Daah wakuu inaniuma sana kukosa nafasi kwenye hiki chuo cha wanyamapori Pasiansi. Ni chuo nilichokuwa napenda kwenda kusoma ila ndio basi tena nmekosa nafasi ya kuchaguliwa na sijui nifanyeje. Kwa wazoefu wa hiki chuo je kuna uwezekano wowote kukawepo na awamu ya pili ya majina? Maana kwenye guidebook ya NACTE inaonyesha kozi niliyoomba wanahitajika wanafunzi 200+ ila majina yaliyotoka yana wanafunzi 60+. Wakuu nipeni msaada wa nini cha kufanya, shukran