini, sikumwachia hata nukta ya kuongea..kuja kuangalia simu hv...muda mrefu ilisha katwa, Ni Kama nilikuwa naongea mwenyewe.

Kimbembe...siku ya tar 31 mkesha wa mwaka mpya, tulikuwa tumepanga kwenda mkesha uwanja wa taifa na rafiki yangu, mchana alipiga simu nyingi sikupokea...akatuma sms akaniambia najua unachotaka kufanya olewako uende huko unakotaka kwenda, nitakuonesha Mimi Ni Nani. Nikatuma sms mfululizo za kumtukana sana, nikamwambia asinitishe, asinipangie Cha kufanya...naweza kufanya Jambo lolote ninalijisikia...hakujibu kitu, ilipofika jion kichwa kiliniuma sana...naweza sema sijawah umwa kichwa kiasi kile jamaa tuliyepanga nae kwenda alikuwa anapiga simu sikuweza hata kupokea, nikiwa katika maumivu makali kuangalia hv mbele yangu namuona live...amechukia sana, nilipiga kelele lakini sauti haikutoka..nguvu ziliniisha...kuna mambo aliongea siwez kuweka hapa nahofia usalama wangu, Jamani nipo kwenye kiapo kibaya sana...Kama Kuna mtu anajiamini anaweza niepusha na haya majanga anisaidie tofauti na hapo, naweza potea Mimi, mama yangu pamoja na huyo atakaenisaidia endapo atashindwa nguvu na huyu jini. Siwez kuendelea kuelezea chochote, nipo kwenye kiapo kizito sana hapa ninapongea Nina alama kwenye paja langu la kushoto...wanaojua haya mambo nafikir wanafahamu hiyo alama ina maana gani kwenye jamii hz za majini. Nipo kwenye kitanzi sijui nachomokaje!

Nahitaji msaada wenu wa dhati ndugu zangu. Zile nguo nilizompa nilifanya kosa kubwa sana.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umenikumbusha niliwahi vagaa mrembo kariakoo kitimtimu kwenye kulala baada ya wiki..nikataka kuzima taa nilichokiona sitokaa nisahau mpaka nakufa..haya mambo yapo jamani..omba sana mungu, naona dalili za kufilisika kwako' be very careful..mm huyo msichana hata sijui ilikuaje ila nilikutanishwa na mtu ambae akataka kunitambulisha kwa huyo bi dada mwenye maduka kariakoo..ili tufanye joint venture..nimeteseka mnooo kuanzia 2016..ipo siku ntakuja na mkasa wake, ila naona downfall yako..si mtu mzuri huyo!
 
Huwa napata tabu kumuelewa kijana tena anaejitanabaisha kuwa wa kiume..

kwanza, akitumia emoji katika maandishi yake

Pili, kukatisha maneno eti '7bu'..sasa hako ndio kakitunguu swaumu gani?

Anyway..hapo njia panda unafanya nini saivi? Au ndio unakula mavitunguu swaumu ili uje uendelee?
Anavunja nazi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umenikumbusha niliwahi vagaa mrembo kariakoo kitimtimu kwenye kulala baada ya wiki..nikataka kuzima taa nilichokiona sitokaa nisahau mpaka nakufa..haya mambo yapo jamani..
Nafikir ww unaweza kunielewa Ni kitu gani nazungumzia Ni wiki mbili tu, ila mambo ninayo kutana nayo...sijapata kuona maishani mwangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umenikumbusha niliwahi vagaa mrembo kariakoo kitimtimu kwenye kulala baada ya wiki..nikataka kuzima taa nilichokiona sitokaa nisahau mpaka nakufa..haya mambo yapo jamani..omba sana mungu, naona dalili za kufilisika kwako' be very careful..mm huyo msichana hata sijui ilikuaje ila nilikutanishwa na mtu ambae akataka kunitambulisha kwa huyo bi dada mwenye maduka kariakoo..ili tufanye joint venture..nimeteseka mnooo kuanzia 2016..ipo siku ntakuja na mkasa wake, ila naona downfall yako..si mtu mzuri huyo!
Ilikuwaje mkuu....
 
Huwa napata tabu kumuelewa kijana tena anaejitanabaisha kuwa wa kiume..

kwanza, akitumia emoji katika maandishi yake

Pili, kukatisha maneno eti '7bu'..sasa hako ndio kakitunguu swaumu gani?

Anyway..hapo njia panda unafanya nini saivi? Au ndio unakula mavitunguu swaumu ili uje uendelee?
Watu wa aina yenu kwenye jamii hamkosekani, hvy sishangai ila nivyema kuangalia content ya mtoa mada kuliko hvy vitu vingine haviwez kukusaidia kitu...zaidi Ni kudhihirisha namna gani una upeo mdogo wa kufikir

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nafikir ww unaweza kunielewa Ni kitu gani nazungumzia Ni wiki mbili tu, ila mambo ninayo kutana nayo...sijapata kuona maishani mwangu

Sent using Jamii Forums mobile app
Bora hata wewe umestuka mapema, mm nimnywaji wa pombe yani story yako zinaendana somehow na yangu..mpaka usingizi umekatika..nilikua kila nikikaa nae jionj nikitoka kibaruani naona mauza uza ya kishenzi..siku alipotaka tukalale tukapiga kinywaji akasema muda umeenda twende kwangu ulale asubuhi uamke uende kazini..

aiseee! Pombe ilikata..nikakurupuka nikawa naanza kuvaa nguo..ardhi ya mule chumbani ikawa ina cheza cheza..inshort nilipotaka taa izimwe alinyoosha mguu na mpaka switch ilipo ni parefu kwenye kale kagiza nilimuona akibadilika uso mara sura hii mara ile nikawasha taa..alinibadilikia..nikalazimisha kuondoka kwani nilifika mbali sasa? Kitu cha fisi wawili wananifuata..giza totoro..milio ya wanyama..hapo ni mikocheni b dsm..

ukiwa kijana una kipato na una muonekano flani ni shida sana..mungu akutangulie brother, natamani tuonane ! Hapa nahema nikiwaza nilivoteseka, kazi nikapoteza na aliniapia wakati namkataa nilimwambia sikuelewi..yani dahh nakuonea huruma..af hua wana access na simu wanajua unawasiliana na nani..
 
Huwa napata tabu kumuelewa kijana tena anaejitanabaisha kuwa wa kiume..

kwanza, akitumia emoji katika maandishi yake

Pili, kukatisha maneno eti '7bu'..sasa hako ndio kakitunguu swaumu gani?

Anyway..hapo njia panda unafanya nini saivi? Au ndio unakula mavitunguu swaumu ili uje uendelee?
kuna sehemu yeyote imeandikwa Wanaume tusitumie emoji?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom