NIMEKOMA kushobokea vi-offer mbuzi! (My Bad Friday Night)

Unge kubali akupeleke bar ya kawaida tu! Maana huyo sharo kakusoma kaona akikwambia pakawaida unge kataa!

Lakini imani za kioga zimemponza na kushauri umwambie na yeye atafute na yeye kiasi kidogo!


Mtu nimemwambia chagua!!!! Sababu ndio utaratibu, msaada haunaga risiti, anaetoa ndo anapangia pa kwenda! Naona alinipima, akakuta anapima kina cha bahari kwa mguu. Hahahaaaaaaaa! Ila as a man namuhurumia kweli, his EGO itakuwa ICU by now!!!! Natamani hata nimpigie nimwambie its okay, sijamind! Ila nikikumbuka SHOTI aliyonitia wacha EGO iende mochwari LOL!
 
1. Mazungumzo ya nanai atalipa bill ni muhimu kufanyika kabla ya ki date.

2. Ni muhimu kujua kama si bei kamili ya chakula na vinywaji wakati unatoa order, bali hata a round figure.

3. Kamwe usile kitu ambacho huwezi kulipia kwani kistaarabu hata kama angeweza kulipia bill yote, siku nyingine ungetakiwa kumtoa yeye (dada zetu bongo sijui kama mila hii imefika huko) na ukishindwa kulipiza itatoa sura si nzuri.

4. Pia ni muhimu kujua uwezo wa kulipia kabla ya wakati kwa sababu mnaweza kuagiza vinywaji kwa raundi, sasa itakuwa aibu mwenzako akiagiza raundi nenda raundi rudi na wewe umebung'aa tu, unajifanya mwanamke wa kileo (unless mshakubaliana kwamba wewe si mwanamke wa kileo) wakati huwezi kanuni ya reciprocity.

Kiranga naona uko nje ya nchi!!!! Nchi hii ni ile ile uliyoiacha, mwanamke yeye kubunyaa tuuuuu, bila kuwaza bili. wanaume wetu wa kibongo wa ukweli sanaaaa (Kamwee sichukui mzungu) na washatuzoea kuwa sisi ni waroho afu wachoyo kinoma, wanaenda na sisi hivo hivo kibingwa.


Bei ilibidi mlipaji aulize, au hata angeomba menu, sasa yeye kauchuna, basiii ndo tukaio likatukuta.

Ila namuhurumia sana AS A MAN HIS EGO MUST HAVE BEEN VERY HURT!!!! HADI LEO EGO ITAKUWA ICU! (Msimuhurumie sana, mie mwenye shoti ndo mnihurumie, manake kesho itabidi nikajitoe muhanga kwa Boss Diaspora kisipoeleweka)
 
Peopleeeeeeeeeessss! (Wakubwa zangu shikamooni)

Natumai wote wazima, na hakuna alieshikwa kwenye maandamano sababu wengi wenu wazee WAKUJIKAUSHA na kufatilia kwenye tv. (With the exception with fazaa, sijui kama umepona mpambanaji wa ukweli) Mie mzima nimetoka kwenye upambe nuksi wa uchaguzi wa Wanawake wa CCM huko (lazima nijikombe viti maalumu mchezo!!!) na mgombea wangu kashindwa, anyway sio mwisho wa dunia, tunajipanga upya. Life has to go on.

Kubwa lilinonileta hapa ni tukaio lililonikuta ijumaa jioni, Daaaaaah! Acheni tu! Almanusura nipewe MITAICHI, TAIKONDO, JUDO, KARATE, SUMARAI, KUNGFU, SUMO NA KICK BOXING KWA MPIGO!!!! Chezeya wachina nyie.

Ishu ilikuwa hivi, mchaga kasafiri kikazi sasa nikaona kuwahi kulala ijumaa kwa sie wanywaji ni zambi, so nitafute mishe mishe za japo kupunguza kiu kwa tuhenken tuwili ili nisiamke na hangover. Basi kuna sharo flani hivi aliniofferga dinner , nikawa sisomeki kwenye radar, sasa kila nikikutana nae inakuwa kama deni vilee, haishi kuniinvite over n over. Nikaona nimtafute tukapunguze mawazo kidogo. Basi nikamuuliza if the offer still stands akasema yah! Tukaonana tayari kwa dinner.

Akaniuliza ungependa kwenda wapi? Nikamwambia chagua weye! (Maksudically sabab yeye ndo anajua ana bajeti gani, itatosha wapi, alaf hawa masharo wasumbufu sana, ukimpeleka uswazi anaweza kukushusha bure) Akangangania bana chagua mwenyewe(mie ndo nichague) Mimi nikachgua bana, twende kwenye kisehem flani cha wachina nasikia wanauza wine na liquor za China, Taiwan na Hongkong. Akakubali banaaa. Kufika ushamba mzigo, nikamuuliza mhdumu whats is the favourite ya wengi hapo, akanitajia nikamwambia tuletee. Inapimwa kwenye tuglass tudogo, sie tunatirishia tumboni tu. Ni tamu kusema kweli, magnificient! Glass moja yaanzisha ingine.

Midamida tukaitisha bili basi, sharo kuona bili sura ikamsawajikaaa! mie kimyaa!,Mara akanigea nikaitazama, ni nomaaa! Kumbe the shit was damn expensive!!!! Ila nikanyuti sikusema chochote. Basi ndo kuniambia kwa upole, i cant cover this bill, nina shoti!!! Mtumeeeeeeeee! Na mie ndo sikubeba pesaa! Chupi ilinibanajeeee! Nikajikaza kibingwa nikamwambia toa basi uliyonayo, Ndo kunipa robo ya bili!!!!!!!!! Nikaona huyu anatka anichakachue, mwenyewe wa kitaa vile vile, nikamwambia Mimi natoa pesa ya nusu yangu tuuu, we hiyo robo iliyobaki utajiju! Nikaza kwenye kitita cha ofisi nikakwapua kadhaa, kumcheki huku mtu chozi linamlengalenga. Nikaona aibu za nini nikamuita muhudumu, nikamlipa bili yote. Sema ndo kanitia SHOTI KUBWAAA! HAIKUWA MPANGO!!!! Tukaondoka kimyakimya, njiani analeta story za ILL MAKE IT UP TO U!!!!( He will make it up to me My As*) I SO SORRY! Blah! Blah! Blah!

Hapa najamba jamba kupata pesa ya kujazia kitita cha ofisi kesho ndo kesho!!!! Na uchaguzi ndo tumepoteza, najihisi malaria, sijui nimwambie nini mchaga anitumie hizo MBESA za watu.

Dada LARA I umekamilisha jpili yangu vyema...huwa si-miss post zako..
 
Last edited by a moderator:
Kiranga naona uko nje ya nchi!!!! Nchi hii ni ile ile uliyoiacha, mwanamke yeye kubunyaa tuuuuu, bila kuwaza bili. wanaume wetu wa kibongo wa ukweli sanaaaa (Kamwee sichukui mzungu) na washatuzoea kuwa sisi ni waroho afu wachoyo kinoma, wanaenda na sisi hivo hivo kibingwa.


Bei ilibidi mlipaji aulize, au hata angeomba menu, sasa yeye kauchuna, basiii ndo tukaio likatukuta.

Ila namuhurumia sana AS A MAN HIS EGO MUST HAVE BEEN VERY HURT!!!! HADI LEO EGO ITAKUWA ICU! (Msimuhurumie sana, mie mwenye shoti ndo mnihurumie, manake kesho itabidi nikajitoe muhanga kwa Boss Diaspora kisipoeleweka)

Halafu nyie mmekosea.

Inabidi mngeuliza kabla, wachina wengine wachakachuaji mpaka kwenye menu, wakikuona unaingia kichwa kichwa kuagiza bila kuulizia bei wanaweza kukupa bei za uongo.

Basi mie nilivyosikia unaanza na habari za mkutano wa UWT na mgombea wako kashindwa bado kidogo nifikiri "huyu ndo Shyrose nini" (joking).
 
Hiyo bill ya watu wa2 halafu mwanaume anashndwa kulipa duh! Tena anadrive?am sure ni usiku ryt? Kwasabab hata kama ni dadys kid si angetoka nazo huko kwao? Huyo muache tu hiyo ego iplumet hadi kwenye visigino ndo ajifunze!
 
Halafu nyie mmekosea.

Inabidi mngeuliza kabla, wachina wengine wachakachuaji mpaka kwenye menu, wakikuona unaingia kichwa kichwa kuagiza bila kuulizia bei wanaweza kukupa bei za uongo.

Basi mie nilivyosikia unaanza na habari za mkutano wa UWT na mgombea wako kashindwa bado kidogo nifikiri "huyu ndo Shyrose nini" (joking).


Sio wachina tu..
hata wabongo...
hasa kama wanaona mwanaume uko kwenye mtoko..
kuanzia dereva taxi,bar maid mpaka wahudumu wa hotel/gesti..
wote wana 'kubamiza'
since wanaona watu wengi akiwa na mwanamke wanajifanya hawajali matumizi..
kila mtu anakutajia bei yake lol
 
Halafu nyie mmekosea.

Inabidi mngeuliza kabla, wachina wengine wachakachuaji mpaka kwenye menu, wakikuona unaingia kichwa kichwa kuagiza bila kuulizia bei wanaweza kukupa bei za uongo.

Basi mie nilivyosikia unaanza na habari za mkutano wa UWT na mgombea wako kashindwa bado kidogo nifikiri "huyu ndo Shyrose nini" (joking).

Hahahaaaa! Itakuwa walitupa bei FEKEROOOOOO! Shyrose tulikuwa kambi moja ya Jimama la Same, kanunaje sasa!!!! Acha tu usinikumbushe!!!! Ila Kina Rose wenzangu wakubwa kwenye chama sie ndo visisimizi huku! LOL!
 
Sio wachina tu..
hata wabongo...
hasa kama wanaona mwanaume uko kwenye mtoko..
kuanzia dereva taxi,bar maid mpaka wahudumu wa hotel/gesti..
wote wana 'kubamiza'
since wanaona watu wengi akiwa na mwanamke wanajifanya hawajali matumizi..
kila mtu anakutajia bei yake lol

Wewe unalitatuaje hili! Manake nakuaminia kwa solution za KIVITA!!!!! Kwa manufaa ya wengi, mwaga vituz.
 
Wewe unalitatuaje hili! Manake nakuaminia kwa solution za KIVITA!!!!! Kwa manufaa ya wengi, mwaga vituz.


the number one rule ya mtoko ni hii kwa mwanaume

Usimpeleke mwanamke sehemu ambayo wewe mwenyewe hujawahi kwenda...
mpeleke sehemu familiar ambayo sio tu unajua bei zote
iwe ni sehemu ambayo unajua mpaka bar manager jina lake
na yeye anakufahamu,
hata ukiishiwa au hata kupoteza wallet...hakiharibiki kitu..
hapa nazungumzia first date...
 
Weeeeeeeeeeeeeeee... kwani huyo "mushaga" anaifanyaje? anakula kwa macho?

UNUSED kwa wengineeee! LOLEST! Mwanaume yoyote ukimwambia mie unused, atakungojea hata karne ilihali apate golden chance ya kukata ribbon!!!! LOLEST! Na sie used ndo TUNAPONEA hapo hapo, coz u never know till u know kama kweli ipo au kushney babu G!!!!!!
 
Hapa najaribu kuomba donations kwa wana CDM sababu CCM nilishalikoroga na team yangu ndo tumebwaga, lasivo tungeshinda ningekuwa nachukua gawio la upambe nuksi!!!! Chonde chonde watanzania wote ni ndugu! LOL!

Hili ndilo tatizo la upambe, hasa huko ccm, nimeambiwa almanusura umtwishe kiti mama nonino? lol

Michango toka kwetu utapata, tena kabla hujaomba tayari makamanda wameshatangaza kukulipia, bila umemsoma king kong na wengine wengi tu.
 
the number one rule ya mtoko ni hii kwa mwanaume

Usimpeleke mwanamke sehemu ambayo wewe mwenyewe hujawahi kwenda...
mpeleke sehemu familiar ambayo sio tu unajua bei zote
iwe ni sehemu ambayo unajua mpaka bar manager jina lake
na yeye anakufahamu,
hata ukiishiwa au hata kupoteza wallet...hakiharibiki kitu..
hapa nazungumzia first date...

Mmmmmmmmh! We ni nomaaaa! Je first date nikipropose mie mwanamke, unafoulishje hapo! (Sio wote Ozokoni na mfumo dume kama wewe, wengine ni wasikivu na wanapenda kuwafurahisha mabinti hivo toa mavituz situation ikiwakuta.)
 
lara 1 shosti nawe this time umechemsha, umetokosa na kutokota .....

TOKA LINI VISHAROUHARO VIKAFAA KWA VIDATE aka OUTINGS?????????
 
Last edited by a moderator:
Mmmmmmmmh! We ni nomaaaa! Je first date nikipropose mie mwanamke, unafoulishje hapo! (Sio wote Ozokoni na mfumo dume kama wewe, wengine ni wasikivu na wanapenda kuwafurahisha mabinti hivo toa mavituz situation ikiwakuta.)

Uki propose binti unatakiwa kuuliza maswali ya kizushi..
binrti akisema twende level 8,unauliza kizushi like hapo level8 beer wanauzaje?soda?
hapo unapata budget,ubaba pesa twice the budget just in case lo
 
Na ungempa kipapaa ukakopwa kabisa jumla bila riba, lol! Huna machale kabisa wewe. Mbona unasound mjanja unaingizwaje mjini kirahisi hivi hahaha
Mwenzanguuuuuu! Sharo kaniingiza KINGI na usafiri wa MDINGI wake, mi nikajua ANAJIMUDU!!!!!!!!1 Kumbe ushuzi mptupuu! NIMEKOPWA LIVE LIVE!!!! Nimenuajeeee! Nasonya kimya kimya tu hapa. LOL!
 
UNUSED kwa wengineeee! LOLEST! Mwanaume yoyote ukimwambia mie unused, atakungojea hata karne ilihali apate golden chance ya kukata ribbon!!!! LOLEST! Na sie used ndo TUNAPONEA hapo hapo, coz u never know till u know kama kweli ipo au kushney babu G!!!!!!

Hahahahaha kukata utepe kuzuri sana asikwambie mtu. Ngoja na mimi niendelee kuwa na subra huend one day nikapata hiyo golden chance, manake kuna mtu hapa JF ameniweka pending siku nyingi kweli kweli.
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom